msovero
JF-Expert Member
- Jun 30, 2019
- 839
- 1,472
Baada ya waziri wa habari kudai wanasubiri ripoti ya uchunguzi wa uvamizi wa kituo cha runinga cha clouds dhidi ya aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa dar es salaam bw. Paul Makonda imenikumbusha ushauri aliowahi kupewa RC huyo wa zamani na msanii wa kizazi kipya 'Rashid Makwilo' a.k.a 'Chid Benz'.
Katika moja ya mahojiano yake 'interview' msanii 'chid benz' alimshauri Paul Makonda wakati akiwa bado ni RC wa jiji la Dar kuwa ni vyema akajikita kufanya mambo ya msingi yaliyomweka kwenye kiti na kuachana na mambo madogo madogo yasiyo na tija ambayo yanaweza kumharibia na hata kumuingiza kwenye jinai.
Katika mahojiano hayo msanii 'chid benz' alimshauri Makonda kushughulika zaidi na mambo ya kiserikali ikiwemo kutatua kero za wananchi kama vile kuboresha huduma za afya mahospitalini, kupanga machinga, kuboresha vituo vya dala dala, kuboresha mazingira ya wafanyabiashara wafanye kazi kwa uhuru n.k.
Msanii 'Rashid Makwilo' a.k.a 'Chid Benz' hakuishia hapo bali alienda mbali zaidi na kumshauri makonda kuboresha mazingira ya magereza zilizopo katika mkoa wake huku akitolea mfano gereza la Segerea kwamba hata yeye kwa matendo anayofanya ipo siku ambayo haijulikani na yeye anaweza kuwa mfungwa mtarajiwa na kufungwa kwenye magereza hayo hayo yenye mazingira mabovu.
Lakini kwa hulka aliyokuwa nayo kijana makonda alipuuza ushauri huo na kuendelea kufanya mambo yake aliyokuwa anaona ni sahihi kwake ikiwemo kusakizia watu kesi za madawa ya kulevya na mambo mengine mengine.
Kwa kuzingatia ushauri huo wa msanii 'Chid Benz' je, ni karma imeanza kumwandama makonda? Je huenda kweli sakata la uvamizi wa Clouds likaibuliwa na makonda akafungwa kwenye magereza alizomtabiria msanii chid benz?
Muda utasema!
Zaidi, msikilize hapa rapper 'chid benz' akimchana live makonda
Katika moja ya mahojiano yake 'interview' msanii 'chid benz' alimshauri Paul Makonda wakati akiwa bado ni RC wa jiji la Dar kuwa ni vyema akajikita kufanya mambo ya msingi yaliyomweka kwenye kiti na kuachana na mambo madogo madogo yasiyo na tija ambayo yanaweza kumharibia na hata kumuingiza kwenye jinai.
Katika mahojiano hayo msanii 'chid benz' alimshauri Makonda kushughulika zaidi na mambo ya kiserikali ikiwemo kutatua kero za wananchi kama vile kuboresha huduma za afya mahospitalini, kupanga machinga, kuboresha vituo vya dala dala, kuboresha mazingira ya wafanyabiashara wafanye kazi kwa uhuru n.k.
Msanii 'Rashid Makwilo' a.k.a 'Chid Benz' hakuishia hapo bali alienda mbali zaidi na kumshauri makonda kuboresha mazingira ya magereza zilizopo katika mkoa wake huku akitolea mfano gereza la Segerea kwamba hata yeye kwa matendo anayofanya ipo siku ambayo haijulikani na yeye anaweza kuwa mfungwa mtarajiwa na kufungwa kwenye magereza hayo hayo yenye mazingira mabovu.
Lakini kwa hulka aliyokuwa nayo kijana makonda alipuuza ushauri huo na kuendelea kufanya mambo yake aliyokuwa anaona ni sahihi kwake ikiwemo kusakizia watu kesi za madawa ya kulevya na mambo mengine mengine.
Kwa kuzingatia ushauri huo wa msanii 'Chid Benz' je, ni karma imeanza kumwandama makonda? Je huenda kweli sakata la uvamizi wa Clouds likaibuliwa na makonda akafungwa kwenye magereza alizomtabiria msanii chid benz?
Muda utasema!
Zaidi, msikilize hapa rapper 'chid benz' akimchana live makonda