Ketoka
JF-Expert Member
- Sep 23, 2015
- 1,087
- 1,913
Habar wana jf
Bila kupoteza muda, nimewahi kuingia kwenye mgogoro na aliyekuwa mkuu wa mkoa x kipindi cha serikali ya awamu ya NNE ya JK.
Huyu mkuu amewahi kumuamrisha mkurugenzi wa Halmashauri ambayo nilikuwa naifanyia kazi kuwa nimekula fedha za mradi fulani ndani ya Halmashauri hiyo,
Nilisimamishwa kazi na maslahi yangu pia yalisimamishwa, kupisha uchunguzi, mwaka mzima nachunguzwa bila majibu sahihi, na ukumbuke mwaka mzima huo sipati mshahara wala posho, familia yangu ikatabika ile mbaya, watoto wakashindwa kusoma
Baada ya mwaka huo kuisha, wakaguzi wakaja na majibu kwamba sijakula hata senti moja ya mradi
Mwaka 2016 nikarudishwa kazini ila nikaomba kuhamishwa kwenda Halmashauri nyingine mkoa mwingine
Katika mabadiliko ya wakuu wa mikoa na wilaya yaliyofanywa na JPM, huyo mkuu wa mkoa kapigwa chini na Halmashauri niliyopo ndo anayokaa anafanya business zake
Sasa kuna zabuni imetolewa hapa Halmashauri na kuna maombi mbalimbali yanaletwa kwa ajili ya mradi huo
Huyu ambaye alikuwa mkuu wa mkoa naye ameomba mradi lakini hana sifa ya kupewa mradi, hakidhi vigezo vya kupewa mradi ila anapigiwa pande na mwenyekiti wa Halmashauri ananishawishi tumpe mradi. Cha kushangaza na yeye bila aibu ananipigia sim tumpe kipao mbele
Sasa nakaa nawaza hivi huyu mkuu anajua kuwa amewahi kuniachisha kazi kwa tuhuma ambazo si za kweli ,au amesahau au hanijui?
Mbona ananipigia simu na kuongea na mimi friendly sana?
Sasa najiuliza, nimpinge asipewe mradi maana hana sifa, au tumpe tu halafu nimkumbushe hicho kisa ambacho amewahi kunifanyia, au nifanyeje wakuu
Bila kupoteza muda, nimewahi kuingia kwenye mgogoro na aliyekuwa mkuu wa mkoa x kipindi cha serikali ya awamu ya NNE ya JK.
Huyu mkuu amewahi kumuamrisha mkurugenzi wa Halmashauri ambayo nilikuwa naifanyia kazi kuwa nimekula fedha za mradi fulani ndani ya Halmashauri hiyo,
Nilisimamishwa kazi na maslahi yangu pia yalisimamishwa, kupisha uchunguzi, mwaka mzima nachunguzwa bila majibu sahihi, na ukumbuke mwaka mzima huo sipati mshahara wala posho, familia yangu ikatabika ile mbaya, watoto wakashindwa kusoma
Baada ya mwaka huo kuisha, wakaguzi wakaja na majibu kwamba sijakula hata senti moja ya mradi
Mwaka 2016 nikarudishwa kazini ila nikaomba kuhamishwa kwenda Halmashauri nyingine mkoa mwingine
Katika mabadiliko ya wakuu wa mikoa na wilaya yaliyofanywa na JPM, huyo mkuu wa mkoa kapigwa chini na Halmashauri niliyopo ndo anayokaa anafanya business zake
Sasa kuna zabuni imetolewa hapa Halmashauri na kuna maombi mbalimbali yanaletwa kwa ajili ya mradi huo
Huyu ambaye alikuwa mkuu wa mkoa naye ameomba mradi lakini hana sifa ya kupewa mradi, hakidhi vigezo vya kupewa mradi ila anapigiwa pande na mwenyekiti wa Halmashauri ananishawishi tumpe mradi. Cha kushangaza na yeye bila aibu ananipigia sim tumpe kipao mbele
Sasa nakaa nawaza hivi huyu mkuu anajua kuwa amewahi kuniachisha kazi kwa tuhuma ambazo si za kweli ,au amesahau au hanijui?
Mbona ananipigia simu na kuongea na mimi friendly sana?
Sasa najiuliza, nimpinge asipewe mradi maana hana sifa, au tumpe tu halafu nimkumbushe hicho kisa ambacho amewahi kunifanyia, au nifanyeje wakuu