Huu ni upumbavu..!!

Ibrahim K. Chiki

JF-Expert Member
Apr 5, 2011
594
163
Hivi, tanzania tunaelekea wapi? tukiacha ushabiki wa vyama, chadema na ccm, kujaza watoto wenye umri kati ya miaka 10 na 15 kujadili muswada wa katiba tunajenga au tunabomoa? mbya zaidi watoto wenyewe wameishia kuchapa usingizi tu ukumbini, hii ni upumbavu tena nadhani inabidi tuanze kuweka utaifa mbele na si uchama, kwa sababu uchama hautasaidia. we should wake up, hicho chama kilichojaza watoto kiadhibiwe accordingly.
 
Ni kweli,kabisa wale watoto wa shule ya sekondari ya City mjini Dom na mmiliki wa shule hiyo ni mbunge wa Dodoma mjini (CCM).Nafikiri walilazimizshwa waende,
 
Nadhani ni katika kumuunga mkono aliyetoa tamko jana kwamba chama chake kina mabasi mengi hivyo wanao uwezo wa kutosha kuleta wanachama wao sasa mmeona?Mnaleta watoto hata kifungua kinywa inaonekana hawkupata mwishowe usingizi kwa kwenda front.Hapa kazi ipo.
 
Cha kushangaza ni kuwa, ilikuaje watu wa usalama washindwe kuzuia hao watoto kutokuingia ukumbini...wanashndwa hata na watu wa madaladala koz wao huzuia wanafunzi kuwa wengi.
 
Ni kweli ni upumbavu wa hali ya juu watu tunajuta kuangalia tv na kuona habari kama hii coz mtu unashndwa kuelewa anayefanya hivi anatumia nini kufikiri?na mbaya zaidi unaambiwa aliyefanya hvi ni kiongozi wako?jamani hi ni aibu,walaaniwe wanaopotosha haki za watanzania,
 
Hivi, tanzania tunaelekea wapi? tukiacha ushabiki wa vyama, chadema na ccm, kujaza watoto wenye umri kati ya miaka 10 na 15 kujadili muswada wa katiba tunajenga au tunabomoa? mbya zaidi watoto wenyewe wameishia kuchapa usingizi tu ukumbini, hii ni upumbavu tena nadhani inabidi tuanze kuweka utaifa mbele na si uchama, kwa sababu uchama hautasaidia. we should wake up, hicho chama kilichojaza watoto kiadhibiwe accordingly.

Nani akiadhibu?Hivi kesi ya Nyani unaweza kumpelekea Ngedere kweli.Wewe vipi?
 
Hakuna kitakachoweza kubadili mbegu iliyopandwa vicvwani mwa watu, hata kama wakijaza watoto kwenye mikutano ya katiba!
Hatoki mtu safari hii!
 
Hatuwezi sema tumekomaaa kisiasa kwa upumbavu kama huu...tunashndwa kupeleka watu wa msingi kutetea muswada kwa maslahi ya taifa. inasikitisha sana.
 
Aisee ile kitu ime ni piss off kabisa na kunitia hasira ya ajabu, inaoneka kuna watu flani hawako serious kabisaaa na KATIBA mpyaa. wale watoto masikini wameletwa pale saa kumi na moja asubuhi eti kisa kujaza nafasi mle ndani Karimjee hall ili watu makini wasipate nafasi ya kuchangia kwenye hoja ya katiba mpyaa. Jamani hivi katiba mpya inajadiliwa siku tatu tu na mikoa mitatu tuu? hapa kuna walakini mkubwa sana tena sana, watawala wetu wanachochea vurugu hivi hivi tukiona. wanalazimisha matakwa yao tuyakubali ili waendelee kukaa madarakani milele yote. mimi kwa kweli nimejawa na hasira za ajabu kwa sababu naona kikundi cha watu wachache wanafanya maamuzi kwa maslahi yao tuu. hii ni mbaya sana wananchi wengi sasa hivi wanahitaji mabadiliko na si udikteta, sasa wakiona haki yao inapunjwa wataingia barabarani na kuleta mtafaruku wa kudai haki yao kinguvu, na kila jambo huanza kama mzaha na kukua kuwa kubwa. CCM naona sasa mnataka mtoke madarakani kwa bakora, yangu macho!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom