Huko ngorongoro kampuni ya uwindaji ya ortello ya UAE, je haihusiki?

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,418
7,206
Huko Ngorongoro kuna wawekezaji wa kitalu cha uwindaji wa miaka mingi wanaitwa Ortello. Hii kampuni inahusisha vigogo wa kifalme wa falme za kiarabu. Inasemekana kigogo fulani wa ccm na serikalini wana maslahi na wamekua wanaibeba kampuni hiyo. Kila mwaka kunakuaga na kutangazisha vitalu ila kitalu cha ortello hapo loliondo ni sawa na mali yao tu.

Huko nyuma imedaiwa ortello wakiendesha uwindaji wanyama bila kufuata taratibu na hata kusafirisha nje ya nchi wanyama hai kupitia kiwanja walichojenga Loliondo.

Migogoro na wenyeji eneo hilo la uwindaji huko nyuma ilidaiwa kusababishwa na kampuni hiyo ya waarabu wa uae. Lengo likiwa kutaka kupatiwa maeneo zaidi kwa kuondolewa wenyeji.

Leo hivi waziri mkuu ameelezea bunge kuhusu mgogoro unaoonekana kuanza Ngorongoro na kusema kwa wepesi tu wachochezi watashughulukiwa.

Hadi speaker ilibidi kumsisitizia waziri mkuu kuhusu umuhimu wa wachochezi kujulikana na kuchukuliwa hatua.
Wasiwasi mkubwa tulionao baadhi yetu ni hawa wawekezaji wa arabuni toka UAE.

Huenda ndio wachochezi kwa hivyo uchunguzi uanzie kwao. Hawa ortello wako kwa miaka mingi wananchi wa kawaida hawajui wana faida kwa nchi au kwa vigogo binafsi nchini.
 
Wachochezi ni wamasai wenyewe ambao wako busy kuikumbatia CCM🐒🐒🐒
 
Hiki ni kisegere nyuma, tuone nguvu za serikali dhidi ya wananchi wake wenyewe. Huu ni uwanasesere. Je mchezeshaji ni nani wananchi au wawekezaji?
 
Huu mradi wa kongorokongoro anaeusimamia ni yule kipara aliepewa uenyekiti wa kijiji makao makuu yake ni kitongoji cha bara.

**** video zipo tiktok jamaa aliwapokea hao matajiri na kuwa ahidi zoezi litakamilika.
Mradi wa gas na huo wa uwindaji ni miradi ambayo pesa ndefu ilikuja bila kuchujwa kiasi waliweka mfukoni na wao wakawekwa mfukoni na nyingine ilienda kufanya kazi za nchi na ni pesa ambayo kuirudisha ni kimbembe bora watu wafe.

waarabu hawana dogo wakitaka kitu hawana ugumu kumwaga pesa si mnaona huko man city ,psg na newcastle wakiamua huwa wanaweka hela wale hata kama kitu hakina thamani ya hivyo kikibwa wakikipenda, wao lengo lao ni furaha ,washindane na watimize wanayofikilia.

waarabu hawana sheria kali tatizo ukila hela zao kurudisha ni kazi " sasa huyo mwenyekiti kisha kula hela na zingine zimezama kwenye nchi bila wananchi kupewa utaratibu " kifo cha bwana mkubwa kilisubiliwa sana na baada ya kutimiza jambo lao lazima litimie la huko kongoro.

kuna watu wataondoka sana na hioo soo ya kongoro kongoro " hyo mama yenu na huyo wa ntwara hawana cha kusema waoga kufa"

kwa kifupi muamuzi ni Mungu aamue kumchukua kipara na rfik yake kpnz ndio watu watafunua bakuli zao.

"Inshot falsafa inayotumika tz kuibiwa na maadui zetu au matajiri kunyonya na kuchukua mali zetu wanapitia watoto wa vigogo na viongozi baazi wenye tamaa za kuishi kama wafalme .

ili wanachi washindwe jinsi ya kuwashitaki,kuwasema na kuwawajibisha.

hata viongozi wakubwa wanawaogopa watoto wa vigogo kuwasema,kuwawajibisha kwa sababu watoto wanababa zao ambao ndio waliibeba nchi lakini kwa sasa ndio wanatumika kuumiza wananchi.

Mfano ushatolewa alikua titifotati wamemlaza haya nani mwingine asimame ? ndo hvyo wanapeana miezi mitatu hlf majibu yatakayo kuja ni kuna wananchi hawataki kulipwa fidia na baazi ni wachochezi ,c tupo hapa tutaona kma kuna mwanaume au mwanamke ataeweza watetea wana kongoro wakati mfano wa aliekua mwamba amelazwa nani mwingine asogee.

bac tu Mungu ajalie nipate ht nyazfa ya kupayuka tuwasaidie....sema tu ndo hivyo huwez fika huko mpk utetee watu mifumo imebana.
 
CCM ina sera safi ila kuna watu wachache ambao wanakiharibu mbele ya jamii.

Kwa mitazamo yao wanaona wapo sahihi ila wanakididimiza kabisa.
CCM ilikufa siku nyingi hii iliyopo ni saccos ya waarabu
 
Back
Top Bottom