Elections 2015 Humphrey Polepole: CCM ilifanya maamuzi ya kiume, Majizi na hasa kubwa lao yakakatwa...

KWAKO NDUGU Humphrey Polepole, ENDELEA KUTUMIKIA MAJIZI MILIONI MOJA HUKO ULIKO!


Mimi napenda mijadala kama wewe na sina shaka katika hilo, tuendelee kujadiliana. Kuna watu unawaita majizi na wezi, kwamba mkubwa wao amekatwa na akaelekea kwa UKAWA-FEKI hii ya sasa na si ile ya BMK. Well and good brother.
Unachosahau ni kuwa, CCM ni kiwanda cha kuzalisha MAJIZI NA WEZI na wakiendelea kukaa hukohuko wanakuwa ni balaa na shida kubwa sana. MAJIZI na WEZI wengine wamekaa hadi IKULU na wakati wanaingia walitangaza mali zao na walipotoka madarakani walipoulizwa wana mali kiasi gani walikuja juu na kutukana, wengine walianzisha makampuni wakiwa ikulu na wengine wamejilimbikizia kila aina ya UKWASI, hawa unawajua lakini kwa sababu wewe ni CCM kindakindaki unaamini katika chama chako kuliko misingi.


Watu wengi walidhani misimamo yako katika katiba ni thabiti lakini ukweli ni kuwa kwa wanasiasa na vyama katiba ni jambo rahisi tu kutofautiana nao kuliko suala la kuendelea kushikilia madaraka ya dola. Ndiyo maana kwenye suala la katiba hata Ofisi ya Waziri Mkuu ilisema inataka serikali tatu japokuwa ilijua CCM inaamini katika serikali mbili. Jaji Warioba ambaye juzi alikuwa anamnadi Magufuli pia alihitaji serikali 3 kwa maana ya kutetea msimamo wa tume yake, hakuogopa kuwa watamshangaa. Leo limekuja suala la madaraka, wewe na wenzako hamuamini kama wapinzani wanaweza kuongoza dola, unaamini ni CCM tu ndiyo yenye uwezo wa kuongoza. Huu ni woga mkubwa sana kwa mtu ambaye hapo kabla alionekana anawaamini wapinzani kwa sababu ya kusimamia jambo kubwa kama katiba.


Unasema ati MAJIZI yalikatwa! Majizi ni yapi hayo? Na jizi KUU ni lipi hilo? Na huko kwenye kiwanda cha kuzalisha majizi yamebaki mangapi? Juzi wakati makada wa CCM wanashirikiana kuiba fedha za umma Bilioni 230 za ESCROW hilo jizi kubwa lilishiriki namna gani? Pale wizara ya ujenzi kwa rais wako Magufuli wakati mabilioni ya fedha yanaonekana kuporwa kwa mujibu wa ripoti za CAG hilo jizi kubwa lilihusikaje? Tunachotofautiana na wewe ni namna gani unautizama WIZI na UFISADI. Mimi nautizama kama KANSA ndani ya CCM na wewe unautizama kama JAMBO la MTU mmoja. Kwani hujui aliyeko madarakani leo anatuhumiwa kwa mambo lukuki tu? Mbona huyasemei? Unajua ukwasi wake ni kiasi gani? Unajua anajenda maghorofa na mahoteli mangapi? Umekaa kimya kwa sababu ni Kiranja mkuu japo najua hutafuti ukuu wa wilaya. Mfumo wa uongozaji wan chi kutoka CCM ni UOZO MTUPU na hapo ndipo tunatofautiana.


Hebu fuatilia kuona namna gani wabunge wa CCM na madiwani wamepitishwa ndani ya chama chao. Ni RUSHWA kuanzia jimbo kwa jimbo, kata kwa kata. Hii CCM unayoamini ati inaweza kusafishika haiwezi asilani, ni bora kufanya kazi nyingine kuliko kukisafisha chama ambacho juzi mlikiletea katiba bora kabisa ya kushughulikiwa MAJIZI NA MEZI MAKUBWA ikaikataa? Iliikataa ili kumlinda nani? Na aliyeongoza ukataaji yule unamjua, ni bwana mkubwa. Yeye humgusi na unajua who he is!


Ndiyo, nakubali kabisa kuitambua taswira ya huyu unayemuita JIZI KUU alipokuwa huko ndani ya CCM. Ndiyo, hadi leo na hadi kesho naamini kuwa watu wale waliokuwa wanakusanyika kwake walikuwa wananunuliwa tu, NDIYO. Na simlaumu kwa sababu huo ndiyo mfumo ambao uko huko, kununua watu. Ni kama leo hii namna ambavyo CCM itakuwa imetenga mabilioni ili kununua wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo na kata ili ishinde uchaguzi na impeleke Magufuli Ikulu. Mfumo wa huko CCM ni kununua tu. Mabalozi wa nyumba kumikumi waligawa fedha toka enzi za chama kimoja wakati Mwinyi anaingia madarakani, 1985 wakati mkapa anakuja unafahamu kuwa CCM ilikuwa kwenye wakati mgumu na kwa macho yangu nilishuhudia milungula ikigawiwa ili CCM ishinde, 2005 pia hali hiyo iliendelea kama ilivyo, ni kugawa rushwa tu. Kwa hiyo hakuna mtu aliyekuwa CCM na hatoi rushwa, labda ni Nyerere na Sokoine tu. Waliobakia wengine wote wananuka rushwa, si Lowassa, si Magufuli, Si Mkapa na si kila unayemfahamu. Wote walipata madaraka kwa njia za Rushwa, kwa hiyo huyu unayemuita JIZI MKUU lazima angetenda vile atendavyo na tuliwaona wagombea urais wenzake wakitenda hivyo kwa sababu huo ndiyo mfumo wenu.


Lakini kuwa katika JUKWAA jipya lenye taratibu jipya kunabadilisha kila kitu. Kama juzi alinunua viongozi wa dini n.k. walionunulika, leo hawezi kufanya hivyo kwa sababu huku kuna nguvu ya wananchi, huhitaji kununua. Lakini kaa chini utafakari kuwa huyu JIZI moja aliyeongoka na kuja upande huu na kupewa USUKANI mbona amewaacha MAJIZI kibao tu huko CCM ukijumuisha na yule aliyepewa USUKANI huko CCM? Sasa watanzania watakuwa na kazi ya kuchagua JIZI wa UKAWA ambaye amehamia kwenye sehemu isiyooza na inayofuata misingi, au JIZI la CCM lililobaki katika chama kilichooza, kilichojaa rushwa, wizi, ufisadi, unyonyaji n.k.


Naam, fikisha salamu zangu kwa majizi MILIONI MOJA yaliyobakia CCM na endelea kuyatumikia kwa utashi wako!
Ni mimi ndugu yako katika mijadala, Julius Sunday Mtatiro.


POST HII INAJIBU HOJA ZA POLEPOLE ZILIZOKO KWENYE LINK HII https://www.facebook.com/hpolepole?fref=ts, MJADALA UENDELEE!

'' Kwa kipindi kirefu Lowassa amekuwa akionekana kama mgonjwa na si siri kuwa amekuwa akipata matibabu katika hospitali za kimataifa nje ya nchi.'' ....
Mh.Mtatiro

'' Unachosahau ni kuwa, CCM ni kiwanda cha kuzalisha MAJIZI NA WEZI na wakiendelea kukaa hukohuko wanakuwa ni balaa na shida kubwa sana.''

Mh. Mtatiro.. mbona mmechagua ''JIZI'' ambalo afya yake mgogoro...?
Hata hivyo..kama CCM ni kiwanda cha kuzalisha majizi basi bidhaa zake nazo hazifai ...na hazitakubaliwa popote Tanzania hii. LOWASSA ni moja ya bidhaa ya kiwanda hiki...Mtatiro..mmechagua bidhaa mbovu.
 
Lowassa ndio shetani mkuu wa ufisadi, wizi na rushwa. Ni mpanga mikakati mzuri wa ufisadi mkubwa mkubwa na mpiga dili asiye na aibu wala huruma kwa watanzania maskini. Ndugu mtanzania ukimnyima kura yako huyu jambazi, umekata mizizi ya ufisadi nchini.
tumkatae.
 
Lowasa ndio shetani mkuu wa ufisadi, wizi na rushwa. ni mpanga mikakati mzuri wa ufisadi mkubwa mkubwa na mpiga dili asiye na aibu wala huruma kwa watanzania maskini. ndugu mtanzania ukimnyima kura yako huyu jambazi, umekata mizizi ya ufisadi nchini.
tumkatae

mimi nakuambia kuwa "CCM ndio shetani mkuu wa ufisadi, wizi na rushwa". CCM ni mpanga mikakati mzuri wa ufisadi mkubwa mkubwa na mpiga dili asiye na aibu wala huruma kwa watanzania maskini. ndugu mtanzania ukimnyima kura yako huyu jambazi ( CCM ), umekata mizizi ya ufisadi nchini.
tumkatae@CCM kwa kwa sanduku la kura oct 25.
 
Last edited by a moderator:
Humphrey Polepole awali nilijua ni kijana mwenye ufahamu mkubwa, nilichogundua ni kijana mwenye usanii mkubwa wa kisiasa tena mnafiki asiyejua kujilinda na aibu inayoweza kumpata. Mada zake zote amekuwa akishambulia mtu na kuonyesha chuki zake za wazi kwa Lowasa. Polepole ni mtu anayeamini kuwa "umaskini ni kigezo cha uadilifu" hayo ni mawazo ya kipumbavu, Polepole anakumbuka fadhila za kuteuliwa kuwa mjumbe wa katiba ya wananchi kujaribu kumpendezesha aliyemteua ili pengine kama chama hicho kitaingia madarakani aambulie kitu. Kila mara amekuwa akidai kuwa mafisadi wamekatwa CCM lakini haelezi kama hao waliobaki ccm ni wasafi au la? Mimi nafikiri hata bila kujipendekeza kwa ufahamu alionao anaweza kuutumia kujipatia riziki, hii tabia ya kujaribu kuwa kinyonga ni unafiki mkubwa. Miezi kadhaa iliyopita tulimuona wakifuatana na mzee walioba kila kwenye kongamano kueleza uzuri wa serikali tatu na ubaya wa walioikaata rasimu yao leo hii yuko mstari wa mbele kulamba miguu ya ccm? Kweli umasikini ni utumwa na kudhalilika!!!!!!!
 
Humphrey Polepole awali nilijua ni kijana mwenye ufahamu mkubwa, nilichogundua ni kijana mwenye usanii mkubwa wa kisiasa tena mnafiki asiyejua kujilinda na aibu inayoweza kumpata. Mada zake zote amekuwa akishambulia mtu na kuonyesha chuki zake za wazi kwa Lowasa. Polepole ni mtu anayeamini kuwa "umaskini ni kigezo cha uadilifu" hayo ni mawazo ya kipumbavu, Polepole anakumbuka fadhila za kuteuliwa kuwa mjumbe wa katiba ya wananchi kujaribu kumpendendeza aliyemteua ili pengine kama chama hicho kitaingiia madarakari aambulie kitu. Kila mara amekuwa akidai kuwa mafisadi wamekwata CCM lakini haelezi kama hao waliobaki ccm ni wasafi au la? Mimi nafikiri hata bila kujipendekeza kwa ufahamu alionao anaweza kuutumia kujipatia riziki hii tabia ya kujaribu kuwa kinyonga ni unafiki mkubwa. Miezi kadhaa iliyopita tulimuona wakifuatana na mzee walioba kila kwenye kongamano kueleza uzuri wa serikali tatu na ubaya wa walioikaata rasimu yao leo hii wako mstari wa mbele kulamba miguu ya ccm? Kweli umasikini ni utumwa na kudhalilika!!!!!!!
 
Back
Top Bottom