Ni kujidanganya kudhani kua kuondoka Kwa pro. Lipumba CUF na kuamua kua mwanachama wa Kawaida, na pia Dr. Slaa hakutakua na athari yoyote Kwa Ukawa, labda kama mtu alikua hajui nafasi ya Slaa ama Lipunga katika vyama vyao, ama ukawa Kwa ujumla. Kwa taarifa ni kwamba kuna watu wengi sana wako nyuma ya viongozi hawa, na labda mapenzi yao Kwa ukawa yalitokana na mapenzi ya mmoja Kati ya viongozi hao, kuondoka Kwao kunawaacha wanachama njia panda, wapo watakaodikiria na kuziamia sababu wazotoa zilizowafanya waondoke, na kuamua kumuunga mkono, wapo watakaoamua kubaki katika imani Ingawa nyoyo zao zitabaki na shaka , Lakini wapo watakaoamua kutopiga kura Kabisa Kwa kuona ulaghai unaofanywa na vyama vya siasa. Kumbuka wingi huanza na moja, hivyo athari ya kukosa kura moja ni kubwa sana, na mtu naweza kutangazwa kua mshindi Kwa tofauti ya kura moja tu.