Huu ushuhuda ni upendo au kashfa?

Huu ushuhuda ni upendo au kashfa?

Mwezi uliopita kaka yangu alioa na tukasherehekea kwa furaha sana, jpili iliyopita wanandoa hao wakaja kanisani kushukuru Mungu pamoja na wote walioshiriki, wakapewa nafasi ya kushuhudia lolote juu ya safari yao mpaka kufikia hapo.
Mume alishukuru kwa ufupi then akamwachia mke amalizie ili awakaribishe wati home.

MKE SASA, "Mimi namshukuru sana Mungu kwani nilipata mtihani sana wakati wa uchumba wetu maana nilikuwa najiuliza sana huyu ndiye au la maana nikiangalia KIELIMU mimi nipojuu yeye form IV mi VI, na hata katika swala la kazi ni hivyo hivyo maana yeye fundi nguo mi nimeajiriwa na serikali. lakini nikasikia Roho akinishuhudia kuwa ndiye na nikafikia maamuzi ya kukubali na sasa ni mke na mume"

Kusema ukweli mimi hiyo sikuipenda kabisa, na kwawalio sikiliza ushuhuda huu waligawanyika wengine wakampongeza mke kwa hatua hiyo wengine wakasema alimdhalilisha mumewe, wewe je unasemaje? ungekuwa ni mume ungejisikiaje?

Safi sana, MY LOVE si kaka yako alitaka watu wajue kaoa msomi, ushuhuda ulikuwa wa nini?
 
Last edited by a moderator:
Imeshatokea,ni Kweli Mwanamke Kakosea Tena Sana Tu,lakini Nyinyi Kama Ndugu Mnatakiwa Mkiwa Na Kaka Yenu Hili Suala Msilizungumzie Kabisa Au Hata Ikitokea Kaka Yenu Kalizungumzia Nyie Mumpe Moyo Kaka Yenu Kuwa Hakuna Tatizo Lolote!hii Itasaidia Kujenga Ndoa Yao Kuliko Mapema Yote Hii Ndoa Bado Changa Mkashabikia Kosa La Shemeji Yenu!
 
Kashfa hiyo......lo!

Mke ni mhaya?maana kwa masifa hawajambo.huna jinsi mkuu ndoa imeshafungwa pamoja na usomi wake mme atakua juu yake kitandani

Ni kashfa. Hakuwa na sababu ya kuyaeleza hayo.

Kama elimu ya mume ni hiyo form IV na kazi yake ni fundi nguo, huo ndio UHALISIA wake. Kashfa inatoka wapi hapo? Ingekuwa kashfa iwapo mume angekuwa ni Std 7 halafu anasema yye ni form IV leaver.
 
Siyo nzuri nadhani hata ktk maisha yao huyu mume akikosewa na mwanamke atachukulia ni zarau kwa vile kamzidi na hivyo alivyovisema
 
Mke ni mhaya?maana kwa masifa hawajambo.huna jinsi mkuu ndoa imeshafungwa pamoja na usomi wake mme atakua juu yake kitandani

...saa zingine anaweza kuwa chini yake au nyuma yake pia...!
 
dharau izo....uyo mwanume ajiandae lazima atawaliwe huo ni mwanzo tu..ataisoma
 
Mimi nitachangia kuhusu hiyo elimu. Tangu lini form 6 akajiita yuko juu..!? Watu wameolewa na std 7 wakati wao ni PhD holders. Pia hiyo sio kashfa kwa sababu alisema ukweli japo hakustahili kuusema mahali pale. Kwa hiyo huyu dada aukumimwe kwa kusema vile mahali pasipohusika wala sio kashfa
 
Shuhuda zingine ni kero tu. Tatizo la wanawake wasomi ndilo hilo kwamba wanataka wajulikane wao ni nani kisa wamesoma.
 
Ukweli lazima usemwe kwenye kutoa ushuhuda. Sasa mtoa mada ulitaka atoe ushuhuda gani. Kama vipi wewe ndo ungetoa ushuhuda kama mke wa huyo kaka yako!
 
Hapo hamna mke.

Je na mwanaume angesema sijamkuta sealed na hana malinda angeonekanaje?
 
Mi kwa maoni yangu, hapo mwanaume ndo graduate pamoja na ufundi wake. Tatizo la wanawake siku hizi ndo wana mijisifa utafikiri wamelogwa! Sijui wamekula ya mbuzi au....Pumbaf! Mi ningekuwa mme wake ningetoa ushuhuda kwa kumnanihii hadharani na waone anavyolala chini na usomi wake!
 
sioni kama ni kashfa.. Kwani si wwalikuwepo waliokuwa wanayajua hayo.??
 
inawezekana si kashfa, ila unajua wengine si mafundi wa kuongea mbele ya watu!
inawzekana yeye alisema kwa nia njema tu ila hakujua athari yake.!
ila kwa kifupi, hakutakiwa kutamka maneno kama hayo..
 
Mwezi uliopita kaka yangu alioa na tukasherehekea kwa furaha sana, jpili iliyopita wanandoa hao wakaja kanisani kushukuru Mungu pamoja na wote walioshiriki, wakapewa nafasi ya kushuhudia lolote juu ya safari yao mpaka kufikia hapo.
Mume alishukuru kwa ufupi then akamwachia mke amalizie ili awakaribishe wati home.

MKE SASA, "Mimi namshukuru sana Mungu kwani nilipata mtihani sana wakati wa uchumba wetu maana nilikuwa najiuliza sana huyu ndiye au la maana nikiangalia KIELIMU mimi nipojuu yeye form IV mi VI, na hata katika swala la kazi ni hivyo hivyo maana yeye fundi nguo mi nimeajiriwa na serikali. lakini nikasikia Roho akinishuhudia kuwa ndiye na nikafikia maamuzi ya kukubali na sasa ni mke na mume"

Kusema ukweli mimi hiyo sikuipenda kabisa, na kwawalio sikiliza ushuhuda huu waligawanyika wengine wakampongeza mke kwa hatua hiyo wengine wakasema alimdhalilisha mumewe, wewe je unasemaje? ungekuwa ni mume ungejisikiaje?

nimeipenda hii, jamani wakati mwingine tunaweza kua na mawazo na nia njema kabisa ila jinsi ya kupresent ikawa ishi watu kukuelewa, tujitahidi kuangalia aina ya maneno tunayotoa mbele za watu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom