MAHAKAMA ya Rufani nchini, kesho inatarajia kutoa hukumu ya rufaa iliyokatwa na aliyekuwa
Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Godbles Lema, kupinga hukumu ya
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha iliyotengua ubunge wake.
Hukumu hiyo inayovuta hisia za wengi nchini, inatarajiwa kuhudhuriwa na wafuasi wengi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama chaDemokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Mamia ya wafuasi wa Lema kutoka mjini Arusha, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa mkoa huo, Aman Gulugwa, wanatarajia kuongoza msafara wa magari kwenda jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusikiliza rufaa hiyo ya kihistoria.
Habari za kuaminika toka ndani ya Mahakama ya Rufani jijini Dar es Salaam, zilisema kuwa
tayari jopo la majaji watatu; Nataria Kimaro, Salum Massati na Bernad Ruhanda, limeshamaliza kazi na kwamba uongozi wa mahakama umepanga hukumu hiyo isomwe
kesho. Tarehe ya hukumu ya rufaa iliyofunguliwa na Lema ni kesho, hivyo mfike bila kukosa,
kilisema chanzo chetu cha habari.