Hukumu Kesi ya Mgomo wa Walimu: Mgomo ni batili

Ndio maana nakubaliana na Tundu Lisu! Tusipobadilisha namna ya uteuzi wa majaji hatuwezi kuleta mageuzi ya aina yoyote katika utoaji wa haki nchini. Haiwezekani mteule wa Rais, mara nyingi kama zawadi, atahukumu dhidi ya Rais! Wanatuambia mahakama iko huru na Jaji anamua kwa uhuru. Lakini haitoshi tu kusema hivyo, ni lazima ionekane kuwa Jaji yuko huru kuamua. Kwetu hapa Jaji aliyekuwa "handpicked" na Rais, kwa kufuata vigezo visivyo wazi, haonekani kuwa huru kuamua kesi ambayo Rais ameiongelea jana. Ndio maana hiyo ruling yake ina reasons zile zile alizotoa Kingkwete jana - notice ya 48 hours ili-include Saturday na Sunday. Sijui, kati ya Jaji na Rais, nani amekopi kwa mwenzake.
 
Hapo penye red, Hii ni kichekesho, kama suala liko CMA, yeye alikuwa anafanya nini sasa leo? Kama yeye hawezi kuingilia na kutoa uamuzi ulioko huko CMA, si angegoma kusikiliza kesi angewarudishia?
Je, mbona ameamua kubatilisha mgomo, badala ya kurejesha kesi hiyo CMA? I am confused.

Kweli hapa kuna mgongano kisheria. Haya maamuzi ya mahakama hayana athari zozote kwa shauri lililopo CMA?
 
Kwani wanafunzi walikuwa walalamikaji katika shauri hili? Anatoaje order ya watu wasiokuwa sehemu ya shauri walipwe fidia? Ama kweli tuna majaji miaka hii!

Si alisema Tundu Lissu? wanachaguliwa na JK bila vetting, bila kumbukumbu za kesi/hukumu zao walizotoa huko nyuma kuchunguzwa etc etc, kwa ujumla huwateua kishikaji tu.
 
mahakama ina-tobw-a,jaji una-tobw-a kama hau-firw-i.mnauz na kucheza na maisha ya watu
 
HurEee mgomo kwishhneyyy mmeumbukajeee na M4C yenu nyooo!!
unavurugwa wewe, nikiambiwa mbwa kubwa wewe, Mambo ya msingi wewe unaleta utani ipo siku tutauana tuu we ngoja watu kama wewe nitakuwa napiga panga tu. Haki iatapatikana
 
Naililia nchi yangu, unaweza kubatilisha mgomo moto, lakini kamwe mgomo baridi haubatilishwi. Watanzania tulio na watoto wetu katika shule za kata na za kayumba, tujililie nafsi zetu na vizazi vyetu, na tusishangae hadithi ikiendelea kuwa ile ile; 'wanafunzi elfu 5 waliofaulu kuingia kidato cha kwanza hawajui kusoma na kuandika', shule inayoongoza kwa kufaulu ni xyz boys au abc girls, wanakosoma watoto wa majaji'
Maskini serikali yetu (yenye sifa aliyoisema Mnyika) haijui au haijali kwamba walimu walikwishagoma kwa miaka mingi sasa.
 
wanaoshangilia hukumu iliyotolewa, shangilieni hata hili;

Wanafunzi 5,000 waliofaulu hawajui kusoma, kuandika
Monday, 09 April 2012 20:42


Fredy Azzah
IMEBAINIKA kwamba wanafunzi 5,200 waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu, hawajui kusoma wala kuandika.

Kutokana na sababu hiyo, habari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinasema kwamba wanafunzi hao wataachishwa masomo na Serikali inaangalia uwezekano wa kuchukua hatua za kisheria wanafunzi hao na wakuu wa shule wanazotoka ili kukomesha tatizo hilo.

Wanafunzi hao wanatoka katika mikoa yote ya Tanzania bara, isipokuwa Kigoma ambao taarifa zake hazijafika katika wizara hiyo.

Wanafunzi hao wamebanika kutojua kusoma wala kuandika baada ya kupewa majaribio ya kupima uwezo wao wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) baada ya kuripoti shuleni kama ilivyoagizwa na Serikali.

Desemba 14, mwaka jana wakati akitangaza matokeo ya Mitihani ya Darasa la Saba, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo aliagiza wanafunzi wote watakaoingia kidato cha kwanza mwaka huu wapimwe kwanza uwezo wao wa Kusoma na Kuandika.

Agizo hilo lilitokana na udanganyifu uliojitokeza kwenye mtihani huo na kusababisha watoto 9,736 kufutiwa matokeo.

Wanafunzi waliofanya mtihani huo walikuwa 983,545 na waliofaulu ni 567,567. Kati yao wasichana walikuwa 278,377 sawa na asilimia 54.48 na wavulana walikuwa 289,190 sawa na asilimia 62.49.

Akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) mwishoni mwa wiki, Mulugo alisema tathmini inaonyesha kuwa Mkoa wa Kilimanjaro umeongoza kwa kuwa na wanafunzi wengi wasiojua kusoma na kuandika.

"Mkoa wa Kilimanjaro una wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika wapatao 660, Tanga 490 na Dar es Salaam 208," alisema Mulugo bila kutaja matokeo ya mikoa mengine.

"Hili ndilo janga la kitaifa sasa. Siyo hayo mengine ambayo watu wanasema ni majanga ya kitaifa. Lazima tujiulize kwa nini watoto wanamaliza darasa la saba wakiwa hawajui kusoma wala kuandika na halafu wanafaulu?" alihoji kuongeza:

"Je, siku hizi hakuna tena somo la kusoma na kuandika? Kwa nini mtoto amalize shule bila kuwa na maarifa ya KKK? Mitaala (mitalaa) mnayoandika kwa nini hamsaidii mtoto katika hili? Nataka leo nijue tatizo liko wapi, mengine (matatizo) ya Serikali; walimu, vitabu, miundombinu na majibu yake sisi tunayo."

"Jambo la kusikitisha kuna mpaka baadhi ya wanafunzi wa kidato cha tatu, ambao hawajui kusoma wala kuandika. Tulipofikia siyo pazuri hata kidogo, lazima tuwe makini jamani. Tuheshimu Baraza la Mitihani (Necta) tupate ufumbuzi wa mambo haya taifa hili ni letu sote, lazima tuhakikishe linasimama imara."

Alisema Serikali kwa upande wake, imejipanga kufanya utafiti na kujua chanzo cha tatizo na kuwa imepata Sh150bilioni kutoka Global Partnership for Education (GPE), kwa ajili hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa TET, Habib Fentu alisema mitalaa waliyoandika imesisitiza mwalimu kufanya tathmini ya kile alichofundisha kila baada ya mada husika kumalizikia.

"Kwa hiyo hapa sasa suala la uwajibikaji linakuja, inakuwaje mtoto amalize darasa la saba akiwa hajui kusoma, kuandika wala kuhesabu na mwalimu wa darasa yupo, mwalimu wa taaluma, mwalimu mkuu na kamati ya shule vipo?"

Katika matokeo ya darasa la saba yaliyotangazwa mwaka jana, Mkoa wa Manyara uliongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliofutiwa matokeo ukifuatiwa na Arusha.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

[h=4]Comments [/h]


0 #5 2012-04-10 20:42 HILI NI JANGA LA KITAIFA TUSUBIRI ILE KAULI YA KUWA NA VIHIYO WENGI KAMA TUNAINGIZA SIASA KWENYE ELIMU IMENISIKITIHSA SANA BAADHI YA WABUNGE TOKA ZANZIBAR WANATETEA WANAFUNZI WALIOFU[NENO BAYA] MITIHANI NA"NECTA" SINA UHAKIKA WATOTO WAO WANASOMA SHULE HIZO TUWE NA UCHUNGU NA NCHI YETU WAALIMU WOTE WALIORUHUSU WANAFUNZI WASIOJUA KUSOMA NA KUSOMA NA KUANDIKA WAHUKUMIWE KAMA MAFISADI WA ELIMU HADHI YA TANZANIA KIELIMU ITASHUKA RASILIMALI WATU YA TANZANIA ISITEGEMEE KUPATA SOKO POPOTE DUNIANI NASHANGAA WANAOTETEA U[NENO BAYA] HUU
Quote










0 #4 2012-04-10 20:15 Matokea ya RUSHWA HAYA.
Hawa wanafunzi bomu baada ya miaka kadhaa watakuwa Madaktari, makakimu,nk

MADHARA YA RUSHWA UKiMWI CHA MTOTO!

Quote










0 #3 2012-04-10 17:07 Nchi hii ni ya ajabu sana. hayo matatizo hayajanza leo. Mimi nakumbuka miaka ya 80 nilimaliza darasa la 7 kikijini kwetu na watu wengi tu ambao hawajui kusoma nikafaulu kata nzima nilifaulu peke yangu. Viongozi wetu hataki kuchukua hatua za dhati kutatua matatizo ya nchi hi. wanaenda ulaya kila siku lakini hawaigi lolote la maana watuletea matapeli kama richmondi iptl downs. Lakini wanao teseka zaidi ni watoto wa masikini. maana leo hii watu wote wenye kauwezo wakiwepo hao mawaziri wansomesha watoto wao kwenye (academy).Hivi ni kwani tunaua taifa letu wenyewe? Vingozi kazi kujisifia. eti kila mto aende secondari! Walimu wenyewe mbumbu. madwati hakuna. Labda malaika waje watukomboe bila hivyo tumekwisha.
Quote










0 #2 2012-04-10 09:01 Ndugu wahusika, inashangaza kuuliza maswali huku majibu mnayo, walimu wa sasa hawana wito, kazi ya ualimu inaitwa "voda fasta" kwani ndilo kimbilio la wote waliofeli mitihani ya kidato cha nne na sita, vyuo vya ualimu navyo vimepoteza mwelekeo na kupokea kutokana na shinikizo walimu bomu, wakaguzi wa elimu nao leo hawako na kama wako ni ofisini tu siyo kwenye "field".
Kazi ya ualimu imekuwa kwa watoto wa masikini, lakini watoto wa masikini lakini watoto wa vizito na matajiri ni kule BOT, NBC NMB na kwingineko kwenye mapato mazuri. Walimu huko vijijini hakuna anaye wajili kwa hiyo nao hawana moyo wa kuhangaikia watoto kuzijua hizo KKK Zenu, wao cha msingi kwao ni kufanya biashara katika shule ili kuendeleza na kuongeza kipato tu.SWALI: KWANINI FANI YA UALIMU WARUHUSIWE WALIOPATA DIVISION (IV? JE HIYO NDIYO SERA YA ELIMU? NA DIVISION(III) KWA KIDATO CHA SITA? JE HAO WALIOFELI WATAFUNDISHA NINI IKWA WAO WENYEWE WALISHINDWA? IWEJE MWALIMU DARASA LA SABA AFUNDISHE DARASA LA SABA TENA? JE WALIMU WANGAPI WANAKWENDA KWENY MASOMO YA JUU KUJIENDELEZA?HUO UTAFITI WENU ISIISHIE KWENYE MAKABRASHA TU BALI TUONE MATOKEO, kwani kuna kila dalili na za wazi kuwa kuwa kunatabaka la watoto linaandaliwa ili kulitawala tabaka lingine jambo ambalo hatutakubali kamwe.
Kwani watoto wenu mnawapeleka nje kusoma na wetu kwenye shule zisizo hata na mabenchi.

Quote










0 #1 2012-04-10 02:54 Yaani hapa nashindwa nisemeje ili nieleweke vyema! Ina maana hao wangejua kusoma na kuandika huko sekondari ingekuwa sawa kama masomo hawayawezi? Kama tunazungumzia kutokujua kusoma na kuandika kwa ngazi ya sekondari, ina maana kwa ngazi yadarasa kla pili, tatu, nne mpaka darasa la saba tuzungumzie nini? Ninavyojua tulitakiwa tushangae mwanafunzi asiyeweza kusoma na kuandika akiwa darasa la pili, inakuwaje tujadili hawa wa sekondari? Hili ni janga kubwa! Hapa haitakiwi kutaka wizara iwajibike kwani nayo naona bado ni kidogo mno. Mfumo mzima wa serikali na baraza zima la mawaziri linahusika, hata aliyeteuliwa leo ingepaswa aonyeshe ni nini haswa mustakabali wa nchi yetu kuhusu sekta ya elimu,sina maana waziri wa elimu tu, bali baraza la mawaziri lote akiwemo mwenyekiti wao!
 
Kama haitafika siku tukawa na sauti ya umoja na kusema pamoja, basi tusitegemee kutoka hapa tulipo..Taifa hili linapiga hatua moja mbele na kumi nyuma kila mwaka, sasa baada ya miaka 5 tutakuwa wapi? We must say NO and join together to fight against the corrupt system in power,the system that acts for minority and not majority. Members of parliament, ministers don't have to go to courts to have their salaries and benefits increased, they just press the buttons to achieve it. If leaders are for this country, why don't they act for the interest of the people? A true leader sacrifices for his people. It hurts alot!!
 
Kwa mtindo huu tutaendelea kuona, kusikia na kupata akina KAYUMBA kila siku kwani hakuna Mwalimu atakayefundisha kwa moyo, hii inaonyesha jinsi serikali isivyoweza kutatua matatizo ya wananchi kwa ujumla wake wakiwemo (wakulima, Wafanyakazi, wanafunzi kwa ngazi zote ikiwemo hata watoto)
 
Jk alishatoa hukumu jana pamoja na mahakama kukosa uhuru wa kufanya maamuzi. Inasikitisha na ni aibu kwa Taifa letu kuwa na majaji wanaowatetea waliowateua na kuwahukumu wanyonge na umma wa watanzania wasio na namna lakini wanamtegemea mwenyezi Mungu tu. Ipo siku kwa kilio cha hawa watu, watawala na vizazi vyao vitaathiriwa na laana za hawa watu na hawatakuwa na pa kuomba msamaha. Mungu si Athumani.
 
Hii ni sawa na enzi za Karume. Sifa ya mtu kuwa hakimu ni kutojua kusoma na kuandika kabisa
 
Walimu tuendelee na mugomo wetu wa siku nyingi wa mugomo baridi.Maisha ya walimu ni magumu huwezi amini na kazi yenyewe ngumu watoto wengi sana.Hao viongozi hasa raisi hawezi kuongeza pesa hakuna mtoto wake anae somea kwenye shule zxetu za walalahoi.Wzazi/walezi hamishieni watoto wenu kwenye shule binafsi.
 
Huu ni ushenzi wa hali ya juu. Kazi ya udaktari na ualimu si ya kuhamisha matofali ili baadae uhesabu ni matofali mangapi mtu kahamisha. Akili ya mwalimu na ya daktari anayo yeye peke yake na ni uamuzi wake kuona aitoe kiasi gani kumhudumia mgonjwa au kumfundisha mwanafunzi. Kitendo cha mahakama kwa waalimu na madaktari ni sawa na kutangaza mgomo usioisha milele! Watanzania tujiandae kuwa mambumbumbu kwa kufundishwa na mwalimu aliyegoma moyoni, na tuendelee kufa kwa kutibiwa na daktari aliyegoma! Mungu ibariki Tanzania, alaaniwe ****** na kichaka chake kinacoitwa MAHAKAMA.
 
Uamuzi wa Mahakama, uliingiliwa na ushawishi wa Mkuu wa Kaya. Mkuu wa Kaya, huku akijua ni kosa la jinai kuiongelea kesi iliyoko mahakamani nje ya mahakama, katika hotuba yake ya siku moja kabla ya mahakama, alitoa ufafanuzi, ambao moja kwa moja ulikuwa na ushawishi, ambao alijua unaweza kuathiri uhuru wa mahakama. Hivyo, hukumu ya leo haishangazi na tulitegemea iwe hivyo.

WAZO LANGU:- Kama nchi inaendeshwa kiujanja ujanja namna hiyo, Mkuu wa kaya anapotosha vyombo vya haki maksudi, Nchi inaelekea wapi???????????????
 
polen walimu hao ndo viongozi wenu wajanja wajanja na serikali iliyoshindwa kuwasaidia wananchi wake kwa kupenda kukimbilia mahakaman kulinda udhalimu wao poleni sana
 
Walimu wameishaanza kulipa wanafunzi na taifa la Tanzania pindi walipokata tamaa miaka kadhaa nyuma!!!!!!!!
Km hujui jiulize inakuwaje kuna wanafunzi 5,0000 sekondari wasiojua kusoma na kuandika/ wasiona sifa za kuwa hata kidado cha kwanza!!!!!!!!!
Miaka miwili kuanzia ss namba itakuwa 15,0000!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! TAIFA LA wasomi LINAANDALIWA!!!!!!!!
 
Tanzania hatuna mahakama tuna mahakaCCM hatuna Polisi tuna PoliCCM hatuna Takukuru tuna TakuCCM hatuna NEC tuna NECCM listi ni ndefu!!
 
Back
Top Bottom