Hussen Bashe, muasi ndani ya CCM(?)

Hussen Bashe, muasi ndani ya CCM(?)

Last edited by a moderator:
Kabisa...... Ni ujasiri wa hali ya juu..... Wale wote waliojikomba kwa mtoto wa Namba 1 leo hii wanakula neema.... Kama Bashe angetaka hizo neema angezila sana.....


Ndugu,

Msipate tabu sana. Wekeni akiba ya maneno. Muda bado. Bashe hajasema kama anagombea Ubunge, na kama anagombea anagombea wapi. Mimi sijasema kama nitagombea Ubunge ama la, na kama nitagombea, basi nitagombea wapi. Kwa sasa nimeweka wazi nia yangu ya kugombea Urais, na ndicho ninachohangaikia kwa sasa. Tulieni.

Na hata kama ikatokea nikagombea Ubunge, na kushindwa, yote matokeo tu. Nitamshukuru Mungu kwa matokeo hayo, kama nilivyofanya mwaka 2010, na kurudi kuendelea na mambo mengine.

Sina na sijawahi kuwa na ugomvi, uadui wala ushindani na Bashe. Nashangaa wapambe wake mnahangaika kushughulika kutuchonganisha watu tusio na ugomvi.

Kuhusu Uteuzi wangu 2010 (Kubebwa): zile zilikuwa ni rehema za Mungu na baraka za vikao, wala siyo mbeleko ya Mama Salma Kikwete, mke wa Rais Kikwete. Ilitokea aliyeshinda (japokuwa kinyemela, alishinda na nilikubali), na mimi niliondoka kurudi kwenye shughuli zangu nikimshukuru Mungu kwa matokeo, japokuwa nilizidiwa ujanja. Lile lilikuwa somo. Na haya matusi, kashfa na kejeli mnazonipa nazichukulia kama ada za shule niliyopata 2010 kwenye kura za maoni na za shule ninayoendelea kusoma. Kama nitagombea tena mwaka huu na miaka mingine ijayo, somo lile litanisaidia. Yaliyotokea 2010 kamwe hayatojirudia. Kwa wapambe wake, hakikisheni bosi wenu amekuwa sawa kwenye mambo ya Uraia ili msijefanya kazi ya kutwanga maji kwenye kinu. Suala la Uraia kwenye uongozi, hakuna serikali huwa inafanya mzaha, hata ulie na kusaga meno, kama hauko sawa kwenye sifa hiyo hakuna chama ama nchi italegeza msimamo wake kwenye sifa hiyo. Ubunge ni nafasi nyeti ya uongozi kwenye Taifa lolote lile. Sikumbuki ni lini vikao vya chama vilijiridhisha juu ya sifa hiyo. Sina hakika kama chama kitameza matapishi yake endapo hali ya Bashe ya Uraia ni kama ilivyokuwa 2010 na ni kama alivyosema aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Lau Masha.

KTY, hili tu huwa linanifanya nishangae watu mnapodhani kuwa Bashe ni mshindani wangu kisiasa Nzega, maana nina uhakika hajawahi kurekebisha makaratasi yake ya Uraia na yuko sawa. Maana, kwa mujibu wa sheria, kama alianza mchakato wa kurekebisha makaratasi yake ya Uraia, basi alipaswa asubiri miaka 10 (akiwa Raia mwema) kabla hajapewa, na katika miaka hiyo 10, hapaswi kujihusisha na mambo ya siasa. Hivyo, wapambe muulizeni kama anagombea ama la! Na kama anagombea, ametatua hili tatizo. Wapambe mtadanganywa kwamba alikatwa jina sababu ya ugomvi wake na Ridhiwan Kikwete, uongo mtupu - Vikao vilivyomkata jina, Ridhiwan hakuwa mjumbe na vilikuwa na wajumbe zaidi ya 20 (CC) na zaidi ya 100 (NEC). Kungekuwa hakuna ushahidi wa kuthibitisha yeye kukosa kwake sifa vikao visingemkata (hao wajumbe ni wengi sana jamani) na zingatia ukweli kwamba tupo kwenye demokrasia ya vyama vingi na yeye alipata kura 14,000+, na aliyefuatia 2000+, na mimi 1800+, hivi chama kina wajumbe 'wehu' kiasi gani wakubali kumkata mtu aliyekubalika namna hii kwenye kura za maoni? Si kingeshindwa na upinzani tu? Tafakari!

Wakatabahu,
HK.

Haya si maneno ya Ngongo,haya ni maneno ya Dr Kigwangalla akiwapa vidonge wapiga debe wa Bashe.
 
haa haa it will be too late...

Natamani ungekuwa unajua behind the scene Mkuu.... Anyway haya mambo ya siasa yaache tu kaka, kuna mengine utayajua siku chache zikazo...... Ngoja ninyamaze, ila soon utaanza kuelewa...
 
Last edited by a moderator:
Kukimbilia Nzega Vijijini haimaanishi Bashe ni raia hivi ni vitu viwili tofuti kabisa.Hoja yangu ni kwamba Bashe ni raia wa makaratasi.Sheria na taratibu zipo wazi kabisa akiataka siasa asubiri hadi mwaka 2020.

Mbona sasa kakimbilia Nzenga kijijini? Na ni Bashe huyo huyo anayemsaidia kumchapa Seleli......
 
Mbona sasa kakimbilia Nzenga kijijini? Na ni Bashe huyo huyo anayemsaidia kumchapa Seleli......

Ocampofour mkuuu hawa hawafaham uwezo binafsi na ushawishi wa Bashe ndio kijana pekeee alieaminiwa na matycoon kupewa mzigo mzitto. Muaminifu, innovative na lobyst mkubwa
 
Last edited by a moderator:
Natamani ungekuwa unajua behind the scene Mkuu.... Anyway haya mambo ya siasa yaache tu kaka, kuna mengine utayajua siku chache zikazo...... Ngoja ninyamaze, ila soon utaanza kuelewa...
kama wewe ni mtu wa nzega ingekuwa bora sana mkfikiria kuwa na mbunge kutoka chama kingine hata TADEA lakin cyo ccm unakopigania bashe kugombea, mtakuwa wajinga wa mwisho kufikiria kuwaamini ccm tena waendelee kuongoza nzega, ccm ambao walidiriki kusimamia lami ipite mjini nzega wakashindwa kuwathamini lami ije tu hata pale stand achilia mbali faida zingine basi angalau adha ya vumbi ipungue, leo bado mnawaona wanafaa, kama si wehu huu ni nini?? mgodi wa wa lusu umefungwa tyr nzega mji wa zamani tena uko njiapanda hauna shule ya kidato cha 5 na 6, hospital hakuna hakuna kitu chochote cha kusisimua uchumi..halafu senti za bashe zinawatia wazimu mwingine..acheni upumbavvu nyie!
 
kama wewe ni mtu wa nzega ingekuwa bora sana mkfikiria kuwa na mbunge kutoka chama kingine hata TADEA lakin cyo ccm unakopigania bashe kugombea, mtakuwa wajinga wa mwisho kufikiria kuwaamini ccm tena waendelee kuongoza nzega, ccm ambao walidiriki kusimamia lami ipite mjini nzega wakashindwa kuwathamini lami ije tu hata pale stand achilia mbali faida zingine basi angalau adha ya vumbi ipungue, leo bado mnawaona wanafaa, kama si wehu huu ni nini?? mgodi wa wa lusu umefungwa tyr nzega mji wa zamani tena uko njiapanda hauna shule ya kidato cha 5 na 6, hospital hakuna hakuna kitu chochote cha kusisimua uchumi..halafu senti za bashe zinawatia wazimu mwingine..acheni upumbavvu nyie!

Hayo yote yasingefanyika kama Bashe angekuwa mbunge 2010..... Naamini akiingia mwaka huu atazidi kusimamia maslahi ya wananchi kwa ujumla wao....

Mimi ni mkazi wa Rorya, nasubiri kwa hamu mtanange wa Lameck Airo (CCM) na Stephene Owawa (Ukawa)....
 
Natamani ungekuwa unajua behind the scene Mkuu.... Anyway haya mambo ya siasa yaache tu kaka, kuna mengine utayajua siku chache zikazo...... Ngoja ninyamaze, ila soon utaanza kuelewa...

Bashe hana tatizo la uraia hilo swala lilisuluhishwa na ni mambo ya utawala, wakati fulani Ally Kesy maarufu Ally Mabodi alikua na mgogoro kama huu tena yeye akiwa mdogo alikua analipiwa ukaaji wake Tz alipogombea kupitia NCCR tunakumbuka kilichotokea, miaka michache badae akagombea kupitia CCM mambo yake yakawa sawa.

CCM ni chama dola wakiamua jambo litakua tu, huu ni wakati mzuri sana kwa Bashe kuliko 2010 kwani wanajua kwamba Bashe alikua upande gani namdifu kwa kujipambanua hii ndiyo siasa yale yamekwisha na amekubali matokeo.

Ajali haiji mara mbili ndiyo kusema hawez kukatwa mara mbili. kila 1437666671750.jpg
 
mkuu hayo yote ni kweli asilimia 100... Umenena vyema sana, watu wanapenda sana kufanya siasa uchwara na kuchafua wale wanaoona ni tishio kwao...

i never real knw the guy but i always like bashe especialy since wamuengue kwa kigezo cha uraia
 
unamjua mungu wewe? Acha kumhusisha mungu kwenye ujinga, wala mungu hambariki mzushi, mwenye chuki, asie na adabu,,nk mshaurini bashe wenu atafakari vyema, sababu zilizomtoa 2010 bado zipo hatapitishwa, kilichomtokea aliekuwa anamsapoti kwenye harakati za urais kitamtokea yeye pia..mwambieni u o n g o z i si kufurahisha watu kwa kuwapa fedha au mtaji, chunga sana, sidhani km watu wa nzega na ccm watakuwa wajinga kumpitisha mtu wa hivi..

hivi kiswahili ni kigumu kiasi hichi au mahaba tu yanakutuma?

Wapi nilipoonesha namsapoti au kumjua bashe?
Shame on u mazafanta
 
Mjinga wewe. Nani kakuambia hana uwezo wa kulipa elfu 20 secondary ya kata?
 
Nomile

1. Kipindi Bashe anaingia Habari Cop kama CEO alikuta wafanyakazi hawapati mshahara zaidi ya miezi 4 mpaka 5, leo hii ukienda pale utakuta kila mwisho wa mwezi wafanyakazi wanakenua meno....

2. Bashe leo hii kawawezesha wafanyakazi wote bila kujali nafasi zao kupata mikopo ya magari. Leo hii mpaka mhudumu anaendesha verosa au Rav 4. Hata BOT hawawezi kufanya hivyo...

3. Bashe kipindi anaingia kampuni ilikuwa inachapisha Jamana, ila leo hii kafunga mashine mbili mpya kabisa kwa ajili ya uchapishaji na magazeti ya Nipashe yataanza kuchapishwa hapo Sinza kwa muda kabla mashine yao kuwa tayari...

4. Kima cha chini cha mshahara ni 360,000 Tsh. Huyo ni mfagiaji. Unataka afanye nini jamani, kama sio upumb.vu kuongea vitu usivyovijua....

5. Leo hii wafanyakazi wanakopa banki ya CBA. Ni mara ya kwanza tokea Uhuru kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo kuwa na uwezo wa kukopa benki...

6. Bashe kafanikiwa kujenga majengo mawili yenye ofisi zaidi ya 26 kwa kipindi kifupi alichokaa pale. Ulitaka afanye nini?

7. Ni kampuni hiyo ndio inaongoza kwa kuwa na waandishi wenye ueledi wa hali ya juu kama Msacky na Kibanda. Unataka afanye nini cha ziada?.

8. Bashe kila ijumaa anatoa sadaka wa wahitaji zaidi ya million 1mpaka 3, kama unataka kuthibitisha ijumaa pita pale Sinza kijiweni ushuhudie foleni. Unataka nini cha ziada?

9. Ni kampuni hiyo inayosomesha zaidi ya wanafunzi 400 Tanzania nzima, wengi wao wakiwa wakazi wa Nzenga wasio na uwezo wa kulipa ada. Unataka afanye nini cha ziada kama sio uji.nga wako na upumba.vu wako...

10. Leo hii Habari cop sio ile ya zamani. Amefanya ukarabati ofisi zote, eneo la nje, ukuta nk....

Utachafua watu wote lakini kamwe huwezi kumchafua Bashe, tena una bahati sana, ukiongea hayo maneno mbele ya vijana walahi utapata kipigo cha milele....

Ni kweli mkuu New Habari chini ya Bashe imekuja na mapinduzi chanya kwa wafanyakazi, mi ni mmoja wa wanufaika wa hayo usemayo, mtu ahukumiwe kwa haki si kwa majungu
 
mkuu hamisi kakimbia jimbo la nzega mjini ameenda jimbo jipya, kamkimbia bashe. bahati mbaya na seleri nae kamkimbia bashe wameenda kupambana na kingwangala. wote anajua kua hawamuwezi hussein bashe. mleta mada nadhani ameliona hilo na anachuki binafsi that why anasema akatwe maana kwa kupiga kula hawamuwezi bwana bashe.


Hamis Kigwangala anamuogopa sana Bashe..Kigwangala alizawadiwa ubunge kwa kujipendekeza kwa rizwani,,Sasa hivi hakuna wa kumbeba ubunge atausikia redioni tu.. Wana nzega wanamtaka Bashe
 
haya tutajie wewe kiongozi mzuri sisi watu wanzega, wewe sindio kitengo haya sema sasa.maana sisi tunamtaka bashe wewe unataka kutuchagulia nani mwaka huu mkuu. tujibu kabla ya tarehe 1 next month


Jifunze kuifikirisha akili yako kwa upeo mpana, usituonyeshe kuwa una akili size ya kifaranga cha kuku, hufikirii mbali zaidi ya unapoona..tafuta sifa za kiongozi mzuri uwasaidie watu wa nzega kujua kiongozi mzr ni yupi, hata watz wngn..
 
Back
Top Bottom