Hii nchi ina mambo ya ajabu sana. Rais wa nchi aliyeunda tume ya Warioba hana mamlaka ya kusimamisha hili Bunge la Posho! Mwenye mamlaka hayo ni huyo fisadi Sitta!!! Hivi hii sheria ya Bunge hili la posho kutoweza kuvunjwa na Rais bali mwenye mamlaka ya kulivunja ni Spika ilitungwa katika kikao kipi cha Bunge? Kama kuna mtu ambaye amewahi kuiona sheria hii hebu aiweka hapa. Kweli hi nchi ni kichwa cha mwendawazimu, Rais wa nchi anaona pesa za walala hoi bilioni 21 zikiteketea bila la maana lolote kufanyika. Rais kauchuna tu!!!
Hivi Kikwete leo hii akiamua kulivunja Bunge hili la posho, mamlaka ambayo hana je, atachukuliwa hatua za kisheria zipi!? Na ni taasisi ipi itakayomchukulia hatua za kisheria Rais? Bunge la posho au Bunge la Jamhuri? au ni Sitta ndiye atampandisha kizimbani Rais? Je, Rais kwa kulivunja Bunge hili la posho na hivyo kunusuru mabilioni ya pesa za walipa kodi anaweza kufungwa au kuondolewa madarakani kwa nguvu!? Ujinga umezidi kukithiri nchi hii.