Kuna mchangiaji mmoja kasema you sound like him, huwezi mlinganisha Nape na Zitto wala Lissu, tunajua Zitto alivyotetea maslahi ya taifa tuambie toka Nape awe vuvuzela amelisaidia nini taifa zaidi ya m/kiti wake? usichanganye mambo ya kitaifa na kichama, Nape kapewa cheo (miezi kama 8) lakini muda wote kautumia kupambana na Chadema na kuchonganisha wanachama wenzake sasa mtu kama huyu utamfananisha na Zitto au hata Mnyika mara kumi useme hata January kajaribu kutetea kwenye kamati ya nishati.Naona ama kweli kumbe Nape ni tishio la wapenzi wa Chadema walioko humu ndani jamvini,Reality na sio facts wakimfukuza NAPE kwa na sio LOWASA kwa sasa CCM inavunjika kuliko angeondoka Lowasa japo Ukweli wa RICHMOND unaanza kuwa wazi,lakini sioo kuwa unamuondolea kitanzi cha lawama.Lakini kwa waelevu inaleta hoja kubwa zaidi ya kwani kama sifa hizo za utendaji wenye kubeba sifa ya kujiudhuru kulinda kitu ambacho kimekuja kuwa ni donda la AIBU YA TAIFA.Je kuna stahiki yoyote ya kuaminiwa tena.
Kama kuna mpango wowote kumuondoa kijana NAPE,ambae kwa namna fulani amesaidia sana kubadilisha UPEPO wa mwelekeo wa SIASA za CCM hakika toka kipande kile CHADEMA na watanzania wako kwenye pick ya kulalama UKAIBUKA mpango wa kuijvua gamba ambao ulipigiwa chepuo na vinala kibao kisha mbele ya safari wengineo wote walijitoa akabaki kijana Nape ambae spirit yake inanguvu kwa kuwa na sifa kubwa mbili moja ni UJANA na ya PILI,ni aina sahihi ya kizazi cha nyakati [Generation Era]. Hakika nyuma ya NAPE kuna watu makini [NJE YA MAFISADI] watakaoibuka ambao wamekaa pembeni wakiangalia SYNTHESIS ambayo inajaribu kutafuta JIBU LA KWELI NA KUIBUKA KWA DHANA MPYA KAMA CCM IFE AU CCM IZALIWE UPYA.
1: CCM IFE [kama itaendelea kuwabeba watuhumiwa na wale wote jamii inayowapigia kelele kuwa hawatakiwi ndani ya CCM NA SERIKALI]
2: CCM IZALIWE UPYA-[Kuwaondoa viongozi wote watuhumiwa wa UFISADI na ikibidi kuwafukuza ndani ya chama na kuwekwa kwa kanuni mpya ikiwemo kuanzishwa kwa sheria za wafanyabiashara kutokupewa madaraka ndani ya CCM huku wakiwa ni washriki wa biashara zao na kuweka wazi masharti na kanuni zenye kutoa haki sawa kwa mwanachama yoyote kuwa na ushiriki wa haki na sio wa rushwa kwenye chaguzi na maamuzi ya chama.
Nape ni kizazi cha upambandaji wa kijamii dhidi ya kinanchopaswa kuondoka na kinachotegemea kubaki na kuendeleza maisha kwa miaka 30 mpaka 50 ijayo.Nape ni kizazi cha kushinda na wakina ZITO,TINDU LISSU na wengineo kwa mujibu wa ITIKADI za vyama vyao.Hivyo CCM kukaa na kuanza kupoteza muda wa kujadili POSITIVE efforts za kuhujumu bidii za NAPE ambazo kwa ukweli ndizo REALITY [Hata kwa favour ya nature na spiritual wise] ambayo ni sawa na kumzuia LISSU au ZITTO kuwakilisha hoja yayote ya msingi dhidi ya TAIFA,basi nikushindana na NATURE na mwisho wake ni AIBU mara dufu.
Hivi rudi nyuma enzi ya ZITTO alipokuwa akipambana na WALAJI WA KEKI YA TAIFA, kuna mambo yalipita mengi sana dhidi yake lakini kwa kuwa asilia [nature] inamsimamia kwa mujibu ya dhana ya kizazi kipya na zama ya wengi, baadhi ya watu waliumia na nguvu iliyokuwa nyuma ya ZITTO ambayo ni umma,baada ya kuibuka kutaka kumnyamazisha,asizungumze ukweli kwa niaba ya kizazi kilichopo na kijacho.
Leo hii kwenye upinzani nguvu hiyo unaweza kuiona kwa TINDU LISSU,na kwa CCM nguvu hiyo iko kwa NAPE,kwa wanaojua how nature works na wenye kuheshimu uwepo wa Mungu wanajua nguvu hizo,hivyo sio za kupingana nazo bali kuzifuata vinginevyo ni kuzalishwa kwa aibu na majanga yasioweza kuelezeka kwa binadamu wasio tambua kuwa kuna nguvu za MUNGU zinaojua HILA [UONGO] na UKWELI unaozalishwa na sisi binadamu,kwa nia na makusudio na faida binafsi.
Na mbaya zaidi nyuma ya nguvu hiyo watu hawa wanakuwa walishaanza mapambano toka kwenye damu za mama na baba zao.LEO hii wakati nguvu ya LOWASA ni moja kuwa yeye ndiye uzao wa kwanza kwenye madaraka ya CCM kwa nguvu hiyo.NAPE na MAKONGORO kila mmoja ana nguvu mbili mpaka tatu za ziada kutokana na kuwa imekua hivyo ndani ya toka kwa wazazi.Na ndio maana Makongoro aliweza kusema yale ambayo ndani ya CCM wengine hawakuweza kusema kwa kumwambia Mwenyekiti wake Taarifa kutoka SITE [KWA WATANZANIA] juu ya RACHEL.Ile dare au uthubutu hauji hivi hivi uko ndani ya damu na uthubutu huo ndio huo wa wa NAPE.
Na hakika kama kweli wamempeleka kwenye CC,ni kualika Majanga ya ndani ya CCM na SERIKALI yake kwa kuwa muda huo ungetumika kuzungumzia madhara ya UFISADI ndani CCM na taarifa nyingine za msingi za kuludisha matumaini ya Watanzania ya kuichoka CCM,na nini kifanywe kuludisha Mapenzi hayo kwa Umma.
Yakiendelea hapo mtoto wa muhasisi wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere,aliposimama akamuuliza Mwenyekiti wake kuwa alipowainua mikono RACHEL wakati wa uchaguzi 2010,Wananchi walisema HII NDIYO NINI?Basi wajue Swali lile bado Wananchi awajajibiwa hivyo wasikimbie kuzima moto kwa Mtungi wa Gasi ya Kupikia,badala ya kutumia Fire Extinguisher.
JohnShaaban kuna wengine huwa ni wasema kweli, Nape hana kosa lolote kuzunguka na kueneza yaliyokubaliwa na NEC (kama yapo) lakini kaponzwa na ujinga wake narudia ujinga wake wa kutokubali ushauri alokuwa anapewa kuwa amewekwa pale kama chambo la wakubwa kutimiza malengo yao baadae atatupwa. Lakini sina tatizo kama alikuwa najua mwisho wake utakuwa huu.Watanzania tuna matatizo makubwa sana ya kimantiki.
Humu jamvini ukiuliza wangapi wanaamini EL na Chenge ni wachafu, zaidi ya 70% watajibu "yes". Sasa:
Nashangazwa na wachangiaji hapa, maana wapo wanaosema EL for presidency 2015. Lakini, wanaomkandia Nape, ndio haohao wanakataa EL kuwa rais; nini msimamo wenu?
- tunataka malaika aje kusema uchafu wao?!
- Nini kosa la Nape kuzunguka na kusema ukweli kama tunaamini hawa jamaa ni wachafu?!
- bado tuko kwenye zama za funika uchafu kwenye carpet kumfurahisha mtu?!
- kama tunadhani approach ya Nape haikuwa nzuri, nini mbadala -- tuendelee kunywa nao chai?!
Tumerogwa?????
... Na nikweli kuwa kabla Nape na Chilgati hawajachukuliwa hatua ... Mwenyekiti wao aliyeasisi mchakato huo je yeye atakuwa kwenye nafasi gani?
Maskini vuvuzela! Alikuwa mjumbe kwenye halmashauri kuu ya uvccm. Akaamua kugombea uenyekiti wa uvccm na sera ya kuwashtaki EL kwa kusaini mkataba wakinyonyaji kwenye ujenzi wa jengo jipya la jumuia yao.
Akaishia kufukuzwa na kufungiwa "mbinguni na duniani". Kwa huruma ya m/kiti akapewa ukuu wa wilaya na hatimae ukatibu uenezi kwenye chama. Hata mwaka haujaisha, tayari sera ya kuvuana magamba imemgeuka!
Sasa wanataka kumvua yeye na wao (aliowaita magamba) wabaki. Mtoto anabahati mbaya sana huyu. Bora aachane na siasa akafanye kazi yake ya kichungaji aliyoisomea. Ni ushauri tu!
Kwani ameshachukua fomu?Watu unajua ni wapayukaji sana hawamjui lowassa vizuri...yaaani huyu jamaa anachukua uraisi hivi hivi
Kuna mchangiaji mmoja kasema you sound like him, huwezi mlinganisha Nape na Zitto wala Lissu, tunajua Zitto alivyotetea maslahi ya taifa tuambie toka Nape awe vuvuzela amelisaidia nini taifa zaidi ya m/kiti wake? usichanganye mambo ya kitaifa na kichama, Nape kapewa cheo (miezi kama 8) lakini muda wote kautumia kupambana na Chadema na kuchonganisha wanachama wenzake sasa mtu kama huyu utamfananisha na Zitto au hata Mnyika mara kumi useme hata January kajaribu kutetea kwenye kamati ya nishati.
mnachanganya mambo vijana hali ni tete kwa lowassa ndio maana analia lia apate wa kufa nae,kiufupi yeye lengo lake lilikua suala hilo la kujivua gamba lizikwe na nec ambako aliamini na ana wafuasi wengi,wapinzani wake hawakutaka nec ishughulike na suala hilo bali walitaka nec itoe kibali kwa kamati kuu kushughulika na hilo ambako huyo nape na chiligati ni wajumbe,lowassa hayumo kwenye kamati kuu na pia hana ushawishi,na kwa kuwakumbusha zaidi chiligati pia ni mjumbe wa kamatia ya maadili pia!
Kamati ya Maadili ina wajumbe wazito, baadhi yao ni: Mwenyekiti Kikwete, Makamu wenyeviti, Pius Msekwa na Amani Karume, Makamu wa Pili wa SMZ, Balozi Seif Iddi,Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu, Wilson Mukama na Manaibu Katibu Mkuu, Kapteni mstaafu John Chiligati na Vuai Ali Vuai.
Hawa ndio watakaomshughulikia Lowassa!!!!
hebu acha tabia ya kuropoka.hujui nini kinaendelea. hivi unafikiri nape anaweza kuzunguka nchi nzima na kuwalaani mafisadi bila baraka za mwenyekiti wake wa chama? au umeamua kuropoka tu kwa sababu umepewa mdomo wa kuongea. acha ushabiki wa kijinga. hujui unaongea nini wewe.hivi unafikiri kikwete yeye ni mjinga wa kukubali toka mwanzo ripoti ile ya richmond kusomwa hadharani wakati yeye alikuwa anajua fika kuwa lowasa amehusika kwenye mchezo mzima?jk angeweza kukataa ripoti ile isisomwe pale bungeni, lakini kwa sababu alijua lowasa ni mwizi ndio akaamua kumuumbua pale kwa staili ile ya kusomwa ripoti. na kwa taarifa yako lowasa atamalizwa keshokutwa kwenye kikao cha cc. acha kutetea ujinga ambao utakugharim hata wewe filipo.acha mawazo ya kitoto. haihitaji ufike udsm kutambua haya ninayokueleza filipo.lowasa, chenge na rostam wote ni wezi wakubwa.
hebu acha tabia ya kuropoka.hujui nini kinaendelea. hivi unafikiri nape anaweza kuzunguka nchi nzima na kuwalaani mafisadi bila baraka za mwenyekiti wake wa chama? au umeamua kuropoka tu kwa sababu umepewa mdomo wa kuongea. acha ushabiki wa kijinga. hujui unaongea nini wewe.hivi unafikiri kikwete yeye ni mjinga wa kukubali toka mwanzo ripoti ile ya richmond kusomwa hadharani wakati yeye alikuwa anajua fika kuwa lowasa amehusika kwenye mchezo mzima?jk angeweza kukataa ripoti ile isisomwe pale bungeni, lakini kwa sababu alijua lowasa ni mwizi ndio akaamua kumuumbua pale kwa staili ile ya kusomwa ripoti. na kwa taarifa yako lowasa atamalizwa keshokutwa kwenye kikao cha cc. acha kutetea ujinga ambao utakugharim hata wewe filipo.acha mawazo ya kitoto. haihitaji ufike udsm kutambua haya ninayokueleza filipo.lowasa, chenge na rostam wote ni wezi wakubwa.