Huyu mpenzi wangu simuelewi

Huyu mpenzi wangu simuelewi

Tatizo haweki
Kama unampenda give him some time utafurahia maisha usiteme JoJo kwa karanga za kupewa mkononi. Mimi wangu tulikaa hivyo miaka minne tena akiwa anafanya kazi na Mimi mwanafunzi wa chuo Mwanza to dar mwisho mambo yame tick tunafurahia maishaaa. Ila kama umependa kweli na sio masihara mjumbe.
misingi ya mapenzi yetu. Unajua kitu chochote kinahitaji misingi
 
Naomba msaada wa ushauri hasa wanaume.

Nilianza kuwasiliana boyfriend huyu kwa njia ya simu mwaka 2014 mwanzoni ambapo wote tulikuwa hatujuani tukawa tunapendana sana tumeendelea na mapenzi yetu ya simu hadi kufikia mwaka jana 2015 Decemba ambapo nilifanikiwa kusafiri hadi hapo alipo na tukajuana tukakumbatiana sana na kukakutanisha na miili yetu ambapo nililala kwake siku mbili.

Cha kushangaza nilidhani tulivyoonana ndo ingekuwa muda mzuri kwa mimi na yeye kupanga mikakati ya mahusiano yetu lakini haikuwa kama nilivyodhania. Alikaa kimya na kunisindikiza kwenda kupanda gari kurudi kwetu Njombe yeye akiwa Dar es Salaam.

Nilipata safari ya pili kwenda Dar nilifikia kwake na nikalal siku moja na kurudi kwetu bila mipango yoyote juu ya mahusiano yetu.Sasa nikwamba tunawasiliana kama mtu na mpenzi wake kwa miaka miwili sasa lakini haoneshi mwelekeo wowote wa kuwa ananihitaji in future na wala hasemi chochote na kila nikisema nataka kumuacha huwa hakubali.

Siku za karibuni nimepata mwanaume yuko serious kabisaaa anataka kunioasasa naogopa kumkubalia wakati sijajua hatima ya yule wa Dar ambaye hasemi chochote.Naomba kwa mlionielewa mnisaidie mawazo hapo nimpige chini huyo wa zamani nimkubali mpya mwenye nia na mimi au niwe mwaminifu hadi aniache huyo wa Dar?

Nawaza nakosa majibu tafadhali msaada
ukimpa na huyu wa sasa atakugonga afu atasepa, kuwa makini na kulambisha lambisha ovyo,kama una malengo ya mbali na huyo jamaa kaa nae muongee kiutu uzima , km unataka starehe tu, mpe mgegedo afu muendelee kupiga makitaimu..
 
usijeitaka ndoa kwa pupa bibie,,,, utarudi na talaka......tatizo wewe akili yako ni ndoa tuuu...ndoa si mchezo dada,,, ndoa si kuzaa wala kuduu pekee.... shauri yako.??? Njombe mpaka Dar.... kweli wanaume tunajua kuimbisha,,, hata nauli umetumia pesa yako,,, ulimletea magimbi?
 
Usikurupuke katika hili. Mi naamini wewe mwenyewe unawafahamu zaidi hao watu wawili kuliko sisi tunaoshirikishwa humu jukwaani. Jiridhishe kwa mapana zaidi ni yupi kati ya hao jamaa ni muoaji na yupi ni mgegeda papuchi tu. Swali la kiuchokozi; unapoenda Dar hua kanauli unajijua mwenyewe au kidume anasimamia show? Ila kiukweli kama ni mwaka wa pili kwenye mahusiano na hamjajua hatima yenu, kubali tu huyu wa dar ni mpitaji.
 
Sio hivyo kaka yangu, yaani hata kuongelea mambo yetu na kuweka misingi ya mahusiano yetu nayo inahitaji nini maana muda wa miaka miwili tulikuwa tunajuana ndo maana tukadumu muda wote huo. Cha kushangaa ndo hicho he doesnt care anything about our future

Na ndio maana nikakwambia inahitaji muda. Give him sometime kwa sababu watu wote hatuko sawa. Pengine wewe ungeweza kufanya hivyo mara baada ya kuonana kwa mara ya kwanza lakini si wote wanaweza kufanya hivyo kwa sababu watu wote hatuko sawa wala hatufanani kitabia.
 
Ni kweli yaani nampenda sana huyu wa Dar yaani hata sielewi kwa nini yeye hashtuki kuwa mi nalala namuota yeye ndo maana napatta nguvu ya kywakataa wengine kwa sababu nampenda sana yeye, Na analijua hilo lakinin hata hashtuki


Usiposhtuka mapema utakuja kuleta uzi unaomuhusu kwa aliyokufanyia! Heri nusu shari kuliko shari kamili ndugu yangu
 
Ha ha h ah ah mpendwa...ni shida sana kwa kweli!



Ila huyu ni heri awaache wote aje kwangu...tena mimi na nauli nitamtumia tumfanyie maombi! Nisaidie kumshauri hilo mpendwa.
Mmmh sio kwamba nawe unataka kukutanisha miili?
 
Hana mpango na ww huyo. Chukua 120 zako,maana naskia mnasema kuolewa zali siku hizi.
 
"..Kuna kitu anakihitaji kutoka kwa mwanamke, labda wewe huna hicho.. pia nadhani wanawake mmesahau kwamba wanaume sisi ni walewale miaka rudi miaka nenda"-utaolewa tu.
 
Naomba msaada wa ushauri hasa wanaume.

Nilianza kuwasiliana boyfriend huyu kwa njia ya simu mwaka 2014 mwanzoni ambapo wote tulikuwa hatujuani tukawa tunapendana sana tumeendelea na mapenzi yetu ya simu hadi kufikia mwaka jana 2015 Decemba ambapo nilifanikiwa kusafiri hadi hapo alipo na tukajuana tukakumbatiana sana na kukakutanisha na miili yetu ambapo nililala kwake siku mbili.

Cha kushangaza nilidhani tulivyoonana ndo ingekuwa muda mzuri kwa mimi na yeye kupanga mikakati ya mahusiano yetu lakini haikuwa kama nilivyodhania. Alikaa kimya na kunisindikiza kwenda kupanda gari kurudi kwetu Njombe yeye akiwa Dar es Salaam.

Nilipata safari ya pili kwenda Dar nilifikia kwake na nikalal siku moja na kurudi kwetu bila mipango yoyote juu ya mahusiano yetu.Sasa nikwamba tunawasiliana kama mtu na mpenzi wake kwa miaka miwili sasa lakini haoneshi mwelekeo wowote wa kuwa ananihitaji in future na wala hasemi chochote na kila nikisema nataka kumuacha huwa hakubali.

Siku za karibuni nimepata mwanaume yuko serious kabisaaa anataka kunioasasa naogopa kumkubalia wakati sijajua hatima ya yule wa Dar ambaye hasemi chochote.Naomba kwa mlionielewa mnisaidie mawazo hapo nimpige chini huyo wa zamani nimkubali mpya mwenye nia na mimi au niwe mwaminifu hadi aniache huyo wa Dar?

Nawaza nakosa majibu tafadhali msaada
Huyo mwamaume wa kukutangazia ndoa kwa kuonana siku mbili tu ni nani na wewe? Tulia uchunguzwe acha kwikwi
 
Huyo wa Dar hakupendi, inawezekana haukufikia matarajio yako Kama alivyokuwa anategemea. Hivyo hakuhitaji ila hataki tu kukwambia na kusema kuwa ukimwambia unamwacha anakusihi usimwache ni zuga tu, anajua unampenda na anaona akikubali kirahisi atakudisappoint. Anataka wewe mwenyewe uanze kuzoea taratibu kuwa hupendwi, na pengine upate mtu, halafu ujitoe mwenyewe. Wote mtakuwa mmeachana bila maumivu.
 
Dada angalia nani anakupenda kwa matendo yake.Kama huyo mpya anakupenda olewa tuu.Coz kwa maelezo yako unaonyesha unatamani ndoa.Huyo wa kwanza alikitumia tuu.Kwanza angekupenda usingemfuata dar mara zote angeshakujaga njombe.
Ushauri:Acha kufahamiana na wanaume kwa kuwavulia ,Kama anakupenda akajitambulishe kwenu akuoe.Kama huyo wa pili hamjafahamiana please msifahamiane hadi muoane.Sawa ee.
 
Back
Top Bottom