Huruma ya CC ndiyo pona ya Chiligati na Nape

Kwani kama walienda mikoani kusemea yale waliokubaliana kuna ubaya gani? Basi kama wanastahili kuondolewa basi na mwenyekiti nae hafai kuongoza chama na yote kwa yote huo ulikuwa ni utetezi wa Edo, kumbuka hii ni kama mchezo wa karata 3......hivyo kugeuziwa kibao ni kawaida ila ni wakati muafaka sasa wa chama kuachana na sera za kujivua gamba na ijulikana kwamba chama hiki kiko kwa ajili ya matajiri na wafanya biashara kwani ile kusema ni chama cha wakulima na wafanya kazi inanipa walakini....na hiyo kauli mbiu vyema ikabadilika na itafutwe kauli mbiu nyingine itakayoendana na chama jinsi kilivyo kwa sasa. Maamuzi magumu yanahitaji mioyo migumu pia! Hebu sasa ifanyeni mioyo yenu kuwa migumu kwani ndo mtaweza kufanya maamuzi magumu.....Ah..wacha nichukue nafasi hii kuwapongeza ANC..juu ya Malema (wameweza).
 
Naona ama kweli kumbe Nape ni tishio la wapenzi wa Chadema walioko humu ndani jamvini,Reality na sio facts wakimfukuza NAPE kwa na sio LOWASA kwa sasa CCM inavunjika kuliko angeondoka Lowasa japo Ukweli wa RICHMOND unaanza kuwa wazi,lakini sioo kuwa unamuondolea kitanzi cha lawama.Lakini kwa waelevu inaleta hoja kubwa zaidi ya kwani kama sifa hizo za utendaji wenye kubeba sifa ya kujiudhuru kulinda kitu ambacho kimekuja kuwa ni donda la AIBU YA TAIFA.Je kuna stahiki yoyote ya kuaminiwa tena.

Kama kuna mpango wowote kumuondoa kijana NAPE,ambae kwa namna fulani amesaidia sana kubadilisha UPEPO wa mwelekeo wa SIASA za CCM hakika toka kipande kile CHADEMA na watanzania wako kwenye pick ya kulalama UKAIBUKA mpango wa kuijvua gamba ambao ulipigiwa chepuo na vinala kibao kisha mbele ya safari wengineo wote walijitoa akabaki kijana Nape ambae spirit yake inanguvu kwa kuwa na sifa kubwa mbili moja ni UJANA na ya PILI,ni aina sahihi ya kizazi cha nyakati [Generation Era]. Hakika nyuma ya NAPE kuna watu makini [NJE YA MAFISADI] watakaoibuka ambao wamekaa pembeni wakiangalia SYNTHESIS ambayo inajaribu kutafuta JIBU LA KWELI NA KUIBUKA KWA DHANA MPYA KAMA CCM IFE AU CCM IZALIWE UPYA.
1: CCM IFE [kama itaendelea kuwabeba watuhumiwa na wale wote jamii inayowapigia kelele kuwa hawatakiwi ndani ya CCM NA SERIKALI]
2: CCM IZALIWE UPYA-[Kuwaondoa viongozi wote watuhumiwa wa UFISADI na ikibidi kuwafukuza ndani ya chama na kuwekwa kwa kanuni mpya ikiwemo kuanzishwa kwa sheria za wafanyabiashara kutokupewa madaraka ndani ya CCM huku wakiwa ni washriki wa biashara zao na kuweka wazi masharti na kanuni zenye kutoa haki sawa kwa mwanachama yoyote kuwa na ushiriki wa haki na sio wa rushwa kwenye chaguzi na maamuzi ya chama.

Nape ni kizazi cha upambandaji wa kijamii dhidi ya kinanchopaswa kuondoka na kinachotegemea kubaki na kuendeleza maisha kwa miaka 30 mpaka 50 ijayo.Nape ni kizazi cha kushinda na wakina ZITO,TINDU LISSU na wengineo kwa mujibu wa ITIKADI za vyama vyao.Hivyo CCM kukaa na kuanza kupoteza muda wa kujadili POSITIVE efforts za kuhujumu bidii za NAPE ambazo kwa ukweli ndizo REALITY [Hata kwa favour ya nature na spiritual wise] ambayo ni sawa na kumzuia LISSU au ZITTO kuwakilisha hoja yayote ya msingi dhidi ya TAIFA,basi nikushindana na NATURE na mwisho wake ni AIBU mara dufu.

Hivi rudi nyuma enzi ya ZITTO alipokuwa akipambana na WALAJI WA KEKI YA TAIFA, kuna mambo yalipita mengi sana dhidi yake lakini kwa kuwa asilia [nature] inamsimamia kwa mujibu ya dhana ya kizazi kipya na zama ya wengi, baadhi ya watu waliumia na nguvu iliyokuwa nyuma ya ZITTO ambayo ni umma,baada ya kuibuka kutaka kumnyamazisha,asizungumze ukweli kwa niaba ya kizazi kilichopo na kijacho.

Leo hii kwenye upinzani nguvu hiyo unaweza kuiona kwa TINDU LISSU,na kwa CCM nguvu hiyo iko kwa NAPE,kwa wanaojua how nature works na wenye kuheshimu uwepo wa Mungu wanajua nguvu hizo,hivyo sio za kupingana nazo bali kuzifuata vinginevyo ni kuzalishwa kwa aibu na majanga yasioweza kuelezeka kwa binadamu wasio tambua kuwa kuna nguvu za MUNGU zinaojua HILA [UONGO] na UKWELI unaozalishwa na sisi binadamu,kwa nia na makusudio na faida binafsi.

Na mbaya zaidi nyuma ya nguvu hiyo watu hawa wanakuwa walishaanza mapambano toka kwenye damu za mama na baba zao.LEO hii wakati nguvu ya LOWASA ni moja kuwa yeye ndiye uzao wa kwanza kwenye madaraka ya CCM kwa nguvu hiyo.NAPE na MAKONGORO kila mmoja ana nguvu mbili mpaka tatu za ziada kutokana na kuwa imekua hivyo ndani ya toka kwa wazazi.Na ndio maana Makongoro aliweza kusema yale ambayo ndani ya CCM wengine hawakuweza kusema kwa kumwambia Mwenyekiti wake Taarifa kutoka SITE [KWA WATANZANIA] juu ya RACHEL.Ile dare au uthubutu hauji hivi hivi uko ndani ya damu na uthubutu huo ndio huo wa wa NAPE.

Na hakika kama kweli wamempeleka kwenye CC,ni kualika Majanga ya ndani ya CCM na SERIKALI yake kwa kuwa muda huo ungetumika kuzungumzia madhara ya UFISADI ndani CCM na taarifa nyingine za msingi za kuludisha matumaini ya Watanzania ya kuichoka CCM,na nini kifanywe kuludisha Mapenzi hayo kwa Umma.

Yakiendelea hapo mtoto wa muhasisi wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere,aliposimama akamuuliza Mwenyekiti wake kuwa alipowainua mikono RACHEL wakati wa uchaguzi 2010,Wananchi walisema HII NDIYO NINI?Basi wajue Swali lile bado Wananchi awajajibiwa hivyo wasikimbie kuzima moto kwa Mtungi wa Gasi ya Kupikia,badala ya kutumia Fire Extinguisher.

Kuna mchangiaji mmoja kasema you sound like him, huwezi mlinganisha Nape na Zitto wala Lissu, tunajua Zitto alivyotetea maslahi ya taifa tuambie toka Nape awe vuvuzela amelisaidia nini taifa zaidi ya m/kiti wake? usichanganye mambo ya kitaifa na kichama, Nape kapewa cheo (miezi kama 8) lakini muda wote kautumia kupambana na Chadema na kuchonganisha wanachama wenzake sasa mtu kama huyu utamfananisha na Zitto au hata Mnyika mara kumi useme hata January kajaribu kutetea kwenye kamati ya nishati.
 
Watanzania tuna matatizo makubwa sana ya kimantiki.
Humu jamvini ukiuliza wangapi wanaamini EL na Chenge ni wachafu, zaidi ya 70% watajibu "yes". Sasa:
  • tunataka malaika aje kusema uchafu wao?!
  • Nini kosa la Nape kuzunguka na kusema ukweli kama tunaamini hawa jamaa ni wachafu?!
  • bado tuko kwenye zama za funika uchafu kwenye carpet kumfurahisha mtu?!
  • kama tunadhani approach ya Nape haikuwa nzuri, nini mbadala -- tuendelee kunywa nao chai?!
Nashangazwa na wachangiaji hapa, maana wapo wanaosema EL for presidency 2015. Lakini, wanaomkandia Nape, ndio haohao wanakataa EL kuwa rais; nini msimamo wenu?

Tumerogwa?????
JohnShaaban kuna wengine huwa ni wasema kweli, Nape hana kosa lolote kuzunguka na kueneza yaliyokubaliwa na NEC (kama yapo) lakini kaponzwa na ujinga wake narudia ujinga wake wa kutokubali ushauri alokuwa anapewa kuwa amewekwa pale kama chambo la wakubwa kutimiza malengo yao baadae atatupwa. Lakini sina tatizo kama alikuwa najua mwisho wake utakuwa huu.
 
kwa sarakasi zilizopo ndani ya magamba, hakuna kitu ambacho tunaweza kuwaamini. Nape sasa sijui atakuwa nakisemea chama gani. maana huko aliko amezodolewa na kupgwa masinge ya nguvu.
 
Nape kaponza na kutumiwa na watu wenye interest ya urais 2015,kwakuwa yeye upeo wake mdogo wa kusoma mambo akajikuta anakurupuka,ni bora angebaki na CCJ kama mwaasisi na kukipigania chama chake kikapata usajili wa kudumu kuliko kufanya mazingaombwe yaliyo mgharimu.CCM ina wenyewe na wenyewe wameshamgeuka kilichobaki sasa ni visasi.Ushauri wa bure kwa Nape na mwenzake Chiligati,ni wakati wao sasa nao kumgeuka m/kiti na kuweka mambo hadharani.Kila mtu anajua kuwa m/kiti ndiye aliyemtuma sasa anakana ili tumueleweje?Chenge alisema wakimwaga mboga yeye anamwaga ugali,sasa wamemwaga mboga na ugali Nape na Chilligati watamwaga nini?Kumbe gamba lililokuwa linasubiriwa ni Nape?Yuko wapi Makongoro Nyerere,mbona amenyamza kimya ilihali chama kinachezewa?

Nafikiri ni wakati mwafaka kwa chama kutoa maamuzi magumu kwa mwenyekiti wake kuupotosha umma ilihali akijua kuwa yeye ndiyo gamba lililokuwa linastahili kuvuliwa.tunachosubiri ni CCM kuacha unafiki na kumvua kofia mwenyekiti kwa kushindwa kukiongoza chama na kuendeleza majungu na magawanyo wa kimakundi ndani ya chama.Aliwahi kutamka kuwa anayoyasema Nape yana baraka zake kama m/kiti na baraka za chama sasa leo anaposema chama hakikumtuma anamaanisha nini?Na kwa wadhifa wake ilitosha kumwita Nape nakumuuliza haya mambo ya kuchafua watu unayapata wapi,ikibidi na kuwaadhibu kwa mujibu wa kanuni za chama.

Ili CCM ipone 2015 lazima JK awajibishwe,angalau wananchi tutakuwa na imani na CCM.Kama ndiyo staili ya funika kombe mwanaharamu apite mmekwisha,mnatakiwa kusoma alama za nyakati bila kujali nani ni nani.Ninapozungumzia m/kiti kushindwa majukumu yake ni kwamba akiwa rais na m/kiti wa baraza la mawaziri ameshindwa kudhibiti mfumuko wa bei kwa kipindi chake chote alichopo madarakani lakini si hilo tuu,kama m/kiti wa chama anashangaa serikali anayoiongoza kushindwa kuwadhibitiwa wafanyabiashara kwa kupandisha bei za mafuta,hivi kama kweli huu si usanii nini?Yawezekana hajui majukumu yake!
 
Mnaomtetea nape hamjajua tatizo lake. Kwanzaa yeye indoo amesababisha tote Hays yakampata! Kikubwa Hana msimamo , juzi kaitisha wanahabari akijipinga yeye mwenyewe hajawahi kuwataja kama wao ni wahusika wakujivua Gambia. Haya Akane na huko! Inamaana anawaogopa NA sio mpambanaji
 
... Na nikweli kuwa kabla Nape na Chilgati hawajachukuliwa hatua ... Mwenyekiti wao aliyeasisi mchakato huo je yeye atakuwa kwenye nafasi gani?


mnachanganya mambo vijana hali ni tete kwa lowassa ndio maana analia lia apate wa kufa nae,kiufupi yeye lengo lake lilikua suala hilo la kujivua gamba lizikwe na nec ambako aliamini na ana wafuasi wengi,wapinzani wake hawakutaka nec ishughulike na suala hilo bali walitaka nec itoe kibali kwa kamati kuu kushughulika na hilo ambako huyo nape na chiligati ni wajumbe,lowassa hayumo kwenye kamati kuu na pia hana ushawishi,na kwa kuwakumbusha zaidi chiligati pia ni mjumbe wa kamatia ya maadili pia!



Kamati ya Maadili ina wajumbe wazito, baadhi yao ni: Mwenyekiti Kikwete, Makamu wenyeviti, Pius Msekwa na Amani Karume, Makamu wa Pili wa SMZ, Balozi Seif Iddi,Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu, Wilson Mukama na Manaibu Katibu Mkuu, Kapteni mstaafu John Chiligati na Vuai Ali Vuai.

Hawa ndio watakaomshughulikia Lowassa!!!!
 
Maskini vuvuzela! Alikuwa mjumbe kwenye halmashauri kuu ya uvccm. Akaamua kugombea uenyekiti wa uvccm na sera ya kuwashtaki EL kwa kusaini mkataba wakinyonyaji kwenye ujenzi wa jengo jipya la jumuia yao.

Akaishia kufukuzwa na kufungiwa "mbinguni na duniani". Kwa huruma ya m/kiti akapewa ukuu wa wilaya na hatimae ukatibu uenezi kwenye chama. Hata mwaka haujaisha, tayari sera ya kuvuana magamba imemgeuka!

Sasa wanataka kumvua yeye na wao (aliowaita magamba) wabaki. Mtoto anabahati mbaya sana huyu. Bora aachane na siasa akafanye kazi yake ya kichungaji aliyoisomea. Ni ushauri tu!

hebu acha tabia ya kuropoka. hujui nini kinaendelea . hivi unafikiri nape anaweza kuzunguka nchi nzima na kuwalaani mafisadi bila baraka za mwenyekiti wake? au umeamua kuropoka tu kwa sababu umepewa mdomo wa kuongea.acha ushabiki wa kijinga.
 
hebu acha tabia ya kuropoka.hujui nini kinaendelea. hivi unafikiri nape anaweza kuzunguka nchi nzima na kuwalaani mafisadi bila baraka za mwenyekiti wake wa chama? au umeamua kuropoka tu kwa sababu umepewa mdomo wa kuongea. acha ushabiki wa kijinga. hujui unaongea nini wewe.hivi unafikiri kikwete yeye ni mjinga wa kukubali toka mwanzo ripoti ile ya richmond kusomwa hadharani wakati yeye alikuwa anajua fika kuwa lowasa amehusika kwenye mchezo mzima?jk angeweza kukataa ripoti ile isisomwe pale bungeni, lakini kwa sababu alijua lowasa ni mwizi ndio akaamua kumuumbua pale kwa staili ile ya kusomwa ripoti. na kwa taarifa yako lowasa atamalizwa keshokutwa kwenye kikao cha cc. acha kutetea ujinga ambao utakugharim hata wewe filipo.acha mawazo ya kitoto. haihitaji ufike udsm kutambua haya ninayokueleza filipo.lowasa, chenge na rostam wote ni wezi wakubwa.
 
Ni kweli Nape na Chiligati walizunguka nchi nzima wakitaja majina ya wanaotakiwa kujiondoa CCM bila kutumwa na mtu? Inawezekana kweli hii?
 
Kuna mchangiaji mmoja kasema you sound like him, huwezi mlinganisha Nape na Zitto wala Lissu, tunajua Zitto alivyotetea maslahi ya taifa tuambie toka Nape awe vuvuzela amelisaidia nini taifa zaidi ya m/kiti wake? usichanganye mambo ya kitaifa na kichama, Nape kapewa cheo (miezi kama 8) lakini muda wote kautumia kupambana na Chadema na kuchonganisha wanachama wenzake sasa mtu kama huyu utamfananisha na Zitto au hata Mnyika mara kumi useme hata January kajaribu kutetea kwenye kamati ya nishati.

Mimi ndio niliyetoa kauli hiyo.
Kama utakuwa makini na kupitia thread yake kwa umakini.utaweza gundua ni jinsi gani anavyojitaidi kujifananishe yeye(DSN=NAPE) na viongozi fulalanifulani wa CDM.
Kwa mlinganisho huo wa ndugu DSN utaweza gundua yeye ni nani(kwa nature yake).
 
mnachanganya mambo vijana hali ni tete kwa lowassa ndio maana analia lia apate wa kufa nae,kiufupi yeye lengo lake lilikua suala hilo la kujivua gamba lizikwe na nec ambako aliamini na ana wafuasi wengi,wapinzani wake hawakutaka nec ishughulike na suala hilo bali walitaka nec itoe kibali kwa kamati kuu kushughulika na hilo ambako huyo nape na chiligati ni wajumbe,lowassa hayumo kwenye kamati kuu na pia hana ushawishi,na kwa kuwakumbusha zaidi chiligati pia ni mjumbe wa kamatia ya maadili pia!



Kamati ya Maadili ina wajumbe wazito, baadhi yao ni: Mwenyekiti Kikwete, Makamu wenyeviti, Pius Msekwa na Amani Karume, Makamu wa Pili wa SMZ, Balozi Seif Iddi,Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu, Wilson Mukama na Manaibu Katibu Mkuu, Kapteni mstaafu John Chiligati na Vuai Ali Vuai.

Hawa ndio watakaomshughulikia Lowassa!!!!

pole sana endelea kuota mchana!
 
kuna mtu humu jamvini aliwahi sema kuwa JK anamtumia huyu dogo!! tukamporomoshea maneno! sasa tumeona jinsi alivyomkana!!
JK NOMA JAMANI!!
 
Dunia haitabiriki, CCM haitabiriki chochote chaweza tokea wakati wowote; aliyekuwa anataka kuwavuwa wenzake gamba sasa anakaribia kuvuliwa yeye!!
 
hebu acha tabia ya kuropoka.hujui nini kinaendelea. hivi unafikiri nape anaweza kuzunguka nchi nzima na kuwalaani mafisadi bila baraka za mwenyekiti wake wa chama? au umeamua kuropoka tu kwa sababu umepewa mdomo wa kuongea. acha ushabiki wa kijinga. hujui unaongea nini wewe.hivi unafikiri kikwete yeye ni mjinga wa kukubali toka mwanzo ripoti ile ya richmond kusomwa hadharani wakati yeye alikuwa anajua fika kuwa lowasa amehusika kwenye mchezo mzima?jk angeweza kukataa ripoti ile isisomwe pale bungeni, lakini kwa sababu alijua lowasa ni mwizi ndio akaamua kumuumbua pale kwa staili ile ya kusomwa ripoti. na kwa taarifa yako lowasa atamalizwa keshokutwa kwenye kikao cha cc. acha kutetea ujinga ambao utakugharim hata wewe filipo.acha mawazo ya kitoto. haihitaji ufike udsm kutambua haya ninayokueleza filipo.lowasa, chenge na rostam wote ni wezi wakubwa.


Unawafahamu wajumbe wa kamati ya nidhamu ya CC ya CCM? Kama unawafahamu basi tafuta majina yao kisha ufanye tafakuri!!
 
Ni vigumu sana kufanya kazi katika mazingira yasiyofuata misingi. Chama kinaendeshwa kwa kufuata utashi na hisia za viongozi hasa mwenyekiti ndio matokeo yake. Kwa hili namlaumu Nyerere na kauli mbiu iliyorindima kila kona ya nchi ya "ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CCM".Hivi Nape na Chiligati wasingekua "mediocres" si wangeweza hata kujiuzulu pale pale mwenyekiti alipomjibu Sumaye kwamba watachukuliwa hatua kwa kumwita Lowasa Gamba? Du nimekubali "kumvua Kobe gamba inahitaji timing".
 
hebu acha tabia ya kuropoka.hujui nini kinaendelea. hivi unafikiri nape anaweza kuzunguka nchi nzima na kuwalaani mafisadi bila baraka za mwenyekiti wake wa chama? au umeamua kuropoka tu kwa sababu umepewa mdomo wa kuongea. acha ushabiki wa kijinga. hujui unaongea nini wewe.hivi unafikiri kikwete yeye ni mjinga wa kukubali toka mwanzo ripoti ile ya richmond kusomwa hadharani wakati yeye alikuwa anajua fika kuwa lowasa amehusika kwenye mchezo mzima?jk angeweza kukataa ripoti ile isisomwe pale bungeni, lakini kwa sababu alijua lowasa ni mwizi ndio akaamua kumuumbua pale kwa staili ile ya kusomwa ripoti. na kwa taarifa yako lowasa atamalizwa keshokutwa kwenye kikao cha cc. acha kutetea ujinga ambao utakugharim hata wewe filipo.acha mawazo ya kitoto. haihitaji ufike udsm kutambua haya ninayokueleza filipo.lowasa, chenge na rostam wote ni wezi wakubwa.



Mkuu,
Natambua ufisadi wa EL na pia simkubali kabisa. Natambua uwezo mdogo wa huyo M/kiti wa ccm. Nilichochangia hapa ni kujaribu kuonesha sympath niliyonayo kwa Nape maana kinachoonekana ni kwamba mambo yamemgeukia. Leo yeye ndiye anayetakiwa kuvuliwa gamba na kuwaacha wale aliokuwa anahubiri nchi nzima kwamba lazima waondoke. That was my concern!
 
Back
Top Bottom