Acheni woga usio na sababu jamani; uzito wa kesi ulikuwa kwa walioshtaki. Vitu viwili vikubwa vilikuwa wazi... waliodaiwa kudhalilishwa hawakushtaki, na siku na mahali inapodaiwa kufanyika udhalilishaji huo hapakukubaliana na hata kilichosemwa hakijakubaliana. Ni kesi ya juu juu sana. Majaji wetu wako huru sana kama watamkuta Lema na hatia yoyote ni kutokana na uzito tu wa ushahidi; wala msiwape CCM credit yoyote ile. Binafsi sina wasiwasi hata chembe kuwa ubunge wa Lema utathibitishwa leo. Na nina uhakika wa 99.99 kuwa itakuwa hivyo. Tusiwaogope sana CCM na serikali kiasi cha kuona kuwa wanaweza kufanya lolote, kwa yeyote na wakati wowote vinginevyo itabidi tuanze kupeleka sadaka pale Lumumba!