Huu uonevu wa wanajeshi Ikulu usifumbiwe macho

Huu uonevu wa wanajeshi Ikulu usifumbiwe macho

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,211
Reaction score
99,970
Kwa mara nyingine tena nimeshuhudia Raia akiwa amewekwa chini ya Ulinzi na akirushwa kichura na Wanajeshi walioko pale Feri! Habari kama hii ilishawahi kuripotiwa hapa na Picha kuwekwa.

Najiuliza; kuna ulazima gani wa kushindwa kumwelimisha mtu kama eneo hilo haliruhusiwi kupita, kukaa, kutembea, kusimama, kuongea na simu na vitu vya namna hio hadi umkamate mtu na kumpa adhabu?

Naomba mamlaka husika zishughulikie suala hili tukikumbuka kuwa Ikulu na majengo yake yako kwenye mazingira ambayo wingi wa watu hauepukiki.

Ningewaona wana akili kama wangezuia au wangeimarisha majiko yale ya samaki ili moshi wa samaki wanao kaangwa usinnhgie ikulu au waihamishe lile soko pale kupunguza msongamano au kufunga kabisa ile barabara ila huu upuuzi wa kukamata Raia na kuwapa adhabu ni ujinga na upuuzi uliopitiliza.

Ikumbukwe kuwa jirani kabisa na Ikulu (kama ilivyoripotiwa hapa siku za nyuma) kuna watu wanaishi hapo na kuna kila aina ya uchafu na uhuni uliopitiliza kwenye dunia hii. Wangeenda kuwakamata hao na sio raia wasio na hatia. Narudia tena kitendo au vitendo kama vile havikubaliki wala kuvumilika, lazima hatua zichukuliwe.
Wapumbavu wale, am sorry to say this, ila nimeshuhudia mara nying wakiwasulubu watu pale, had nikajiuliza hiv huu ndo ulinzi ambao mfalme wetu kajiwekea? na picha zao vry soon nitazipata nizilete humu, cz kuna siku walimkamata mtu pale wakamtesa then ikaja vx ya black inaprivate number inaanz8a na A nafkir ikamchukua pale wakatokomea. Sikuwa na camera siku hyo
 
With Google maps, hiyo ya usipige picha eneo hili imepitwa na wakati, mbaya zaidi majeshi yetu ni anti_citizen hasa police! JWTZ ni individuals tuu
 
Lile soko walifunge wawatafutie soko sehemu ingine.
Watumie Usalama wa Raisi kama kigezo basi litafungwa tu.

Ila Raia nao unajua kabisa pale ni Ikulu wapita kufata nini. Mimi nina miaka hata nimesahau rangi ya ukuta wake
 
Nadhani wakati umefika tuhamishe Ikulu kuipeleka mahali ambapo hakuna shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii maana sio kila Mwananchi anajua kuwa pale ni Ikulu na kuwa ni kosa kupiga kando ya ukuta wa Ikulu.
 
Kwani Pinda alisemaje bungeni? Ile kauli ya wapigwe tuu bado inafanya kazi! Mamlaka wameshapewa.
 
Ukishaona serikali inajitenga na watu ujue ni dhalimu.
 
watakupiga tu, maana tumechoka sasa!
asante Sikonge...
 
Last edited by a moderator:
Point yangu ni kwamba, hata kama ni kosa, si suala la kumuelimisha mtu halafu unaachana nae? Unamuweka chini ya Ulinzi raia ambaye hana hata bisbisi mfukoni? Wakati wewe umeshika SMG? Huu ni uonevu usiovumilika. Naomba mamlaka zinazohusika walitolee ufafanuzi jambo hili bila kuwa biased.
 
Point yangu ni kwamba, hata kama ni kosa, si suala la kumuelimisha mtu halafu unaachana nae? Unamuweka chini ya Ulinzi raia ambaye hana hata bisbisi mfukoni? Wakati wewe umeshika SMG? Huu ni uonevu usiovumilika. Naomba mamlaka zinazohusika walitolee ufafanuzi jambo hili bila kuwa biased

Naomba mnisaidie yasije yakanikuta. Niko mikoani miaka mingi nataka kuja Dar wiki ijayo. Hayo ya kichura yako upande upi? Ni barabara ya kule baharini au hii ya kutokea wizara ya elimu kuelekea Ocean Rd hospital?
 
mpola Ukitoka wizara ya Elimu kuja huku kwenye Jengo La Feri au wanaiita soko la samaki...
 
Last edited by a moderator:
Kwani mukigoma kupita barabara hiyo ya IKULU Kova atawashughulikia...kama samaki hata msasani wanapatikana tena ni fresh kuliko wa ferry halafu tena mutaangusha uchumi wa Ilala kwa maana soko la samaki itabidi lifungwe.
 
Wanadamu hawana jema,si mlisema wanajeshi wapo karibu zaidi na wananchi polisi leo unalialia huna lolote unalo lijua zaidi ya kulalamika.
 
Kwa mara nyingine tena nimeshuhudia Raia akiwa amewekwa chini ya Ulinzi na akirushwa kichura na Wanajeshi walioko pale Feri! Habari kama hii ilishawahi kuripotiwa hapa na Picha kuwekwa.

Najiuliza; kuna ulazima gani wa kushindwa kumwelimisha mtu kama eneo hilo haliruhusiwi kupita, kukaa, kutembea, kusimama, kuongea na simu na vitu vya namna hio hadi umkamate mtu na kumpa adhabu?

.

Hii ndiyo shida tupu?

Elimu rahisi ni kuweka vibao sahihi .Tabia hii ya Wanajeshi wetu-siyo njema kabisa huku nikujitengenezea Uadui na Raia-na kuwaondolea Uzalendo wa toka Moyoni. Hawa vijana waliopangiwa haya Malindo ya Ikulu wanatakiwa wawe kati ya wale Best siyo magarasha yasiyokuwa na nidhamu na adabu. Na lazima wawe na akili ya kuzaliwa Pia.Mwisho waweke alama!

Tabia hii ya Taasisi nyingi kuwaachia walinzi au watendaji wake kusimamia Sheria au Kanuni fulani kisirisiri ndiyo kutengeneza mianya ya rushwa. Kuna hoja moja ya Geti la magari kuingilia kwenye pantoni eti ni la Jeshi hakuna maelezo ya maandishi kuelekeza kuwa ni kwajili ya gari za jeshi tu. Hata Picha kweli watu watakuwa hawaioni-Watendaji acheni uvivu fikra.


 
Elli

Una uhakika kwamba ni wanajeshi?!au ni wale walinzi wenye gwanda zenye baka zinazotaka kufanana na za jeshi??!ebu tuweke wazi hapo mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Lile soko walifunge wawatafutie soko sehemu ingine.
Watumie Usalama wa Raisi kama kigezo basi litafungwa tu.

Ila Raia nao unajua kabisa pale ni Ikulu wapita kufata nini. Mimi nina miaka hata nimesahau rangi ya ukuta wake

Kwasababu huna shughuli zinazokufanya upite pale mara kwa mara.
 
Point yangu ni kwamba, hata kama ni kosa, si suala la kumuelimisha mtu halafu unaachana nae? Unamuweka chini ya Ulinzi raia ambaye hana hata bisbisi mfukoni? Wakati wewe umeshika SMG? Huu ni uonevu usiovumilika. Naomba mamlaka zinazohusika walitolee ufafanuzi jambo hili bila kuwa biased

Mkuu unataka mamlaka gani wakati zote ni corrupt tu? Nitajie hata moja.
 
Back
Top Bottom