Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,625
Wakuu weekend inaendaje?
Usafi ni muhimu kila sehemu, na linapokuja suala la chakula mkazo zaidi unahitajika, maana ukizembea kidogo tu unaweza kuathiri vibaya walaji wako hata kupelekea kifo uchafu aliokutana nao hapo ni mkubwa na kutengeneza sumu kali.
Umeshawahi kukagua sehemu unayokula ukaangalia kama maji wanayotumia kuosha vyombo na kupikia ni masafi, kama vyombo unavyotumia vinasafishwa vizuri, au hayakuhusu ukifika unakula tu unasepa zako?
Pichani, ni sehemu ya chakula Dar ambako ilikuwa sehemu pendwa ya kupata mbuzi. Siku moja nikaona hayo maji kwa uzuri, maji ambayo yalikuwa yakitumika kusafishia visu vinavyokatia nyama, ndimu, pilipili, na ndio maji hayo walikuwa yanatumika kusafisha meza na sehemu ambayo nyama (ya ng’ombe, mbuzi, kuku) inawekwa kwaajili ya kukata vipande vya mteja.
Ili kusafisha anachovya kitambaa ambacho nacho rangi inaenda kufanana na maji hayo kwa kuuzoea uchafu huo.
Maji hayo kama unavyoyaona yalivyomachafu, bado kunakuwa na vimabaki vya chakula ambayo vinakuwa vinaanguka hapo akiwa anajiandaa kumfungia mteja, na kuna kisabuni kwa mbaliii!
Siku hiyo nikamfata jamaa aliyekuwa anawasimamia kumuuliza kwanini hawabadilishi maji wanayofanyia usafi hapo mpaka yanakuwa machafu hivyo, jamaa akasema akasema unajua hiyo ni leo tu yanabadilishwa sasa hivi, nilijua anadanganya ila nikamwambia sawa, nitafatilia jambo hilo. Nilichukua picha lakini niliipoteza, hivyo nikarudi siku nyingine maana nlijua ntakuta tu maji machafu.
Siku nyingine niliyoenda ndio nikachukua na picha hii, ambayo kwakweli uchafu ni ule ule tu.
Hii ni hatari, kama tumbo lako hoya hoya unaweza kupigwa na sumu ya chakula matata sasa. Mabwana afya huwa wanapita kweli sehemu hizi za vyakula na kuhakikisha usafi unafuatwa?
Sehemu unayokula ikoje Mkuu, usafi ni wa hali ya juu au tumemjachia mungu?
Usafi ni muhimu kila sehemu, na linapokuja suala la chakula mkazo zaidi unahitajika, maana ukizembea kidogo tu unaweza kuathiri vibaya walaji wako hata kupelekea kifo uchafu aliokutana nao hapo ni mkubwa na kutengeneza sumu kali.
Umeshawahi kukagua sehemu unayokula ukaangalia kama maji wanayotumia kuosha vyombo na kupikia ni masafi, kama vyombo unavyotumia vinasafishwa vizuri, au hayakuhusu ukifika unakula tu unasepa zako?
Pichani, ni sehemu ya chakula Dar ambako ilikuwa sehemu pendwa ya kupata mbuzi. Siku moja nikaona hayo maji kwa uzuri, maji ambayo yalikuwa yakitumika kusafishia visu vinavyokatia nyama, ndimu, pilipili, na ndio maji hayo walikuwa yanatumika kusafisha meza na sehemu ambayo nyama (ya ng’ombe, mbuzi, kuku) inawekwa kwaajili ya kukata vipande vya mteja.
Ili kusafisha anachovya kitambaa ambacho nacho rangi inaenda kufanana na maji hayo kwa kuuzoea uchafu huo.
Maji hayo kama unavyoyaona yalivyomachafu, bado kunakuwa na vimabaki vya chakula ambayo vinakuwa vinaanguka hapo akiwa anajiandaa kumfungia mteja, na kuna kisabuni kwa mbaliii!
Siku hiyo nikamfata jamaa aliyekuwa anawasimamia kumuuliza kwanini hawabadilishi maji wanayofanyia usafi hapo mpaka yanakuwa machafu hivyo, jamaa akasema akasema unajua hiyo ni leo tu yanabadilishwa sasa hivi, nilijua anadanganya ila nikamwambia sawa, nitafatilia jambo hilo. Nilichukua picha lakini niliipoteza, hivyo nikarudi siku nyingine maana nlijua ntakuta tu maji machafu.
Siku nyingine niliyoenda ndio nikachukua na picha hii, ambayo kwakweli uchafu ni ule ule tu.
Hii ni hatari, kama tumbo lako hoya hoya unaweza kupigwa na sumu ya chakula matata sasa. Mabwana afya huwa wanapita kweli sehemu hizi za vyakula na kuhakikisha usafi unafuatwa?
Sehemu unayokula ikoje Mkuu, usafi ni wa hali ya juu au tumemjachia mungu?