Huu mchepuko wa aina hii umenishtua kidogo

Huu mchepuko wa aina hii umenishtua kidogo

Wakuu,
Huu mchepuko wa jamaa yangu umenishangaza kidogo.
Twende kwenye point.

Mshikaji anafanya Biashara zake Arusha, juzi Alhamisi akanipigia kuwa anakuja Dar, alikuwa ameagiza gari zake mbili kupitia Befoward.
Aliambia atakuja na mke wake! So nikawapokee JKNIA bad lucky muda alioniambia nilikuwa nje ya town kabisa!!
Nilimwomba jamaa yetu mwingine akawapokee awapeleke hotel [emoji545]

Kuna hotel pale Kariakoo huwa ndio anafikia, nikijua ningewajoin jioni.
Mambo yalienda poa, mshikaji ninamfahamu mke wake vizuri.
Nilivyowakuta yule Mwanamke hakuwa mke wake, nilijiuliza maswali sana! Mshikaji ni msabato 100%...mcha Mungu, mndhamini wa vikundi kanisani kwao, biashara yake inamwingizia kipato kizuri. Anaheshimika, hagusi pombe...

Mwanamke alikuwa mjamzito, jamaa akamtambulisha kuwa ni rafiki yake wa karibu, Mama kijacho wake!!
Nilishtuka sana, baadae jamaa alinijulisha yule Dada ni Mchepuko wake tu, ulioko kwenye system na gari moja ni ya huo mchepuko.

Mke wake hajui chochote, kilichofanya kuandika hapa sio hata kuwa na mchepuko.
Ishu ni kaka mdogo wa mke wa jamaa(mke halisi) aliyejiunga na sisi jana.
Kuna wakati Dada yake alimpigia simu mshikaji na kuomba kuongea na mdogo wake wakati anampa simu jamaa akaiweka loudspeaker? Ili asikie mke wake anasemaje.

Dah mke akamuuliza hapo mko wangapi? Jamaa akamwonyesha shemeji yake kwa ishara ya vidole vi3. Dogo akajibu hivyo hivyo tuko watatu.(heshima iliyojaa uoga) .
Nimemhurumia sana dogo, shemeji yake ana mchepuko mbele yake! Tumempa lift dogo, yeye aliishia Segera anaenda Tanga.

Alipanda gari niliyokua naendesha na Shemeji yake akawa anaendesha hiyo nyingine na mchepuko wake, sisi tulitangulia so tulivyofika segera tuliwasubiri walivyofika, wakaagana fresh na jamaa akamwachia dogo mpunga kidogo.

Tokea Dar nilikuwa najiuliza maswali kibao kichwani, huyu dogo alilichukuliaje hili swala, japokuwa sikutaka tupige stori za hilo jambo kabisa, bahati nzuri muda wote alikuwa ananisimulia mambo ya chuo coz amehitimu mwaka huu.

Sasa hivi tuko Moshi, nitaishia hapa as long as Arusha sio mbali mchepuko ataendesha gari yake!!
Aisee haya maisha ni full of surprises, huyu jamaa kipindi ninaoa muda mwingi alikuwa ananionya niachane na michepuko.

Kumbe na yeye ni jemedari wa mpango wa kando, na alimpa dada wa watu mimba ili asiolewe na mtu mwingine, ubarazuli namtafutia angle yake!! Mbaya zaidi hadi dogo amejua kuwa shemeji yake anamsaliti dada yake.
Nimeamini hakuna mwanaume asiye na mchepuko chini ya hili jua....
Nilichojifunza ni hivi. Mtoto wa kiume aliye na nguvu nzuri kabisa huwezi mzuia na mchepuko hata awe papa, hata awe askofu. Ki asili wanawake wanaweza vumilia lakini mtoto wa kiume aliyebarehe hawezi. Kuna hali fulani hivi ukikaa hata wiki tu mbegu zikajaa kwenye vifuko vyetu hivi unahisi kuwehuka. Unatamani kutongoza kila mwanamke. Afu ikatokea bahati mbaya kuna missed appointment hasira huwa zinakuwa juu sana. So tusimchukulie poa issue ya sex. Ukiona mwanaume mwenzio kaamua kuwa na mchepuko usishangae hakuna mwanaume anaweza vumilia kukaa bila sex. Katika tibu tibu wagonjwa wangu nilikuja kukutana na case ya Askofu akimtongoza sista. Afu sista sasa akagoma. Aise mama mkubwa akashirikiana na askofu kumtenga huyu Sr. Wakawa kama wame dampo hivi Sr aliugua sana psychological. Lakini baada ya matibabu sasa yupo vizuri. Alinusurika kujiua. So issue ya mchepuko haina mbabe 😂 😂 😂 enjoy guys.
 
Nilichojifunza ni hivi. Mtoto wa kiume aliye na nguvu nzuri kabisa huwezi mzuia na mchepuko hata awe papa, hata awe askofu. Ki asili wanawake wanaweza vumilia lakini mtoto wa kiume aliyebarehe hawezi. Kuna hali fulani hivi ukikaa hata wiki tu mbegu zikajaa kwenye vifuko vyetu hivi unahisi kuwehuka. Unatamani kutongoza kila mwanamke. Afu ikatokea bahati mbaya kuna missed appointment hasira huwa zinakuwa juu sana. So tusimchukulie poa issue ya sex. Ukiona mwanaume mwenzio kaamua kuwa na mchepuko usishangae hakuna mwanaume anaweza vumilia kukaa bila sex. Katika tibu tibu wagonjwa wangu nilikuja kukutana na case ya Askofu akimtongoza sista. Afu sista sasa akagoma. Aise mama mkubwa akashirikiana na askofu kumtenga huyu Sr. Wakawa kama wame dampo hivi Sr aliugua sana psychological. Lakini baada ya matibabu sasa yupo vizuri. Alinusurika kujiua. So issue ya mchepuko haina mbabe 😂 😂 😂 enjoy guys.
Aisee
 
Mkuu, huoni kama unahatarisha urafiki wako na jamaa yako? Kama nae member wa JF (kumbuka tunatumia majina bandia humu ) huoni kama nae atasoma uzi wako? Shemeji yako je?
 
Back
Top Bottom