OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,242
- 103,943
Asubuhi ya jana nikiwa nasikiliza redio kipindi cha dini. Kwenye kipindi kulikuwa na mchungaji anaombea wenye shida na wengine wakawa wanatoa ushuhuda.
Jamaa mmoja akapiga simu kueleza shida yake kwamba kuna hela zimepotea kiutatanishi hapo kwake. Kabla hajamaliza mchungaji akadakia na kuanza kumuelezea mambo ya hapo kwake. Akamwambia hapo kuna mapepo makali sana na pia kupotea hizo pesa kumesababisha mtafaruku wa yeye na mke. Mchungaji akamwambia jamaa hizo hela zipo ndani zimefichwa moja ya room.
Palepale mchungaji akiwa live kituo cha redio akaanza kumpa maelekezo jinsi ya kuzipata hizo pesa. Akamwambia nyumba yake ina vyumba vitatu anaende chumba fulani. Kupitia redio ikawa tunasikia movement za kuelekea chumbani.
Ile hali sikuipotea vizuri nikabadilisha station.
Kwa kweli bado sijashawishika kama kuna maombi ya kiwango hiki. Yaani inakuwa kama upo live na Yesu mwenyewe kumbe ni mchungaji tu.
Jamaa mmoja akapiga simu kueleza shida yake kwamba kuna hela zimepotea kiutatanishi hapo kwake. Kabla hajamaliza mchungaji akadakia na kuanza kumuelezea mambo ya hapo kwake. Akamwambia hapo kuna mapepo makali sana na pia kupotea hizo pesa kumesababisha mtafaruku wa yeye na mke. Mchungaji akamwambia jamaa hizo hela zipo ndani zimefichwa moja ya room.
Palepale mchungaji akiwa live kituo cha redio akaanza kumpa maelekezo jinsi ya kuzipata hizo pesa. Akamwambia nyumba yake ina vyumba vitatu anaende chumba fulani. Kupitia redio ikawa tunasikia movement za kuelekea chumbani.
Ile hali sikuipotea vizuri nikabadilisha station.
Kwa kweli bado sijashawishika kama kuna maombi ya kiwango hiki. Yaani inakuwa kama upo live na Yesu mwenyewe kumbe ni mchungaji tu.