minji
JF-Expert Member
- Sep 2, 2016
- 2,751
- 4,933
11th of Nzi Chuma..
Nitaandika hii mpaka nifike mwisho..
Mwaka wa tatu wa chuo kwangu ulikuwa na ubusy kidogo, so sikuwa na time sana na mapenzi kiviile, muda mwingi nilikuwa chuo, nikirudi usiku sanaa geto nimechoka, naweka simu silent nalala. Nai alikuwa mwanamke mwelewa sana, hakusumbua, shida niliipata hapa kwa single mama, akiwa yupo pale usiku anapiga simu mpaka unajuta yaani..mpaka sometimes nikawa nazima simu..yeye muda wote anataka mapenzi tu!! Mwezi mmoja kabla ya UE huyu single mother nae akapata mimba yangu. Alifurahi sana, alinambia kumbe alihangaika muda mrefu sana kupata mimba nyingine, lakini mimi nimemuwezea. Kwangu sikuona shida, nilijua kwa sababu anafanya kazi na ametafuta mtoto kwa muda mrefu, atazaa tu na atalea.. Lakini haikuwa hivyo. Nilivyoondoka tu pale Moro baada ya kumaliza UE, wiki mbili tu nyuma akaniambia imeharibika, nikajua atakua ameshaitoa.
Niliendelea kuwasiliana na Nai na pia niliendelea kuhudumia mtoto kwa Sophy!. Sikukaa sana kitaa nikapata kazi katika mradi flani ambao walikuwa wanatulipa vizuri, hapo nikaamua kujitegemea rasmi na kuanza mipango ya kuanzisha family.. Moyoni mwangu aliishi Nai tu. Niliamini nitamuoa tu one day.. Baada ya kufanya kazi kwa miezi sita hapa jijini nikawa niko vizuri sana. Nikarudi home na kuwaeleza mikakati yangu juu ya kuanzisha familia, nikawaeleza kuhusu Nai na yote yaliyotokea. Vidume vikajitokeza kunisaidia, nikavipa map vikafika kuonana na wazazi wake Nai..naam mtu mzima dawa, hawakutoka patupu..nikapata mrejesho wa kulipa mahari, nikalipa na kumuoa Nai, mtu niliyempenda zaidi maishani mwangu..!!. Lakini Nai hakuwa na raha na ndoa yetu, alikuwa anajua kuwa hawezi kupata mtoto. Lakini mimi nilimpa moyo kwa kumwambia kuwa ni bora nimekuwa mimi ambaye ndio msababishaji wa yote haya ndiye niliyekuoa kuliko angekua mtu mwengine, angekunyanyasa sana.. Nilijitahidi kufanya kila niwezalo Nai awe na furaha katika ndoa, lakini sidhani kama nilifanikiwa kwa 100%.
Muda flani akaanza kunilazimisha nioe mwanamke mwengine ili nipate mtoto (hapa tulishakaa miaka miwili katika ndoa). Alihisi sina amani. Lakini mimi nilikomaa nae, kila daktari mtaalam wa Gynecology niliyemsikia nilionana nae, dawa nyingi zikitumika lakini bado hatukufanikiwa. Mwisho nikamweleza ukweli Nai kuhusu Sophy, akaniambia niwasiliane na Sophy ili Abdul aje hapa atufariji.. Nikawasiliana na Sophy, nikamueleza mpango wangu, hapo ndipo Sophy aliponibadilikia na kunieleza kuwa yule mtoto hakuwa wangu kabisa, ni kuwa tu baba yake hajiwezi kiuchumi ndo maana akanibambikia, na ndo maana kipindi cha ujauzito hakunishirikisha..lakini baada ya mtoto kuzaliwa wakahisi atakosa huduma muhimu ndo maana wakanibambikia. Hapo hamu ikaniishia, sikutaka kuujua undani sana wa huyo mtoto nikaamua kupotezea.. Nikaconcentrate na Nai wangu..
Miaka ilipofika mitatu bila mtoto, nikalifanyia kazi wazo la Nai, nikaenda zangu kuchukua shombeshombe Pemba (how i met her, it's another story). Huyu ni kama alipata mimba siku ya harusi hivii...hahhahaa manaake alizaa miezi tisa kamili. Lakini Mungu sio Mzee Mkumba, baada ya kuoa, Nai alishika mimba mwezi mmoja tu mbele.. So alipishana na yule mke wangu wa pili mwezi mmoja tu kujifungua. Baada ya mwaka mmoja Nai akashika mimba nyingine na kuniletea toto la kiume (wa kwanza alikuwa wa kike). Kwa sasa nina watoto wanne, wawili wa kike na wawili wa kiume (kila mke mmoja akiwa na mtoto wa kike na kiume). Wanapendana sana na tunaishi kwa amani iliyopitiliza.
Wadau, nimejitahidi kufupisha ili nisiwachoshe.. and this marks the end of how I met my wife...!!.
Nzi Chuma, hadhuriwi na uvundo
Hongera sana ila sophy alikuwa mjanja sana na ulisema mtoto alikufanana kumbe ilikuwa wenge tuu
Sent from my iPhone using JamiiForums