aliekua mjumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba leo ameibuka na kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoendelea nchini kuhusu katiba polepole amesema katiba pendekezwa inamapungufu kuizidi hata ya mwaka 77 tuliyonayo sasa hivyo anapendekeza kua badala ya kuipigia kura ya maoni ni vema pawepo maridhiano kwani bunge la katiba liliipoka katiba ya wananchi na kuifanya katiba ya viongozi kuhusu mgogoro wa zanzibar anasema ufumbuzi wake ulikua kwenye rasim ya warioba lakini katiba pendekezwa imeukuza sana huo mgogoro kuhusu yeye kwageuka ukawa amesema si kweli kua yeye aliwageuka ukawa isipokua ukawa walisaliti misimamo yao kwa kumkaribisha na kumpa nafasi mtu ambae yeye binafsi na wajumbe wenzie walimpinga hata akiwa ccm kwan anaamini kua lowasa hakua na uadilifu wa kumuwezesha kuleta mabadiliko chanya. kuhusu ccm na ufisadi amesema ccm ndio chama pekee hapa tanzania kuwahi kukiri kua kuna ufisadi ndani ya chama na sasa kimedhamiria kuukomesha vyama vingine havijafanya hivyo ingawa kwao pia kuna ufisadi