Huu ndio ubabaishaji serikali imemfanyia Dangote alifikia hadi kutengeneza reli lakini imeshindikana

Dangote ni Mnajeria mfanyabiashara aliyebobea naomba inshu za kuhusu kiwanda cha Cement wachumi wa nchi hii waiangalie vizuri. Tukiingia kichwa na matamko ya kuchomoa mfukoni na kurusha Jamaa huyu anaweza kufukuza wawekezaji kabisa.
 
Namuamini sana raisi wangu magufuli, kama kweli walikubaliana kufanya kazi pamoja na dangote watafanya tu. Magu hawezi muacha muwekezaji kama huyo aondoke tz hivihivi.
Siwezi comment chochote hadi nisikie upande mwingine wa serikali yangu tukufu. There might be a problem with dangote.
 
Ushauli wangu; usihukumu kwa kusikiliza hoja za upande mmoja tuu. Mwisho wa siku utabatilisha hukumu yako.
 
Lazima tukiri serikali yetu imekosa kabisa intrepreneurial leadership. JPM amejaza serikali yake PhD holders kama vile anataka kufungua university Ikulu. Hajui kuwa PhD holders wengi are the worst managers and worst business people. Tafuta takwimu katika top 100 best performing international business companies, mangapi CEOs wao ni PhD holders.

Uongozi ndani ya serikali ulistahili kuakisi agenda ya Taifa. JPM anasema agenda ya Taifa ni kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda lakini anaamini wa kutufikisha huko ni lazima wawe watu ambao hata definition ya kiwanda hawajui, sifa yao kubwa ni kuwa makada waaminifu wa chama. Kwa kushindwa kuteua watu wenye uwezo kuisimamia agenda kwa vile wana uelewa, ana guarentee ya 100% ya kushindwa.

Mkuu Msambichaka, mambo mengi namu-support JPJM hisipokuwa hili la ku-appoint PhD holders karibu kila sekta kitu hicho binafsi kinanipa wakati mgumu kukielewa!!

Hawa jamaa wanafaa zaidi kuwa ma academician na kwenye taasisi za R&D, sijui niwashauri gani wanamwambi kwamba akisha waweka kwenye keyposts basi kila kitu kitakuwa plain sailing!!

Leo nilikuwa nangalia list ya watu walio teuliwa na Donald Trump kuwa ma economic adviser wake wa karibu, utakuta karibu wote ni wale wenye track record nzuri ya ku-run makampuni/vitega uchumi vyao kwa ufanisi mkubwa, kati ya hao 20+ wenye shahada ya PhD awazidi wawili!!

Hizi teuzi za Trump zina dhilisha/tufundisha kitu gani sisi Watanzania na Viongozi wetu -nafikiri kuna umuhimu wa kurudi kwenye drawing board na kijitathimini kama Taifa tujiulize, je, kuna ulazima wowote wa kuwaweka PhD holders kwenye mission critical posts zote Nchini au la? The sooner hilo linatekelezwa the better, nataka nieleweke kwamba sina tatizo na watu hao - tatizo langu ni ,je, wataweza kutuvusha the rubbicon.
 
Hiloo Sio suala la ccm wakuu,hapo ni chuki binafsi na roho mbaya ya hali ya juu mnoo ambayo haiwezi kuelezeka kabisa kabisa,ilianza ati malori yake dangote yana haribu barabara ....
 
Eti kiongozi fulani wa serikali anataka kutuaminisha Dangote anataka Gesi bure,that doesn't make any sense at all! Hii vita Dangote ameshashinda tayari.
 
Mkuu jaribu kurudia kusoma article nzima, huyu jamaa analeta habari za kutunga mno - kama amepewa taarifa hizi kutoka a third party basi wahusika wana lengo la kutaka kuidhalilisha Serikali ya JPJM kwa kutumia adithi za kutunga tu.

Kiongozi gani mwenye akili timamu anaweza kumkorofisha muwekezaji mkubwa na wa maana kama Dangote?? Kwanza Dk.Magufuli akipata taarifa kwamba kuna baadhi ya viongozi ndani ya Serikali yake wanataka kumuhujumu Dangote atawafukuza kazi on the spot.

Tuache kuleta adithi za kutunga, utasikia mara Dangote kakosa mkaa wa kutosha kutoka Tanzania, mara Dangote kakataliwa kuuziwa gesi kwa bei nafuu wakati gesi inapatikana huko huko Mtwara ambako hakuna gharama za usafirishaji, mara Dangote kanyimwa umeme - yaani tumejaa roho za kutu kama wachawi, kazi kuitakia mabaya Serikali ya JPJM - hakuna habari njema/nzuri wanazo zileta humu zaidi ya kulahumu chama tawala na Uongozi

[HASHTAG]#achakujipendekeza[/HASHTAG]!
 
Naona watu wapo busy kumsafisha dangote Kama malaika hakosei.
Hamna serikali ambayo inaweza kumzuia mtu namna hiyo Sema propaganda zenu nao Mmeamua kuishambulia serikali kwa kila inachofanya.
Halafu nahisi Salary Slip na technically ni mtu mmoja sababu kwenye thread Kama hizi Ndo huwa wanajitokeza kupost
Lakini zile za serikali kutoa trioni 1 kununua dawa hata huwaoni...!!

wewe na [HASHTAG]#lizaboni[/HASHTAG] ni mtu mmoja?mbona serikali ikichemka hamuikosoi,kazi kusifia tu?
 
Hii habari ipo nusunusu.
Mbona hataji hvo vitalu wavyomiliki hao majamaa anaodai wanamhujumu dangote kua ni wamiliki wa kitalu namba flani na flani. Pia na yy mbona anakuja na taarifa isoyokamilika mara sijui cents 7 mara 9 mara I'm not sure.
Na km ni mzalendo halisi ajitaje kabisa jina na cheo chake na kampuni yakena sio kujificha nyuma ya keyboards
 
Nchi hii siasa inatumika kwenye utalaam ambavyo siyo sahihi. Fikiri wewe ni engineer, mwanasiasa anakusahihisha na kukufundisha namna ya kutengeneza barabara. Mbaya zaidi ni form four failure au ana pass degree ya political science. Halafu kwa njaa zetu na frustration tunakubali kuburuzwa. Yakiharibika mtaalamu ndiye anabebeshwa lawama.
Hebu tuwage tunaogopa taaluma zetu na tuwe na msimamo both executives na mawaziri watalaam tutaheshimiwa. Mara nyingi ushauri utoke kwa wataalam na maamuzi yatoke kwa wanasiasa, kinyume cha hapo tusikubali.
Swala la dangote litoke kwenye majukwaa lirudi kwenye drawingboards na conference rooms.
Tanzania ni yetu sote ispokuwa tupo kwa kipindi kirefu miaka 35 na zaidi na ndiyo tunaojibu maswali ya ajabu na mwanasiasa yuko kwa miaka mitano ikizidi kumi labda zaidi kwa wale vinang'anizi.
 
Swali kwa dangote, ,,Hayo makubaliano uliyongia na serikali au na watu binafsi walioko serikalini? Maana kama ni serikalini basi yalipaswa kufuata taratibu maalum sababu hiyo ni raslimali ya watanzania na sio ya watu binafsi.
Wewe dangote kama mfanya biashara mkubwa Africa na tajiri,utawezaje kuwekeza mali bila makubaliano ya kisheria? Kama uliamua kufanya hivo ukijua unakiuka taratibu,huoni kuwa ulikuwa na nia OVU,ya kujinufaisha wewe binafsi na sio umma wa watanzania??
TUTAKUAMINIJE WAKATI ULIKUWA NA LENGO OVU,hata kama umetoa ajira kwa watanzania walio wengi???

Hizo ni simulizi zimekaa ki- alif lela ulela!. Mtoa habari hajatujaza data na vyanzo venye mamlaka ya kuzungumzia mambo hayo. Pia Reputable company kama hiyo haiwezi kuingia makubaliano ya hovyo kiasi hicho;

My take: Kama ilivyozoeleka kuna wapigaji waliokuwa wamelengesha mabakuli ya unyonyaji katika mradi huo, lakini kutokana na umakini wa mamlaka ya sasa mirija yao imezibwa na sasa wanajitahidi kuanzisha timbwili wakidhani wanaweza kujipatia fursa za kutumbua bila jasho! Wameshachelewa. Kitaeleweka tu mwisho wa siku:
 
Siku zote ni lazima kuheshimu makubaliano na mikataba. Mengine yote ni ubabaishaji. Kitazamwe kilichokubaliwa wakati wa uanzishaji wa mradi.

Kwenye jamii ya watu wenye akili na waliostaarabika, ni kosa kubwa kutoheshimu makubaliano. Mwekezaji aliweka mradi wake kwa kuzingatia terms za makubaliano. Huenda kama kusingekuwa na makubaliano hayo asingejenga kiwanda chake Tanzania.

Usipoheshimu makubaliano, wewe ni mhuni na mbabaishaji mkubwa. Serikali haitakiwi kuendesha mambo yake kihuni au kiubabaishaji. Tukilikubali ibabaishaji ndani ya serikali, itakuja kutuletea gharama kubwa kama Taifa siku za mbeleni. Tuukemee uhuni na ubabaishaji ndani ya serikali. Watu wasifanye uhuni serikalini kwa kisingizio cha uzalendo. Uzalendo wa kweli ni kulinda hadhi ya Taifa kwa kuheshimu mikataba. Ni lazima, siyo hiari, kuheshimu mikataba.
Elezea hayo makubaliano kabla ya kulalamika.
Mbona hamyasemi hayo makubaliano?

Kwani hiyo Natural gas bei yake ni constant au inakuwa determined na soko?
So what's the market value of Natural gas?

Whenever energy is mentioned, you can forget things like price stability.

Geez!!!
 
Back
Top Bottom