Kiukweli mwanamke huwezi kumchunga bali yeye akiamua kujichunga mwenyewe na kukuheshimu.
Ilikuwa mwaka 2006 pale demu wangu tuliyependana sana aliponieleza kuwa amepata mwanaume wa kumuoa kipindi hicho naishi bukoba,kwakuwa nilikuwa sijajipanga kuoa nilimuruhusu bila kinyongo ila aliniahidi kamwe penzi letu halitakufa.
Siku moja nikawa na shida ya elfu 70 nikampigia simu na kumueleza,akasema usijari ngoja nifanye makeke,kwa mujibu wake kilichotokea ikawa hivi:
Alimdanganya mume wake kwa njia tofauti anavyojuwa yeye ampatie pesa ikashindikana,ikapita kama siku tatu hivi,ilipofika usiku kama saa tano hivi akachukua vicks dawa ya mafua akaipaka kwenye kope za macho afu akaanza kudai tumbo linamsokota,akajinyonganyonga weee huku macho yanatoa machozi kutokana na ile dawa (vicks).
Mume wake akaamua kumpeleka hospitali,hapo alikuwa na mimba changa,basi banah! kufika huko kumbuka mgonjwa ndiye anayeingia chumba cha dokta,alichofanya akampa dokta elfu tano na kumwambia yeye haumwi ila anataka kwenda kijijini so kwakuwa ana mimba changa ampe dawa za kuzugia pia amshauri mumewe kuwa ni vizuri akitumia pia dawa za kienyeji,dokta bila hiyana akafanya hivo.
Haooo! wakarudi home,kesho yake akamuandalia laki na nusu huyoo kijijini wilaya ya muleba kamachumu.
Kesho yake akanitumia laki moja na kuniambia mimi ni mwanamke nina mbinu za kila aina.
Kiukweli nilichoka kwa mbinu aliyoitumia,hadi leo nikikumbuka hata mke wangu huwa simwamini.
Wanawake siyo watu wa mchezo.