wiseboy
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 2,931
- 3,299
hongereni kwa kuivuka pasaka tukiwa na uhai. (TUMSHUKURU ADENAI). Ni tumaini langu kuwa hapa jf ni kama chungu kilichobeba kila aina ya watu, wakubwa, watoto, wafanyakazi, wanafunzi n.k. Tatizo ni kwamba hapa mtaani kwetu kuna binti kanitia huruma na sina uwezo wa kumsaidia bnafsi ndo maana nimeamua kuleta hapa suala lake mnisaidie tatizo lake. Huyu binti alifiwa na mama yake akiwa na miaka 6. baada ya .hapo amelelewa na baba ake mzazi hadi alipofika kidato cha 4 mwaka jana. Akiwa kwenye mitihania kwa bahati mbaya baba ake naye akafariki kwa ajali ya gari, baada ya matokeo mwaka huu hakubahatika kufaulu kwenda 4m 5. Kusema ukweli ana maisha magumu sana na hana wa kumsaidia, hvyo amekuja kwangu na kuniomba nimsaidie sehemu angalau ya kupata kibarua, ki ukweli uso wake unatia huruma na mm bdo mwanafunzi na sina chanel ya vibarua, kama kuna m2 anachanel ya kazi naomba msaada wake. Nategemea msaada wenu tumsaidie yatima huyu anayekata tamaa ya kuishi. KARIBUNI