Huu ufa kwenye hii ndoa unazibika?

Huu ufa kwenye hii ndoa unazibika?

sononaaa

Member
Joined
Jun 22, 2025
Posts
21
Reaction score
77
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji. Chanzo cha yote(tatizo) ni mimi haihusiani na usaliti na tulishakaa vikao na familia tukayamaliza lkn mara zote toka hapo haijawahi kuisha wiki bila kununiana furaha siku 3 nne zillizobaki ni sintofahamu pamoja na kuwa anatimiza majukumu yake yote kama mke.

Usiku wa kuamkia leo baada ya kuniomba talaka yake alimpigia mama yake simu by 7 kasoro usiku kumueleza kuwa hana furaha tena! mama alikuwa na hamu ya kujua nini tatizo lkn binti alisisitiza siioni ndoa yangu tena na kukata simu ila kabla ya kukata alimuahidi kesho ntakuambia kila kitu.

Kwa hili sikuwa na namna sababu nilisharuhusu simu kupigwa japo baada ya kupiga simu nilimuomba usizungumze chochote na mama yako kuhusu hili wewe utajua namna ya kuongea ili kutuliza hali na ameniitikia kwa kunielewa, lkn sijui kichwani anawaza nini!

Nilimuahidi mimi pia nitazungumza na mama yake, jambo jingine nimemuomba nimuache peke yake kwanza nisafiri ili angalau upatikane muda wa utulivu kwanza lkn sio kumpa talaka.
 
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji. Chanzo cha yote(tatizo) ni mimi haihusiani na usaliti na tulishakaa vikao na familia tukayamaliza lkn mara zote toka hapo haijawahi kuisha wiki bila kununiana furaha siku 3 nne zillizobaki ni sintofahamu pamoja na kuwa anatimiza majukumu yake yote kama mke.

Usiku wa kuamkia leo baada ya kuniomba talaka yake alimpigia mama yake simu by 7 kasoro usiku kumueleza kuwa hana furaha tena! mama alikuwa na hamu ya kujua nini tatizo lkn binti alisisitiza siioni ndoa yangu tena na kukata simu ila kabla ya kukata alimuahidi kesho ntakuambia kila kitu.

Kwa hili sikuwa na namna sababu nilisharuhusu simu kupigwa japo baada ya kupiga simu nilimuomba usizungumze chochote na mama yako kuhusu hili wewe utajua namna ya kuongea ili kutuliza hali na ameniitikia kwa kunielewa, lkn sijui kichwani anawaza nini!

Nilimuahidi mimi pia nitazungumza na mama yake, jambo jingine nimemuomba nimuache peke yake kwanza nisafiri ili angalau upatikane muda wa utulivu kwanza lkn sio kumpa talaka.
Tatizo lilianzia mlipopelekana kwa wazazi kusuluhishana
 
Back
Top Bottom