Humphrey Polepole aibuka upya, aongea mambo yenye utata!!

Humphrey Polepole aibuka upya, aongea mambo yenye utata!!

Ndio manake....Gambaz walikuwa wanamtumia kufanikisha yao...na ujira wake alikuwa analipwa kz imekwisha Magufuli yuko Magogoni
Pole pole njoo huku ujibu tuhuma zako
 
Mnafiki Mkubwa, Hana Jipya Hata Mmoja, Juzi Tu Alikuwa Akisapoti Yanayoendelea Kule Zanzibar Na Usafi Wa Chama Chake (CCM) Leo Amegeuka Tena Anakosoa Na Kuyameza Matamshi Yake!! Kumbe Alikuwa Anahitaji CCM Ipate Ushindi Kwa Gharama Zozote!!
 
Mtoto hawezi kumzaa baba hivyo basi katiba ni kubwa kuliko bunge. Bunge lisingehusika kabisa katika kufanya mchakato wa katiba lazima kutakuwa nakutetea maslahi. Katiba ingekuwa na baraza lake lenyewe bila kufungana upande wowote.
 
Huyu anasema ukweli hataki Unafiki wa kina MBOWE
Sikuzote wamemuita mwizi ghafla anawaoa
 
Amemaindi kuona unafiki wa mwenzie mpanjuuu umempa unaibu katibu mkuu
 
Huyu jamaa sijawahi kumuelewa hata siku moja. Ni kigeugeu sana.
Watu wanashindwa kumwelewa Polepole kwa sababu hakuegemea upande wowote. Tatizo la watu wengi sasa hivi wametekwa na uchama sana hivyo hawawezi kusimamia ukweli. Watu mngemuelewa Polepole endapo mngekuwa na fikra huru ambazo hazijafungamana na upande wowote. Si viongozi wala Wananchi wote wamechagua kuwa upande fulani hata kufikia kugombea fito katika ujenzi wa nyumba moja Tanzania. Wanahabari nao ndiyo usiseme hata wameshindwa kubalance story!
Ingekuwa inawezekana Wananchi tusingekuwa na mitazamo ya kisiasa tungewahukumu vizuri sana wanasiasa na wangetuheshimu na kututumikia ipasavyo kwani wasingekuwa na mtazamo wa kuhesebu wana wanachama wangapi bali wamewafanyia nini wananchi.
 
Huyu jamaa nilishampuuza siku nyingi sana. Hata sijui kama nitampa tena nafasi ya kumuamini.

Ova
 
.....hivi bado kuna mtu mwenye akili timamu anamsikiliza polepole!!
 
Back
Top Bottom