Huu ni Ugonjwa(wadada) ama?

Huu ni Ugonjwa(wadada) ama?

Sizinga

Platinum Member
Joined
Oct 30, 2007
Posts
9,519
Reaction score
7,287
Naomba #MODS msiiweke hii srdi kwenye JF Doctor, iache hapahapa ipate michango ya wadada,wakaka na madaktari.

Nina rafiki yangu wa kike yaani anateseka sana akiaanza kuumwa. Sasa tangu anisumulie story yake nimejaribu kumpa ushauri lakini ningependa kujua hii ni kitu gani haswa.

Infact huyu dada ana tatizo la kutokwa na damu nyingi sana kipindi cha Hedhi yake. Period yake inatokea mara mbili kwa mwezi na inakaa zaidi ya siku 10 kuisha, sasa huwa anaumwa sana na tumbo mpaka anakata tamaa, kiukweli she is married na nilimshawahi kumshauri kwamba yambidi ashike ujauzito, akasema amepitia check up nyingi vipimo vingi na madaktari aliokutana nao walimshauri same thing kwamba ashike ujauzito itakuwa ndio solution ya tatizo lake.

Cha kusikitisha ni kwamba siku zake ni Irregular kabisa, amejitahidi sana kufuata kalenda na amejitahidi sana kushika mimba lakini imeshindikana(Kaamua kumwachia Mungu tu). Haamini tena kufuata kalenda na hana uhakika wa kushika mimba. Juzi kapoteza hamu ya kula siku 2 akaumwa sana na alivyoenda medical vipimo alivyofanya ni negative!! Alipewa tu dawa za minyoo, huwa tumbo linamsumbua sana.

Inafika wakati hata kukaa kitandani anashindwa manake damu huwa zinavuja tu. Nimejaribu kumhusisha na mambo ya kiimani kasema hamna kitu kama hicho. Sasa wenye uzoefu na hii kitu hembu toeni muongozo kwa hili tatizo


NB: Huyu dada hajawahi kushika wala kutoa mimba.
 
Backgroud yake ni ipi?

Tangu alipopevuka alianza hivyo au ni baada ya kuanza kutumia njia za uzazi wa mpango. Nikijibiwa swali hili nitafunguka zaidi.
 
kikubwa kwangu ni pole tu, mada imekaa kidaktari zaidi
 
aone madaktari bingwa wa uzazi ambao wameshakutana na kesi kama hizi asiende uchochoroni linatibika hili yupo ninayemfahamu alikuwa anashida kama hiyo na kapona na ana watoto sasa ila ndo sijui alitibiwa wapi sina contact nae kwa sasa
 
Huyo anamatatizo ya tumbo la uzazi! Either homon zimezidi ama uchafu unaosababishwa na mafuta n.k Na kwa hali hiyo hawezi shika mimba sababu mzunguko wake kutoeleweka..aende kwa specialist wa wanawake ama ajaribu kwenye centre za tiba asilia atapona btw-yupo mkoa gani?
 
Huyo anamatatizo ya tumbo la uzazi! Either homon zimezidi ama uchafu unaosababishwa na mafuta n.k Na kwa hali hiyo hawezi shika mimba sababu mzunguko wake kutoeleweka..aende kwa specialist wa wanawake ama ajaribu kwenye centre za tiba asilia atapona btw-yupo mkoa gani?

Hapo kwenye red - BIG UP - Tatizo wabongo uzungu mwingi mno wakati tiba ziko kwenye mimea iliyotuzunguka. Apime ajue tatizo then tiba ni rahis sana kwenye hizo centre za tiba asilia.
 
Hormonal imbalance? Chronic infections? Fibroids? au kitu chochte kingine...

Asikate tamaa. Kila anapoona chance pmya ya kwenda kuwaona madaktari afanye hivyo.

Wasiwasi wangu ni kuwa kwa hospitali tulizo nazo inaweza kuwa ngumu tatizo lake kuonekana kwa uhakika.

Mi namshauri atumie "natural products" zinazojulikana ku-harmonize body secretions lakini pia zinazoondoa maambukizi ya muda mrefu.

Uzuri wa miti shamba, nyingi ni viungo tunavyotumia kila siku kwa hiyo hazijawahi kuonyesha madhara hata ukitumia miaka kumi.

Vitu kama Tangawizi, mdalasini, iliki, karafuu na binzari ni dawa nzuri sana zikitumika regularly.

Lakini pia extracts za miti shamba siku hizi zinawekwa kama vidonge au capsules na huuzwa madukani.

Kama atapenda kutumia dawa zilizotengenezwa purely kutoka kwenye mimea na hajui pa kuzipata, mkuu ni PM nikupe directions

Pole sana kwake...
 
Huyo anamatatizo ya tumbo la uzazi! Either homon zimezidi ama uchafu unaosababishwa na mafuta n.k Na kwa hali hiyo hawezi shika mimba sababu mzunguko wake kutoeleweka..aende kwa specialist wa wanawake ama ajaribu kwenye centre za tiba asilia atapona btw-yupo mkoa gani?

Kweli kabisa bidada...
 
Sizinga wataalam wengi wa utabibu si wapenzi wa jukwaa hili, huitendei haki thread yako. Huku siku hizi watu makini ni wachache sana vimejaa vitoto vingi with cheap topics.
 
Last edited by a moderator:
Huyo anamatatizo ya tumbo la uzazi! Either homon zimezidi ama uchafu unaosababishwa na mafuta n.k Na kwa hali hiyo hawezi shika mimba sababu mzunguko wake kutoeleweka..aende kwa specialist wa wanawake ama ajaribu kwenye centre za tiba asilia atapona btw-yupo mkoa gani?
Yupo Arusha kwa sasa anafanyakazi. Huenda kweli ni tumbo la uzazi na homon inbalance...so ngoja kwanza hizo centre za tiba asilia zipo wapi kwa hapa Chuga?
 
Sizinga wataalam wengi wa utabibu si wapenzi wa jukwaa hili, huitendei haki thread yako. Huku siku hizi watu makini ni wachache sana vimejaa vitoto vingi with cheap topics.
Mkuu Matola ni kweli JF imekuwa ya hovyo sana nowadays tofauti na kipindi kile lakini still kuna vichwa naviamini bado they can share good stuff from them...si unaona kama charminglady ashawahi kuwa na hili tatizo so she can help alot.
Otherwise niiweke pia Jukwaa lile la Doctor is it?
 
Last edited by a moderator:
Kwamba sperm za mume wake ndio chanzo cha tatizo la yeye kutokwa damu nyingi?
Hahaaa hata mi nimeshangaa kwa kweli...!! Au labda ka refer uwezo wa kushika mimba na mme wake
 
Hormonal imbalance? Chronic infections? Fibroids? au kitu chochte kingine...

Asikate tamaa. Kila anapoona chance pmya ya kwenda kuwaona madaktari afanye hivyo.

Wasiwasi wangu ni kuwa kwa hospitali tulizo nazo inaweza kuwa ngumu tatizo lake kuonekana kwa uhakika.

Mi namshauri atumie "natural products" zinazojulikana ku-harmonize body secretions lakini pia zinazoondoa maambukizi ya muda mrefu.

Uzuri wa miti shamba, nyingi ni viungo tunavyotumia kila siku kwa hiyo hazijawahi kuonyesha madhara hata ukitumia miaka kumi.

Vitu kama Tangawizi, mdalasini, iliki, karafuu na binzari ni dawa nzuri sana zikitumika regularly.

Lakini pia extracts za miti shamba siku hizi zinawekwa kama vidonge au capsules na huuzwa madukani.

Kama atapenda kutumia dawa zilizotengenezwa purely kutoka kwenye mimea na hajui pa kuzipata, mkuu ni PM nikupe directions

Pole sana kwake...
Thanks mkuu Tuko Pamoja...ngoja nijaribu kumshauri tiba mbadala akiwa poa nitakutafuta thru PM broda!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom