Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Humphrey Polepole, ni lini na kwa lipi CCM imewahi kuyakumbuka maslahi na haki za akina mama hapa nchini?
Pamoja na hawa akina mama kuwa mtaji wa CCM kuendelea kuwepo madarakani tangu Uhuru, cha kushangaza, Serikali yenu ya CCM imewanyima maji safi na salama.
Aidha, Serikali yenu ya CCM imeshindwa kabisa kuwarahisishia hawa akina mama hali ngumu za maisha wanazokabiliana nazo huku mitaani na majumbani.
Leo unavyowapaka mafuta hapa kwa mgongo wa chupa, Sukari inakaribia kufika Shilingi 3,000/= kwa Kilo moja. Mafuta ya kula ndio usiseme maana ni aibu ya mwaka.
CCM na Dola yenu mnawezaje kusimamia haki za akina mama wa nchi hii ili hali mwanadada Aquiline Akwilina ambaye kesho angeitwa mama fulani, ameuawa bila hatia akiwa safarini na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya wahusika.
Hawa akina mama hawataki kwamba haki na maslahi yao iwe ni hisani ya CCM na Serikali yake.
Badala yake wanataka uwaambie ilipo Rasmu ya Jaji Waryoba maana wanaamini haki na maslahi yao chini ya Katiba Mpya iliyo bora, hakuna hisani ya CCM na Serikali yake.
Na hiki ndio kilio chao kikuu leo mpaka kesho.
Pamoja na hawa akina mama kuwa mtaji wa CCM kuendelea kuwepo madarakani tangu Uhuru, cha kushangaza, Serikali yenu ya CCM imewanyima maji safi na salama.
Aidha, Serikali yenu ya CCM imeshindwa kabisa kuwarahisishia hawa akina mama hali ngumu za maisha wanazokabiliana nazo huku mitaani na majumbani.
Leo unavyowapaka mafuta hapa kwa mgongo wa chupa, Sukari inakaribia kufika Shilingi 3,000/= kwa Kilo moja. Mafuta ya kula ndio usiseme maana ni aibu ya mwaka.
CCM na Dola yenu mnawezaje kusimamia haki za akina mama wa nchi hii ili hali mwanadada Aquiline Akwilina ambaye kesho angeitwa mama fulani, ameuawa bila hatia akiwa safarini na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya wahusika.
Hawa akina mama hawataki kwamba haki na maslahi yao iwe ni hisani ya CCM na Serikali yake.
Badala yake wanataka uwaambie ilipo Rasmu ya Jaji Waryoba maana wanaamini haki na maslahi yao chini ya Katiba Mpya iliyo bora, hakuna hisani ya CCM na Serikali yake.
Na hiki ndio kilio chao kikuu leo mpaka kesho.