Ni matumaini yangu kuwa haki itatendeka
Kosa litakalofanywa ni kumhujumu Lema, hapo ndiyo ccm itaendelea kuporomoka kuelekea waliko akina KANU.
Nasikia hakimu hajapata usingizi usiku mzima: Source mke wake.
Wakuu nipo mahakama kuu ya Arusha Hali ni shwari na baraka tele za mvua spika zimewekwa kuwezesha wale waliofika mahakamani kufuatilia kwa umakini Jaji amemaliza kusoma submission za pande zote sasa ni determination of contentious issues! Nawasilisha kutoka mahakama kuu Arusha.
lema atashinda maana kesi haikuwa na miguu wala mikono lakini kwa kuwa jaji ameelekezwa awafute machozi ccm ataamua kinyume na ukweli ngoja tusubiri tuonekaza buti
Kwa hakika kabisa. Iwapo ushindi wa Lema utatenguliwa itakuwa ni mbaya sana kwa ccm kuliko kwa Chadema. ukifanyika uchaguzi mdogo Arusha mjini CCM itashindwa tena, tena kwa kishindo kikubwa zaidi ya ile mara ya kwanza na hii itakuwa na impact kubwa sana kwa nchi nzima kwa uchaguzi mkuu wa 2015.
Sheria ni msumeno, msitegemee kubebwa kama Lema alitenda makosa; hatakwenda wiki ijayo mjengoni DOM
ATTENTION!
Wenye taarifa na update watupie hapa,la sivyo kwa kuendekeza porojo tutakuwa tunapoteza seriousness ya huu uzi!
Ni mtazamo wangu tu!!
Acheni woga usio na sababu jamani; uzito wa kesi ulikuwa kwa walioshtaki. Vitu viwili vikubwa vilikuwa wazi... waliodaiwa kudhalilishwa hawakushtaki, na siku na mahali inapodaiwa kufanyika udhalilishaji huo hapakukubaliana na hata kilichosemwa hakijakubaliana. Ni kesi ya juu juu sana. Majaji wetu wako huru sana kama watamkuta Lema na hatia yoyote ni kutokana na uzito tu wa ushahidi; wala msiwape CCM credit yoyote ile. Binafsi sina wasiwasi hata chembe kuwa ubunge wa Lema utathibitishwa leo. Na nina uhakika wa 99.99 kuwa itakuwa hivyo. Tusiwaogope sana CCM na serikali kiasi cha kuona kuwa wanaweza kufanya lolote, kwa yeyote na wakati wowote vinginevyo itabidi tuanze kupeleka sadaka pale Lumumba!