Humphrey Polepole afunguka, Maaskofu semeni tu

Humphrey Polepole afunguka, Maaskofu semeni tu

Polepole unajichanganya sana kwa ujumla hii nafasi haikufai kwani hii kauli sio ya kujenga zaidi ni ya kubomoa.

Unasema unawajua baadhi ya Maskofu ni wa vyama gani kama umeusoma waraka unajielezea yakuwa kila Askofu na Mkoa anaotoka kama umeliona hilo inakuje unamuusisha Askofu mmoja ktk kilichopitishwa na umoja wao.
Huoni kwamba ujumbe wako unawagawa Maskofu kama ulivyosema wao ni wakubwa wakiongea lolote laweza kutokea zuri au baya kuendana na ujumbe watakao utoa je hawa uliowagawa moyoni kwako unajua wanachokifikiria juu ya msimamo wa chama changu ccm kilichokutuma uje uongee ulichokiongea.
Hivi Rais au ww unavyoendaga ktk mikutano na kutoa msimamo wowote juu ya chama kuna mtu maandishi yoyote huwa unayatuma kwa hao uliowatolea msimamo na kama sio hivyo inakuwaje unaulizia ujumbe kutoka kwa Maskofu hapa umewakosea wao wametoa msimamo wao kama kanisa kuendana na yanayoendelea hapa nchini kwa hiyo ss ccm kufanyia kazi ujumbe wao sio kuwadai ujumbe yaani inaonyesha ujumbe wao hujausikia na kama ujausikia ulikuwa na haja gani ya kuuongele kwani ungekaa kimya na huku unafanyiwakazi ni mbaya.

Inafika mahali unawaagiza yaani kama wanajambo lolote waje kwako au kwa wakubwa zatu hii ni dhihaka ndugu hawa ni viongozi wetu wa kiimani tunawaheshimu kuliko viongozi wa kisiasa hata nyie viongozi hili mnalijua vizuri bila unafiki.
Kwani Polepole hoja Maskofu na Mange inatofauti gani na kama zinafanana unawatuhumu vipi Maskofu flani ni wa chama flani je hao Maskofu wanaotuunga mkono sisi ccm Waraka wao unasema je kama hawana waraka basi naomba huu Waraka ni wa Maskofu wote wa Tanzania.

Ee Mungu naomba uipushe nchi yangu na mabaya
 
Maaskofu Hawa walishikwa kichwa na mbowe ziro watalipeleka taifa kubaya na matamko ambayo hata hawakubaliani
maaskofu na mbowe walikuwepo hata kabla magufuli hajawa rais,ma rais wote waliopita hawakuwahi kutoa wakala kwa nini kwa jpm
 
kama unafiki ni dhambi basi wa kwanza kuchimwa atakuwa polepole,hamna mnafiki Tanzania namba 1 kama huyu jamaa aliyekuwa anasimama majukwaani akitetea katiba mpya kuwa kama itapita basi CCM Ikabidhi madaraka kwa hiari leo hii ndio walewale
 
NNimeamini bongo kuna vilaza wengi sana maana watu wengi wameshindwa kugundua hizi kelele na haya maazimio yanatokana na nini?? Bongo lala mnaona kawaida tu Hii ni vita ya kiuchumi nyumbuu nyie angalieni huko mbele. Hivi mnafikiri watu wa nchi jirani na hao watu wa makinikia na madawa ya kulevya wanaitakia hii nchi mema?? Ila kwa vile wabongo wengi vilaza wanafuata mkumbo tu hawajui hata hawa wanaowachochea wanataka nini. Za kuambiwa changanya na za kwako.
Bongolala nawe ukiwamo siyo! Hayo madawa yanaingizwa na kuuzwa na nani kama sio hao viongozi wenu wa ccm! Hayo madini na makinikia aliyagawa nani kama siyo mawaziri wenu wa ccm! Hivyo vita vya kiuchumi kasababisha nani kama sio ccm? Hamna namna bora ya kujisafisha zaidi ya kujimwagia petrol na kujiwasha moto ndipo uchafu wenu utatoka!
Ona, hao mabongolala wa sasa ni wajanja na wanaulewa mpana kuliko hao maccm wenzako waliogawa rasilimali na maliasili za nchi hii kama vihamba vya urithi kule kwenu!
Jipelekeni wenyewe kwenye mahakama ya mafisadi mliyofungua mkaponee kwa majaji!
 
NNimeamini bongo kuna vilaza wengi sana maana watu wengi wameshindwa kugundua hizi kelele na haya maazimio yanatokana na nini?? Bongo lala mnaona kawaida tu Hii ni vita ya kiuchumi nyumbuu nyie angalieni huko mbele. Hivi mnafikiri watu wa nchi jirani na hao watu wa makinikia na madawa ya kulevya wanaitakia hii nchi mema?? Ila kwa vile wabongo wengi vilaza wanafuata mkumbo tu hawajui hata hawa wanaowachochea wanataka nini. Za kuambiwa changanya na za kwako.
unajifanya unajua kumbe hujui chochot ,vita ya kiuchumi unaijua ww?? hivi kwa akili yako unawezaje kuwa na vita ya uchumi na mtu ambaye unategmea technolojia kutoka kwake au? na sio ya kuchimba dhahabu tu bali technologia ya uzalishaji ya bidhaa zote zinazotumika nchini
 
Maaskofu hawakurupuki; kuna tatizo kubwa nchini kwetu.
 
Askofu akiisifia serikali na kuiombea anakuwa mzalendo, huyo huyo Askofu akiikosoa serikali anakuwa mpinzani.
 
Sifieni kama kuna mambo ya kusifia na onyeni kama kuna mambo ya kuonya lakini hekima busara kwa sababu kauli hiyo ni kauli ya moto inaweza ikatujenga inaweza ikatubomoa.Kuna namna nyingi za kurekebisha, tusije tukageuza na kujadiliana na Maaskofu, Askofu anasema tunamjibu, tutakuwa tunamkosea Mungu.

Mimi sitaki kusema Maaskofu wamekosea au hawajakosea lakini nataka kusema haya majadiliano ukiyaangalia yanatokea wapi? Tusije tukaingia kwenye mtego wa Ibilisi tukajikuta tukimtizama askofu fulani tunaona chama fulani. Askofu unaonekana kama chama fulani, mfano mimi ni mwanaccm nina dhambi zangu nataka kuja kuungama kwako, ntaungamaje kwako wakati wewe una itikadi tofauti na mimi?

Chama chetu kinaamini binadamu wote ni sawa, kinaamini katika utu, kinaamini katika kujitegemea, kinaamini katika heshima ya watu, kinaamini katika kusema kweli, kinaamini katika vita dhidi ya rushwa, kinaamini katika umoja kinaamini katika kujitoa, kinaamini katika kazi ni kipimo cha utu.

Sasa nikikutizama wewe unaamini katika ubwanyenye, unamini katika kuhodhi mali, unaamini katika umangimeza, unaamini katika mimi ni mwenyekiti peke yangu na hakuna mwingine. Sasa utaanza kunipoteza.
Ccm ipi inaamini katika usawa?

Ccm ipi inaamini ktk heshima ya watu?

Ccm ipi inaamini ktk umoja?

Ccm ipi inaamini watu wote sawa?

Pole pole naona analeta utani kwenye issue zisizohitaji utani
 
Wanaopaswa kutumia hekima na busara kuonya ni Maaskofu tu sio ila nyie watawala hampaswi kuwa na hekima na busara ?

Hivi Pengo huwa unamtazama kwa jicho la chama kipi

Hii takataka ndio ilikuwa inataka katiba mpya leo anatumika kama toilet paper anakuja kuwakashifu Maaskofu kwamba ni wanasiasa kisa wamesema ukweli ?

Bado kitambo kidogo tu ,kizazi hiki sio hicho cha kwenu na kina Sizonje kuna siku watasema basi na hakika siku hiyo lazima nile nyama ya tako ya mtu
 
Greenlight ya kuelekea 2020
Kitaeleweka upande mmoja umechokozwa sana ukakaa kimya sana washasema its over
Always madikiteta wanapata mwanya watu wakikaa kimya
 
Maaskofu Hawa walishikwa kichwa na mbowe ziro watalipeleka taifa kubaya na matamko ambayo hata hawakubaliani

Unadhani bado kuna watu wajinga wa kuwapotoshea ukweli. Hao maaskofu wanaulewa wa kutosha wala hawahitaji kuambiwa na Mbowe. Mmeeona maaskofu wamesema kweli, hivyo mnataka kuhusishana na cdm ili mpoteze mantiki. Ni hivi, Magu amevuma miaka miwili iliyopita kwa kupaizwa na propaganda. Kwa sasa ni mwaka wa tatu, ukweli wa uwezo na udhaifu wake uko wazi, hivyo hao maaskofu wametazama wameona kuna maendeleo ya kawaida, ila zinatumika mbinu za kibabe kulazimisha kutawala bila busara. Ule wizi wa kura ulipokuwa unafanyika hao maaskofu hawakuwa wamefumba macho. Hilo bunge liligeuka mateka na kutii kila kitu toka kwa jamaa usidhani hao maaskofu hawajui tofauti mpaka wamsubiri Mbowe awaambie ukweli. Hivi kwa akili yenu maaskofu wanauwezo mdogo wa kuelewa mambo, mpaka Mbowe awaeleweshe.
 
Kama
Sifieni kama kuna mambo ya kusifia na onyeni kama kuna mambo ya kuonya lakini hekima busara kwa sababu kauli hiyo ni kauli ya moto inaweza ikatujenga inaweza ikatubomoa.Kuna namna nyingi za kurekebisha, tusije tukageuza na kujadiliana na Maaskofu, Askofu anasema tunamjibu, tutakuwa tunamkosea Mungu.

Mimi sitaki kusema Maaskofu wamekosea au hawajakosea lakini nataka kusema haya majadiliano ukiyaangalia yanatokea wapi? Tusije tukaingia kwenye mtego wa Ibilisi tukajikuta tukimtizama askofu fulani tunaona chama fulani. Askofu unaonekana kama chama fulani, mfano mimi ni mwanaccm nina dhambi zangu nataka kuja kuungama kwako, ntaungamaje kwako wakati wewe una itikadi tofauti na mimi?

Chama chetu kinaamini binadamu wote ni sawa, kinaamini katika utu, kinaamini katika kujitegemea, kinaamini katika heshima ya watu, kinaamini katika kusema kweli, kinaamini katika vita dhidi ya rushwa, kinaamini katika umoja kinaamini katika kujitoa, kinaamini katika kazi ni kipimo cha utu.

Sasa nikikutizama wewe unaamini katika ubwanyenye, unamini katika kuhodhi mali, unaamini katika umangimeza, unaamini katika mimi ni mwenyekiti peke yangu na hakuna mwingine. Sasa utaanza kunipoteza.
Kama chama chenu kinaamini katika usawa kwann mmefukuza kazi wenye vyeti feki ila bashite na ww mwenyewe baado mnakula kodi zetu na mi zero yenu
 
Tamko la maaskofu 35+27 haya ni majibu tosha kwamba serikali ya awamu ya tano imekosa ridhaa ya kisiasa kuongoza nchi.
 
Sisi tunachokataa ni unafiki.uWatu wanateswa wanauawa halafu kiongozi akiingia kanisani anakaa mbele anaonyesha ana hofu ya Mungu.Watu wanabomolewa nyumba zao bila fidia wengine Mwanza wanaambiwa wasibomolewe maana ndio waliompa kura.
 
Confusion, confused -stressed. Unafiki mtupu. Kukemea mauaji, watu kupotea...ndo uchama fulani? Wadanganyeni wajinga...
 
MUNGU AKUBARIKI polepole wewe huwa ni mtu makini.

Maaskofu ni Baba zetu hata kama wanatumika sisi ni watoto wao; ni vizuri Mkuu kuwajibu kwa hekima kama ulivyojibu.

Kwa hekima yako hii utakuja kufika mbali,wewe ni kiongozi
 
Sifieni kama kuna mambo ya kusifia na onyeni kama kuna mambo ya kuonya lakini hekima busara kwa sababu kauli hiyo ni kauli ya moto inaweza ikatujenga inaweza ikatubomoa.Kuna namna nyingi za kurekebisha, tusije tukageuza na kujadiliana na Maaskofu, Askofu anasema tunamjibu, tutakuwa tunamkosea Mungu.

Mimi sitaki kusema Maaskofu wamekosea au hawajakosea lakini nataka kusema haya majadiliano ukiyaangalia yanatokea wapi? Tusije tukaingia kwenye mtego wa Ibilisi tukajikuta tukimtizama askofu fulani tunaona chama fulani. Askofu unaonekana kama chama fulani, mfano mimi ni mwanaccm nina dhambi zangu nataka kuja kuungama kwako, ntaungamaje kwako wakati wewe una itikadi tofauti na mimi?

Chama chetu kinaamini binadamu wote ni sawa, kinaamini katika utu, kinaamini katika kujitegemea, kinaamini katika heshima ya watu, kinaamini katika kusema kweli, kinaamini katika vita dhidi ya rushwa, kinaamini katika umoja kinaamini katika kujitoa, kinaamini katika kazi ni kipimo cha utu.

Sasa nikikutizama wewe unaamini katika ubwanyenye, unamini katika kuhodhi mali, unaamini katika umangimeza, unaamini katika mimi ni mwenyekiti peke yangu na hakuna mwingine. Sasa utaanza kunipoteza.

Duu sasa na wa upande ule nao si watasema askofu fulani ni wa chama fulani au? Wanasiasa msitufikishe huko. Maaskofu wamesema tuwajibu kwa hoja ya kuwa waliyoyasema si kweli na kama ni kweli je tutayarekebisha vipi. Tujenge taifa moja tusiamze kugawanyika na kugawana maaskofu kivyama hatubaki salama
 
Back
Top Bottom