Hujuma zaanza 'Train ya Mwakyembe'

Hujuma zaanza 'Train ya Mwakyembe'

chibidula

Member
Joined
Jan 3, 2011
Posts
63
Reaction score
39
Janana leo nilibahatika kupanda train ya TRC kutoka Tabata Matumbi hadi Posta ambayo ilinichua dakika 30 kufika Posta.

Ninawapongeza watanzania kwa kujitokeza kwawingi kupanda train na pia Mh. Mwakyembe kwa kusimamia kuanzishwa kwa trainhii. Lakini nimenisikitishwa ni hujama za wazi zinafanywa na watendaji pamojana wazabuni waliopewa kazi ya kukusanya nauli ndani train.

Train hii imekuwa ikiendeshwa bila kuwa na ratiba maalumu kitu ambacho kimekuwa kikikatisha tamaa abiria ambao wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu mathalani jana nilipanda train Tabata matumbi saa 2.15 asubuhi kuelekea post lakini leonilipofika saa 8.00 kituo niliambiwa kuwa train imechelewa kuanza safari asubuhi kwa sasa wapo safari ya kwanza bado posta eti kisingizio ni kuwa jana walichelewa kumaliza hadi saa 4.00 usku kwani hiyo driver amechelewa kuamka, jejambo hilo ni sahihi? Kwani hakuna driver mwingine ambaye angewahi kuamka nakuanza kuendesha train kulingana na muda?

Pia nimeshangazwa na wakatisha tiketi wa Selcom wireless ambao wako ndani train lakini hawafuati wateja kudai walipe zaidi ya hapo kwenye behewa nilolipanda waliakatisha ticketi sio zaidi ya 30 wakati ndani tulikuwa zaidi ya abiria 200 kwenye behewa moja na train yote ilijaa.

Sikweza kuvumilia nilipofika mwisho nilimuuliza kiongozi wa TRC kwanini watu hawadaiwi ticket/nauli wakajitetea kuwa wao wanashangaa. Niionavyo mimi hii ni hujuma ili ionekane kuwa gharama za uendeshaji ni nkubwa kuliko mapato na hivyo kupelekea kusimamishwa hudumu hii muhimu sana kwa wananchi wa Dar es Salaam.

Ninamshauri Mh. Mwakyembe na TRC ya yafuatayo:

  1. Kuweka ratiba makini ya train kwa kila kituo ili abiria ajue muda gani atapanda train katika kituo gani na kuelekea wapi
  2. Kuteua kampuni nyingine au watendaji wengine watakao husika na ukatishaji ticket ili kampuni iweze kupata mapato stahili yatakayopelekea kuboresha train hii na
  3. Kuongeza idadi ya Train au mabehewa kwa kila train kwani tumekuwa tukibanana sana kiasi inaweza kuatarisha afya za watumiaji.

Nafikiri kama mambo haya yatatekelezwa basi usafiri huu utakuwa mkombozi kwa watu wengi sana.
 
Inasikitisha sana.

Kwa mtindo huu Tanzania kuendelea ni vigumu mno, mawaziri wenyewe wanaoneana wivu, mafisadi wanaachwa watambe... yani utafikiri tumelogwa
 
Katika Hali yoyote Haya unayoyasema Niliyategemea!! Ila cha Muhimu ni Kuwa na Uwajibikaji siku Zote!! Fikiria kuweka ratiba Kwenye Kila kituo sio Kitu Kigeni katika Jamii yoyote iliyostarabika!! Huwezi Kwenda Kupanda Train bila kujua ratiba yake!

Sasa Hawa wafanyakazi wa TRC mbona wanaonekana kama wanahujumu Kazi yao wenyewe?? Ni bora Mheshimiwa Mwakiembe akapendekeza responsible person incharge of complains!

And make a quick solution, Tupo karne ya 21, Haya madogo kwa nini yatushinde??
 
Inasikitisha sana.kwa mtindo huu Tanzania kuendelea ni vigumu mno.mawaziri wenyewe wanaoneana wivu,mafisadi wanaachwa watambe..yani utafikiri tumelogwa

Nyerere is a prophet; Aliyaona haya na kutuonya ila sisi hatukusikiliza!!
 
Tungeweza hata 'kuazima' utaratibu wa wenzetu wa kutumia kadi. Zifungwe system zitakazo-charge kadi ya mtu pale anapotumia usafiri huo, na siyo kumtegemea bwana konda. Na mtu ata-load kadi yake na pesa kama anavyofanya kwenye simu, kuwa aweke kutokana na uwezo wake na siyo kung'ang'aniza kuwa kuna kadi ya elfu tano na elfu kumi tu!

Anyways, safari hatua.
 
Nyerere aliondoka na uzalendo na hao aliowaacha wakayatupa yale yote aliyowafundisha ili wayasimamie.
 
Kwani Ma-dereva wa gari-moshi wanatakiwa kufanya kazi kwa masaa mangapi ?
Je hilo gari-moshi lina dereva mmoja tu......
Kama huyo Dereva alifanya kazi zaidi ya masaa yanayotakiwa ,basi ni hatari kwa usalama wa abiria.
 
Naomba wanipe kazi ya kukusanya nauli mimi ili niwafundishe kazi hao manyang'au wanaotaka kumwangusha Mwakyembe katika kubadilisha usafiri Dar.watakua wametumwa na Lowasa hao mbwa
 
Ndo tatizo letu kubwa. Wizi kila sehemu. hawa watoza nauli siku si nyingi wataanza kuiba. Mimi nashauri serikali iajili wataalamu kama 3 kutoka makampuni yanayojulikana duniani kuendesha biashara ya train kusudi wasimamie mapato walau kwa miaka 2 mpaka hapo Watanzania watapoelewa maana na umuhimu wa kukusanya mapato katika kuendesha biashara na huduma hii ya train.
 
Mkuu niko tayari kusaidiana na wewe kwani naujua umuhimu wa Train sana. Inanichukua saa moja kusafiri umbali wa kilomita 85 kila simu kwenda kazini. Bila train nisingeweza.
 
Kumbe ninyi wageni na hii inji,mradi wowote ule kama hauna maslahi binafsi hauwezi kuendelea,huo ni mwanzo tu iko siku mtakuta mataruma hayapo!Balaaa
 
Huu ndio upumbavu atutakiwi kuulea hata mwakyembe anaubeba kwanza unaanza na dreva huyo aliechelewa unamsimaisha mwezi mmoja ama miwili bila mshahara ajifunze then unaendelea na mengine

nilishangaa ati kumuona mwakyembe analalama kuna hujuma bandari wakati wahujumu anawajua wewe mtu anatakiw akutia saini gari zitoke anaondoka kablaya muda alafu unalalama kwenye tv si wote mnaonekana vichaa fukuza kazi wapo vijana wengi waadilifu wa vyuoni wanatafuta kazi

hawana adabu hao wahujumu uchumi kabisa
 
Hawa wezi wa nauli, hawana haya kabisa.!

Walaniwe na vizazi vyao pia
 
Tungeweza hata 'kuazima' utaratibu wa wenzetu wa kutumia kadi. Zifungwe system zitakazo-charge kadi ya mtu pale anapotumia usafiri huo, na siyo kumtegemea bwana konda. Na mtu ata-load kadi yake na pesa kama anavyofanya kwenye simu, kuwa aweke kutokana na uwezo wake na siyo kung'ang'aniza kuwa kuna kadi ya elfu tano na elfu kumi tu!

Anyways, safari hatua.

Kaka nakuunga mkono card payment system ndio best solution kama dubai wanazo metro hamna konda ni ww na kadi yako tuu shirika lao la usafiro RTA wanapate hela zao kama kawaida cuz hakuna mtu wa kati hapo
 
Mkuu ninadhani hatua ya haraka ya kuchukua ni kwa Dr. Mwakyembe kutengeneza kamati ya kufuatilia na kucimamia usafiri huu maana ninahici tayari michakachuo imeshaanza na watu wazima wanapanga jinci ya kuhujumu mapato.. Haya mambo ya Selcom wireless tickets ni kuhalalisha wizi 2.. Kama waliweza kutuletea mgao feki watashindwa nini kuhujumu usafiri huu wa reli hapa Dar..!
 

Ninamshauri Mh. Mwakyembe na TRC ya yafuatayo:
[/SIZE][/FONT]
  1. Kuweka ratiba makini ya train kwa kila kituo ili abiria ajue muda gani atapanda train katika kituo gani na kuelekea wapi
  2. Kuteua kampuni nyingine au watendaji wengine watakao husika na ukatishaji ticket ili kampuni iweze kupata mapato stahili yatakayopelekea kuboresha train hii na
  3. Kuongeza idadi ya Train au mabehewa kwa kila train kwani tumekuwa tukibanana sana kiasi inaweza kuatarisha afya za watumiaji.

Nafikiri kama mambo haya yatatekelezwa basi usafiri huu utakuwa mkombozi kwa watu wengi sana.
[/QUOTE]

1.Haiwezekan No Hurry in Tz 2.Wacalculate na Wawape kadirio la kati kulingana na idadi ya mabehewa. Mfn kila cku wawakilishe 10 milion tzshs. 3.Linawezekana.
 
Nimeamini TZ watu wa ngenga....ila waguse kwenye mapenzi....hawachoki hata kama hawajala
 
Behewa moja likila nyomi asubuhi au jioni 200*400=80000
80000*6=480000
Hapo kwa route moja hili Train akipewa Mangi mbona linalipa sana umakini tu unatakiwa litalaza pesa ndefu kwa siku.
 
Back
Top Bottom