The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,962
- 2,943
Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo ameibuka na kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoendelea nchini kuhusu katiba.
Polepole amesema Katiba Pendekezwa ina mapungufu kuizidi hata ya mwaka 77 tuliyonayo, sasa hivyo anapendekeza kuwa badala ya kuipigia kura ya maoni, ni vema pawepo maridhiano kwani bunge la katiba liliipoka katiba ya wananchi na kuifanya katiba ya viongozi.
Kuhusu mgogoro wa Zanzibar, anasema ufumbuzi wake ulikua kwenye Rasimu ya Warioba, lakini katiba pendekezwa imeukuza sana huo mgogoro kuhusu yeye kuwageuka Ukawa amesema si kweli kuwa yeye aliwageuka Ukawa, isipokuwa ukawa walisaliti misimamo yao kwa kumkaribisha na kumpa nafasi mtu ambae yeye binafsi na wajumbe wenzie walimpinga hata akiwa CCM, kwani anaamini kuwa Lowassa hakuwa na uadilifu wa kumuwezesha kuleta mabadiliko chanya.
Kuhusu CCM na ufisadi, amesema CCM ndio chama pekee hapa Tanzania kuwahi kukiri kuwa kuna ufisadi ndani ya chama na sasa kimedhamiria kuukomesha, vyama vingine havijafanya hivyo ingawa kwao pia kuna ufisadi.
Polepole amesema Katiba Pendekezwa ina mapungufu kuizidi hata ya mwaka 77 tuliyonayo, sasa hivyo anapendekeza kuwa badala ya kuipigia kura ya maoni, ni vema pawepo maridhiano kwani bunge la katiba liliipoka katiba ya wananchi na kuifanya katiba ya viongozi.
Kuhusu mgogoro wa Zanzibar, anasema ufumbuzi wake ulikua kwenye Rasimu ya Warioba, lakini katiba pendekezwa imeukuza sana huo mgogoro kuhusu yeye kuwageuka Ukawa amesema si kweli kuwa yeye aliwageuka Ukawa, isipokuwa ukawa walisaliti misimamo yao kwa kumkaribisha na kumpa nafasi mtu ambae yeye binafsi na wajumbe wenzie walimpinga hata akiwa CCM, kwani anaamini kuwa Lowassa hakuwa na uadilifu wa kumuwezesha kuleta mabadiliko chanya.
Kuhusu CCM na ufisadi, amesema CCM ndio chama pekee hapa Tanzania kuwahi kukiri kuwa kuna ufisadi ndani ya chama na sasa kimedhamiria kuukomesha, vyama vingine havijafanya hivyo ingawa kwao pia kuna ufisadi.