Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,158
- 48,421
Unapotamani kwenye chaguzi za CCM kusiwepo na rushwa au upendeleo, ni kama unataka kusema CCM isiwepo!
Huwezi kuitenganisha CCM na rushwa halafu CCM ikaendelea kuwepo. Rushwa kwa wana CCM wengi ni kama ndiyo damu na pumzi inayoifanya CCM iwe hai.
Siasa za ndani ya CCM zinahitaji Hela nyingi mno kuziendesha. Na matumizi makubwa ya Hela hizo huwa kwenye kutengeneza mitandao ya wapambe, kuhonga wajumbe wa vikao vya maamuzi na mwisho wa siku kuhonga wapiga kura za maoni.
Kwa kweli hapa ilipofikia CCM haiwezekani kuitenganisha na rushwa. Humphrey Polepole aelewe hilo.
Huwezi kuitenganisha CCM na rushwa halafu CCM ikaendelea kuwepo. Rushwa kwa wana CCM wengi ni kama ndiyo damu na pumzi inayoifanya CCM iwe hai.
Siasa za ndani ya CCM zinahitaji Hela nyingi mno kuziendesha. Na matumizi makubwa ya Hela hizo huwa kwenye kutengeneza mitandao ya wapambe, kuhonga wajumbe wa vikao vya maamuzi na mwisho wa siku kuhonga wapiga kura za maoni.
Kwa kweli hapa ilipofikia CCM haiwezekani kuitenganisha na rushwa. Humphrey Polepole aelewe hilo.