Sinai
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 288
- 47
Jamani, kuna rafiki yangu wa karibu sana kaniambia kuwa yeye anaurafiki na dada mmoja hivi (urafiki wa kawaida tu) kwa muda mrefu sasa! Hajawahi kumtongoza hata siku moja, lakini juzi kati hapa, jamaa akapata mchumba na anataka kwenda kutoa posa. Lakini alipomwambia huyu binti ambaye ni rafiki yake wa kawaida juu ya swala hilo, huyo rafiki alikasirika sana, akamjibu hovyo kuwa kwanini anamwambia mambo yao? Ili aumie moyo au? Akawa anafyonya hovyo na kuondoka zake. Tangu siku hiyo hata akimpigia simu hapokei, hata sms hajibu! Sasa jamaa anashangaa, tatizo/kosa lake ni lipi? Anaomba msaada wana jamiii!!!!!!!!!!!!!