Huu ushuhuda ni upendo au kashfa?

Huu ushuhuda ni upendo au kashfa?

Hahahaha dunia ina mambo bhna
Mwezi uliopita kaka yangu alioa na tukasherehekea kwa furaha sana, jpili iliyopita wanandoa hao wakaja kanisani kushukuru Mungu pamoja na wote walioshiriki, wakapewa nafasi ya kushuhudia lolote juu ya safari yao mpaka kufikia hapo.
Mume alishukuru kwa ufupi then akamwachia mke amalizie ili awakaribishe wati home.

MKE SASA, "Mimi namshukuru sana Mungu kwani nilipata mtihani sana wakati wa uchumba wetu maana nilikuwa najiuliza sana huyu ndiye au la maana nikiangalia KIELIMU mimi nipojuu yeye form IV mi VI, na hata katika swala la kazi ni hivyo hivyo maana yeye fundi nguo mi nimeajiriwa na serikali. lakini nikasikia Roho akinishuhudia kuwa ndiye na nikafikia maamuzi ya kukubali na sasa ni mke na mume"

Kusema ukweli mimi hiyo sikuipenda kabisa, na kwawalio sikiliza ushuhuda huu waligawanyika wengine wakampongeza mke kwa hatua hiyo wengine wakasema alimdhalilisha mumewe, wewe je unasemaje? ungekuwa ni mume ungejisikiaje?
 
Aliongea ukweli ila haikuwa mahali sahihi ilitakiwa tu atoe shukrani tu na kukaribisha watu home,asilaumiwe sana we differ labda alivyosimama mbele za watu akapata aibu akajiona labda hawamech akajikuta anaropoka ili ajifunike kmb alimsikiliza Roho ingawaje huyo mtu c sahihi kwake,roho ya kiburi inamtesa so anahitaji maombi.
 
Kweli hakufanya vzr, mambo ya kazi na elimu yanakujaje mbele ya kadamnasi, si walikuwa wameshayaongea uko na huyo roho mtakatifu iweje tena aje aropoke mbele za watu. kifupi mke hana hekima
Ni kashfa. Hakuwa na sababu ya kuyaeleza hayo.
 
ushuhuda jamani? kweli kuna miujiza
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom