Human microchips analysis

Endelea kujipa moyo wapo hatua za mwisho mzee hata haitafika 2020 hawa mbwa hawajaanza leo hii project yao n ya kitambo sana ! ukiona kitu tayari kilicho kuwa cha siri kimemfikia mwafrika ujue kishafika hatua za mwishi hii ni kutuaandaa kisaikolojia tu ili ikija tuone ni kitu cha kawaida sana!! Ngoja rais ajae wa Marekani ndiyo atakaye kuja kumalizia hii kazi! huwezi kuwakwepa
 
Wabongo kwenye ubora wao.. hehehe upuuzi tu hakuna kitu hapo.
Sio kila kinachoandikwa kwenye internet ni kweli. Ila watanzania wengi walivyo wapumbavu kichwani hawawezi kulielewa hili. Mshana ukifungua shule utapiga hela sana kwa kua kama kiongozi wa wajinga.

Hizi conspiracy za microchips tumezisoma online toka 1999 enzi hizo wengi wenu hata hamjajua internet ni nini. Leo hii miaka 17 baadaye tumesoma technology tukaelimika, tunajua huu ni upuuzi, bado na mtasubiri sana huku mnakufa njaa, endeleeni kujipa moyo.
 
Hata katika zama za Nuhu walikuwepo watu kama wewe, wakati Nuhu akiwaambia swala la garika walimuona mpumbavu ila tukio lilivyoanza wakahangaika mpaka umauti ukawafika...endelea wala usiwe na Shaka kuwa tomaso mkuu Yesu atakuletea mikono yake uhakikishe kwa macho yako mawili
 
Hukupaswa kumjibu chochote, ungempuuza kama nilivyofanya mimi
 

Hehehe usiingize mambo ya dini kwenye huu upuuzi, nyie ndio mlioshika dini vibaya leo hii mnafulia kwa kumaliza pesa zenu kwa mapastor wanaotumia kulala na wanawake. Hata mimi ni Mkristo vilevile ila siwezi kukaa nasikiliza ujinga wa huyu jamaa nikauchukulia kichwani hata siku moja. Wewe unajua engineering kweli? specifically electronics, kama hujui hutokaa ujue hata siku moja kutengeneza chip kama hiyo inahitaji nini.

Short story, haipo na haijawahi kuwepo, hii story ilikuwepo miaka zaidi ya 20 sasa, hiyo microchip hakuna aliyeiona hata moja, watu wanatunga story wanazipublish hewani wajinga ka wewe mmejaa mnapenda sana kuzisoma, mnafungua mnasoma watu wanapiga hela. Mmeshika dini vibaya sana, kila mnachoambiwa mnaamini, hehe dont be stupid
 
Mleta mada upo sahihi lkn ninachokwamba ni kwamba kuna watu wengine as we speak right now wapo bize wanatengeneza miundombinu ya kubomoa hizo microchips kama ilivyo ulimwengu unatawaliwa na watu wabaya na watu wema pia wapo kwa ajili ya ku control damage.
 
Yeah kwenye kila jambo kuna mbadala wake na kinyume chake...kama ilivyo hasi na chanya
 
Inawezekana zimeaanza kazi ila hatujui. Ebu jiulize una uwezo wa kutofungua simu yako kwa masaa 2 hata kama hujapigiwa? Ulishawahi kuona dala dala ambayo hakuna simu isiyochat? Inawezekana wametumia mtindo tofauti na tunaoujua, kupinga tu si suluhisho, fanya uchunguzi wa kina
 
Piga kwa hoja na si kuanza kutukana watu humu mkiambiwa ukweli anaanza kuangaza mimacho! hujalazimishwa kuamini wala hujaitwa humu kwahyo yafaa ukatuacha na upumbavu wetu humu!!
 
Piga kwa hoja na si kuanza kutukana watu humu mkiambiwa ukweli anaanza kuangaza mimacho! hujalazimishwa kuamini wala hujaitwa humu kwahyo yafaa ukatuacha na upumbavu wetu humu!!

username yako inaongea yote ambayo ningesema
 

Mkuu ulichokiandika pamoja na hoja za mshana hii makitu ndani ya miaka kadhaa tutaanza kuitumia hasa watakapo ibua ishu ya kudhibiti ugaidi, maana tunavyopenda kwenda nchi za magharibi na kutumia kila kitu chao hasa kwenye ishu ya tekinolojia kweli wametushika pabaya
 
Duuh!! Aisee basi nitakimbilia huko kwenye mapango na kuozea huko maana uraini bila chip hupati kitu
 
Nawaza tu hapa .

Kama sasa duniani mwendo wa microchip tu basi second coming ya mwenye viumbe itakuwa ndo hapohapo.

Aisee hatari sana
 
There are three roads to ruin; women, gambling and technicians. The most pleasant is with women, the quickest is with gambling but the surest is with technicians. "Gorges Pompidou"
 
Tatizo letu waTanzania wengi ni wabishi na wavivu wa kusoma na kufuatilia mambo. Makala za Micrchip ziliandikwa sana na gazeti la Mtanzania mwaka 2007. Pia wiki hio tarehe 17 radio DW kiswahili waliandika kwamba kilifanyiwa maonyesho mjini Hannover. Dunia inaenda kwa kasi mno na hakuna namna ambavyo hii kitu inaweza kukuwepeka katika kizazi hiki. Tafadhali kabla hujaamua kubisha kitu,jaribu kukifuatilia kwanza upate facts juu yake. Asante Mshana kwa kukumbushia.
 
Hawa ndio huwakuta kutwa kucha wanasoma magazeti ya udaku na ukimkuta mtandaoni basi ni insta fb badoo na ngono
 
Mimi najua mkombozi wetu atakuwa North Korea,ngoja nianze kujiandaa kukimbia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…