Ruvuma: Waziri Jafo awaelekeza NEMC kuhakikisha Wachimbaji wa Migodi Wanarejesha udongo sehemu walizochimba

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Suleiman Jaffo akiwa katika ziara Mkoani Ruvuma katika Mkaa ya Mawe ili kujionea hali halisi ya utunzaji wa mazingira amesema biashara ya Makaa ya Mawe imekuwa kubwa Duniani.

Katika ziara hiyo ya Juni 21, 2023 Jaffo amesisitiza kuwa Tanzania ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa bidhaa hizo lakini mchakato wote lazima uzingatie utunzaji mazingira.

Amesema “Mfano Mgodi wa Ruvuma ni mkubwa na unazalisha wastani wastani Tani 200,000 kwa mwezi, pia nimefarijika migodi niliyotembelea inafanya shughuli za uchimbaji wa Makaa ya Mawe na kurejesha udongo sehemu walizochimba.

“Nimewataka wawekezaji wengine wa migodi mingine Nchini wahakikishe wanapochimba rasilimali madini, wanarejesha maeneo waliyofanya uchimbaji kama inavyofanyika Ruvuma.

“Nimemuelekeza Mtendaji Mkuu wa NEMC, Dkt. Samwel Gwamaka kutembelea migodi mingine yote hasa ya Kanda ya Ziwa ambao wanachimba lakini hawarejeshi udongo.”

Ameongeza kuwa katika kuzingatia utunzaji wa mazingira, ametoa maelekezo ya maji tiririka kutoka migodini kuwa yanapokutana na maji ya mvua inakuwa changamoto katika ardhi.

Pia ametoa maelekezo kuwa magari yanayosafirisha madini hayo yawe na mfumo mzuri wa ufunikaji wakati wanapokuwa wamebeba Makaa ya Mawe kwa kuwa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya Wananchi kuwa wanadondosha makaa hayo mtaani.

Naye, Mtendaji Mkuu wa NEMC, Dkt. Samwel Gwamaka aliyekuwa ameandamana na Waziri katika ziara hiyo amesema kuna fursa nyingi ambazo zimezidi kujitokeza.

Amesema “Tuna maeneo mengi yenye Makaa ya Mawe, nawashauri wale wenye leseni ya kuchimba washirikiane na Serikali katika kukuza soko lao kwa kuwa mambo kama haya huwa yanaendana na teknolojia, majanga kama ya vita yanatokea mara chache.

“Pamoja na kutumia fursa ya kuchimba lazima mazingira yaendelee kutunzwa na kuhifadhiwa, katika ziara yaetu tumeona kuwa masharti ya utunzaji mazingira yanafuatwa na Kampuni zote tulizotembelea.

“Bado kuna maeneo machache ambayo tungependa waendelee kuyafangia kazi kubwa ikiwemo ufungwaji wa migodi ambalo ni takwa la kisheria, inatakiwa kuzingatiwa hasa katika Migodi ya Makaa ya Mawe ambayo inatumia sehemu kubwa.

“Wakati huohuo baada ya kuchimba na maeneo yaliyochimbwa yanarejesha katika hali ya awali kwa kuwa tunaamini vizazi vijavyo vinaweza kuendekeza maeneo hayo.”
 
Huyu Jafo nae poyoyo.


Udongo si ndiyo makinikia? Wenzaje wanajenga smelters yeye anataka udongo urudishwe, wale wanaowekeza kwenye smelters atawarudishia gharama zao?

. Hii miwaziri mingine huwan inakurupuks bila mpango. Jafo mama hauna cha kusema i heri ukae kimya kuliko kuongea utumbo.
 
Huyu z

Jafo nae poyoyo.


Udongo si ndiyo makinikia? Wenzaje wanajenga smelters yeye anataka udongo urudishwe, wale wanaowekeza kwenye smelters atawarudishia gharama zao?

. Hii miwaziri mingine huwan inakurupuks bila mpango. Jafo mama hauna cha kusema i heri ukae kimya kuliko kuongea utumbo.
Jafo ni zaidi ya poyoyo
 
Hapo jambo limefika penyewe #NEMC watalichukua hilo nawatalifanyia kazi haraka sana ninachowapenda NEMC wamebadilika sana walichelewq lakini sasa wanaenda vizuri hili litaisha salama na nyie watu migodi anzeni kujitafakari mnakubaliana vizuri halafu mnakwenda kinyume sasa NEMC wakijakufunga msije andamana fanyeni kazi kwa weledi
 
Waziri Jafo kwakweli unafanya kazi nzuri kwa kweli halipingiki na ushirikiano wako na #NEMC Umezaa matunda kuanzia kwenye zuio la mifuko ya plastiki ikafika wakati wa kelele chafuzi mkaweza kuzuia kama sio kumaliza tatizo sasa mpo Kwenye hili shikamaneni nalo liishe NEMC siku izi pana viongozi shupavu kweli najua watalibeba mara moja tatizo liishe

#NEMC NA WAZIRI JAFO pokeeni Maua yenu💐💐💐💐
 
Kazi na iendelee
Wahakikishe pia wanapanda miti mingi maeneo yote yanazunguka migodi
 
NEMC mnafanya kazi kubwaa katik kutunza mazingira ya binadamu na viumbe vyote hapa nchini, hongeren kwa kazi nzuri
 
Apo kwenye kufunika magari yao umesema vyema Mheshimiwa barabara zinachafuka sana wafunike vizuri makaa yasianguke. Nemc kazi nzur sana
 
Hapa hatuna shaka na NEMC, Taasisi hii katika kipindi hiki imekua mstari wa mbele katika kuhakikisha Wananchi wanatunza mazingira. Kongole kwa Mtendaji Mkuu wa NEMC Dr. Mafwenga
 
Huyu Dr. Toka apewe hii taasisi mwaka 2019 Kiukweli amefanya mageuzi makubwa sana ya kiutendaji ndani ya NEMC.

NEMC Walilala sana kipindi cha 2018 kurudi nyuma huko, ila kwa sasa tunaona jitihada za dhati zinazofanywa na taasisi hii katika kuhakikisha Utunzaji wa mazingira unatekelezwa kwa kiasi kikubwa kwa Stakeholders wote nchini.
 
Back
Top Bottom