Huyu mdudu anaitwaje?

Huyu mdudu anaitwaje?

Aliniuma juzi juzi, ana maumivu makali pale alipokuuma na uvumba kiasi, pia unahisi kama vile una maumivu ya mishipa ya fahamu upande wa alipouma. Inachukua kama siku mbili hata tatu kujisikia kawaida. Sikutumia dawa yoyote mbali na kuweka barafu aliponiuma na kunywa maji mengi sana.
 
Habari wakuu,

Hapa nnapo ishi nimekutana na hawa wadudu mmoja ni mkubwa balaa na mwingine ni mdogo kama huyu, sasa nauliza hawa wadudu wanaitwaje je wanauma na akikuuma dawa yake ni nini na njia ya kuwazuia ni ipi.Nimewakuta wawili wapo karibu na shimo la maji machafu wanakula mende.

View attachment 696000

HABARI,
Huyo ni Tandu (Centipedes-Kwakiingereza na Kingdom yake ni ANIMALIA na class yao ni Chiloponda)
Wako wa aina nyingi sana wao hutaga mayai na kuyalinda kwa kuyakumbatia kwenye miguu yao mingi.Wapo wenye sumu na wasio na sumu.

Nchini China na Nchi nyingine za Asia hutumiwa kama chakula tena hutungwa kwenye waya au vijiti huku tunaita mishkaki au kuungwa na viungo vingine kutumika kama mchuzi na ni kati ya vyakula vyenye bei mbaya.

LUMUMBA
 
Huyo mdudu akikuuma kadri anavyo tembea ndivyo sumu inasambaa mwilini
Siyo kweli, akikuuma panakufa ganzi kwa muda baadae unakuwa sawa sumu yake siyo kali kama ya nyoka na wala hawana madhara sana kama watu wanavyotishwa
 
. Nilimuita mmoja eti akasema kama ni nyoka angekuja ila huyo mdudu hana shida nilale tu. Dada ndo alinisaidia maana mimi nilikua nishagoma kuingia ndani kulala.
Ahahah muoga.....eti angekuwa nyoka ningekuja,ingekuwa kweli nyoka huyo jamaa kama mnaishi nyumba moja kisha ukamwambia wallahi angalihama nyumba!
 
Back
Top Bottom