Humphrey Polepole, tumekuletea Lowassa badala ya Lipumba na Slaa!

Humphrey Polepole, tumekuletea Lowassa badala ya Lipumba na Slaa!

magode

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2014
Posts
2,204
Reaction score
3,338
Wanabodi, Sina hakika kama Humphrey Polepole ni member hapa JF.

Siku chache zilizopita wakati UKAWA wakiwa kwenye mchakato wa kuteua mgombea wa urais, alinukuliwa akisema; UKAWA kama wanataka kushinda uchaguzi, watafute mgombea mwingine tofauti na Prof. Lipumba na Dr.Slaa. alidai hao hawana mvuto tena machoni pa wengi.

UKAWA ni kama walizingatia maoni yake, wameteua mtu mwenye mvuto zaidi kuliko hata mgombea wa CCM.

Ningependa kusikia maoni yake baada ya uteuzi wa Lowassa ana maoni gani! Kama hayupo humu jukwaani, aliye karibu nae atuitie tupate maoni ya kijana mwenzetu mwenye fikra mpya.

Nawasilisha..
 
Last edited by a moderator:
Hivi kwanini Professor Lipumba kaamua kujiuzulu nafasi yake?

Kuna kitu hapa!
 
ametimiza tu haki yake kikatiba sidhani km kuna impact kubwa kwa yeye kutoka UKAWA
What i know pipo have changed and wamechoshwa na ilani na mikakati ya kuja tekelezwa mwaka 2025!
 
Hivi kwanini Professor Lipumba kaamua kujiuzulu nafasi yake?

Kuna kitu hapa!

Kama sikosei CUF imepewa 28% ya majimbo ndani ya UKAWA, ni sababu hiyo ilosabisha Lipumba kujiuzulu kwa shinikizo la Maalim Seif.
 
Ukisikia wakati wa UKOMBOZI basi ndio sasa hatutapata wakati mwingine kama huu kwani viashilia vyote vinaonyesha kama ifuatavyo:-

1. Kua na Muungano Thabit wa Vyama vya Upinzani.
Tanzania haijawahi kupata Uzoefu huu wa angarau vyama vikuu vya upinzani kuungana kama ilivyotokea sasa kwa UKAWA, hii ni kiashilio kikubwa kua SAA YA UKOMBOZI IMEFIKA.

2.Chama Tawala (CCM) Kupoteza Umoja Wao
Tumeona Chama Tawala kimepoteza Umoja wao na Mshikamano wao ambao ndo ulikua silaha kubwa kushinda Upinzani kwa Asilimia kubwa.

3.Chama Tawala Kukimbiwa na Watu Mashuhuli (Lowassa n,k)
Ni kwa mara ya kwanza Tanzania tunashuhudia CCM ikikimbiwa na Watu Mashuhuli kama Lowassa ambae aliwahi kua hadi Waziri Mkuu na pia Watu mbalimbali ambao walikua Key members ndani ya CCM na pia CCM inategemewa kukimbiwa na wtu wengi zaidi kadri muda unavyokwenda.

4. Wasaliti Wa Upinzani Kukimbia Kishindo Cha Harakati ya Mabadiliko (Lipumba)
Ni kwa mara ya kwanza pia Tanzania kushuhudia Wasaliti wa Upinzani kuogopa Kishindo cha Mabadiriko ya Fikra na kukimbia kishindo hicho kama alivyofanya Lipumba kuondoka CUF lakini bado Chama kinasonga Mbele tena bila hata kuteteleka.

5. Kususia Harakati za Kweli (Dr silaa)
Popote kwenye Harakati za kweli huwa kuna watu muhimu Kususia mabadiliko ya kweli kama ilivyo kwa Dr Silaa. Hii sio nzuri lakini haina budi kutokea kwani ndio viashilio kua Hatupo mbali na UKOMBOZI. Tumemuelewa Dr Silaa na tunaomba arudi tumalizie Safari.

"KWELI UKOMBOZI UMEFIKA"
 
Ni kujidanganya kudhani kua kuondoka Kwa pro. Lipumba CUF na kuamua kua mwanachama wa Kawaida, na pia Dr. Slaa hakutakua na athari yoyote Kwa Ukawa, labda kama mtu alikua hajui nafasi ya Slaa ama Lipunga katika vyama vyao, ama ukawa Kwa ujumla. Kwa taarifa ni kwamba kuna watu wengi sana wako nyuma ya viongozi hawa, na labda mapenzi yao Kwa ukawa yalitokana na mapenzi ya mmoja Kati ya viongozi hao, kuondoka Kwao kunawaacha wanachama njia panda, wapo watakaodikiria na kuziamia sababu wazotoa zilizowafanya waondoke, na kuamua kumuunga mkono, wapo watakaoamua kubaki katika imani Ingawa nyoyo zao zitabaki na shaka , Lakini wapo watakaoamua kutopiga kura Kabisa Kwa kuona ulaghai unaofanywa na vyama vya siasa. Kumbuka wingi huanza na moja, hivyo athari ya kukosa kura moja ni kubwa sana, na mtu naweza kutangazwa kua mshindi Kwa tofauti ya kura moja tu.
 
Kama sikosei CUF imepewa 28% ya majimbo ndani ya UKAWA, ni sababu hiyo ilosabisha Lipumba kujiuzulu kwa shinikizo la Maalim Seif.

Hivi sasa wabunge waliopo katika vyama vinavyounda UKAWA, wale wa CUF wanaweza kua ni asilimia ngapi?. Je alitaka 50% maana kuna NCCR, NLD na CHADEMA nao lazima wawe na % yao. Kwa sababu hata tukichukua assumption tugawe sawa kwa vyama vyote 4, kila chama kinapata 25% (assumption).
 
Hivi mnachojadili hapa ndicho hicho nilichoandika au mmeamua tu kujadili kitu kingine nje ya bandiko langu!!??
 
Hivi mnachojadili hapa ndicho hicho nilichoandika au mmeamua tu kujadili kitu kingine nje ya bandiko langu!!??

Aliyebadili mwelekeo wa bandiko lako ni huyo aliyecomment baada tu ya bandiko lako. Soma comment yake.
 
Mmmmmm....wewe wa wapi????wameachia nyadhifa za uongozi sio uanachama...kura zao kwa UKAWA!
 
Aliyebadili mwelekeo wa bandiko lako ni huyo aliyecomment baada tu ya bandiko lako. Soma comment yake.
Kwa hiyo ukifungua uzi unaanza kusoma kwanza maoni ya wengine au unasoma kwanza lenyewe halafu ndo unatafakari cha kuchangia!!?
 
Back
Top Bottom