KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,214
- 56,855
Wala haitaji kutumia akili kubwa sana kumjua mchoraji mahili na mchoraji asie mahili.
Kama utakuwa ni mtu mwenye fikra pana na uonaji sahihi hakika utaona mchoro wake UMEPINDA!
Anataka aonekane yeye ni mchoraji makini kushinda waliopita huko ni kujitakia sifa ambazo hana na ni sifa hizohizo ndizo zinazomuangusha na kuzidi kupindisha mchoro wake dhahiri! Hakuanza leo wala jana tena alianza kwa maigizo yaliyovuta hisia watu,hakuishia hapo kwenye maigizo bali akaanza pia kufuta walipochora wengine akidai palikosewa kumbe yeye ndo anakosea na wala hajui.
Anachokifanya anazidisha yale makosa machache kuwa mengi! Na katika uchoraji wake anaiamini miwani yake ambayo hajui kuwa inamtoa nje ya mchoro.
Mchoraji anataka kuaminisha wacholewa kuwa mchoro anaouchora hivi sasa ndio mchoro unaotakiwa na ati wengi wamerudisha imani zaidi katika mchoro huo!
Hivi ni mchoro upi makini wenye kuchorwa kwa nguvu pasipo kutumia akili,na mchoro huo ukawa mchoro mzuri na halali?
Isitoshe hata zana za mchoro hazitumii ipasavyo! Panapotakiwa penseli yeye anachorea pen! Panapotakiwa rangi nyeusi ye anaweka njano!, kwenye blue anaweka kijani na alivyo mpenda sifa kaweka na rangi nyekundu ambapo ktk mchoro huo hapakutakiwa rangi hiyo!
Kaamua kuwafata wanaomshangilia na kuwaumiza ambao wanalia! Tena kawapa na jina wanaolia kawaita "wachoraji wa nje" mchoraji huyu anajikosesha Kisha anafuta halafu anasema Kuna mchoraji alichora vibaya Kisha anachora yeye tena!.. lkn haachi hivihivi ktk kurudia michoro yake huwatoa kafara wajakazi wake wadogowadogo.
Mchoraji huyu asipokanywa basi mchoro wake atauharibu zaidi maana mpk sahivi kauharibu nusu! Na kwajinsi asivyoelewa nusu iliyobaki ataizongorota si kifani! Na mumuambia walikuwepo wachoraji wazuri zaidi yake nao wamepita. Walikuwepo wachapa rangi wazuri zaidi yake nao wamepita! Kila anachokiona kitapita na ataviacha Sasa ni jukumu lake kuache vyema kuliko kuacha vibaya maana siku zote mwisho wa ubaya ni ubaya.
Kama utakuwa ni mtu mwenye fikra pana na uonaji sahihi hakika utaona mchoro wake UMEPINDA!
Anataka aonekane yeye ni mchoraji makini kushinda waliopita huko ni kujitakia sifa ambazo hana na ni sifa hizohizo ndizo zinazomuangusha na kuzidi kupindisha mchoro wake dhahiri! Hakuanza leo wala jana tena alianza kwa maigizo yaliyovuta hisia watu,hakuishia hapo kwenye maigizo bali akaanza pia kufuta walipochora wengine akidai palikosewa kumbe yeye ndo anakosea na wala hajui.
Anachokifanya anazidisha yale makosa machache kuwa mengi! Na katika uchoraji wake anaiamini miwani yake ambayo hajui kuwa inamtoa nje ya mchoro.
Mchoraji anataka kuaminisha wacholewa kuwa mchoro anaouchora hivi sasa ndio mchoro unaotakiwa na ati wengi wamerudisha imani zaidi katika mchoro huo!
Hivi ni mchoro upi makini wenye kuchorwa kwa nguvu pasipo kutumia akili,na mchoro huo ukawa mchoro mzuri na halali?
Isitoshe hata zana za mchoro hazitumii ipasavyo! Panapotakiwa penseli yeye anachorea pen! Panapotakiwa rangi nyeusi ye anaweka njano!, kwenye blue anaweka kijani na alivyo mpenda sifa kaweka na rangi nyekundu ambapo ktk mchoro huo hapakutakiwa rangi hiyo!
Kaamua kuwafata wanaomshangilia na kuwaumiza ambao wanalia! Tena kawapa na jina wanaolia kawaita "wachoraji wa nje" mchoraji huyu anajikosesha Kisha anafuta halafu anasema Kuna mchoraji alichora vibaya Kisha anachora yeye tena!.. lkn haachi hivihivi ktk kurudia michoro yake huwatoa kafara wajakazi wake wadogowadogo.
Mchoraji huyu asipokanywa basi mchoro wake atauharibu zaidi maana mpk sahivi kauharibu nusu! Na kwajinsi asivyoelewa nusu iliyobaki ataizongorota si kifani! Na mumuambia walikuwepo wachoraji wazuri zaidi yake nao wamepita. Walikuwepo wachapa rangi wazuri zaidi yake nao wamepita! Kila anachokiona kitapita na ataviacha Sasa ni jukumu lake kuache vyema kuliko kuacha vibaya maana siku zote mwisho wa ubaya ni ubaya.