How govt will spend Sh21bn for nothing

How govt will spend Sh21bn for nothing

Unlike Robin Hood who robbed the rich to give to the poor, this robber from Urambo is robbing the poor who cannot even afford a meal a day!!! Mungu atamuadhibu hapa hapa duniani siku si nyingi.

nimependa sana post hii !
 
halafu ukiwaangalia hata waliobaki ndani ya CA hawajiamini KABISA na wanaona aibu sana ! Wamebaki tu kwa kuogopa KUSHUGHULIKIWA , UNACHANGIAJE KITU AMBACHO UNAJUA HAKITATUMIKA POPOTE ? SHAME !
 
Naomba kujua hivi katika viongozi wa dini waliopo kuna Padre au Askofu wa Katoliki ambaye bado yuko katika hili bunge? Km ndiyo naomba kujua ni padri wa Parokia gani na au Askofu wa jimbo gani?
 
Sitta is driven by the hidden sides of his personality traits which are not less than ego, stubbornness, arrogance and dictatorship. Continuing with the CA meetings against consensus reached by his Party Chair who is also a President with UKAWA proves unreasonable insubordination, brutality, lack of team spirit and hypocrisy. It is clear now Sitta is fighting for both Ccm and personal interests or else he would have not have been adamantly proceeding with the controversial CA even where he knows about the agreement reached.

I guess Sitta wants to utilize this opportunity to meet his personal intents knowing is the last chance in his life as no one , in any circumstances will entrust him with such authority again after this mess.

Besides, I see this is a typical true color of Ccm . disrespecting leadership and freedom of every one to use whatever he possesses and any available means to achieve what one wants. The world has been witnessing how corruption, manipulation, cheating and political assassinations without checks, and in totality have been blessed and put in best practices of Ccm!.

Honestly I dont expect any force from outside is gonna impart positively changes to ccm cultural practices. The best solution is to vote ccm out, regardless qualities of individual contestants as is now evident that ccm as a system is coercing everybody into its madness. No one remains the same when is involved with ccm, the conscious' assassin.

21 Billion is a lot and for a sensible Government, it would have significantly contributed to provision of various solutions to the suffering Tanzanians. BUT PASSING THAT FAKE CONSTITUTION WOULD BE MORE COSTLY COMPARED TO 21 BILLIONS. Imagine If ccm has been shameless able to ignore outcries of Tanzanians, and deliberately misappropriate 21 billions without nerves, how much would be STOLEN directly and indirectly through the Ill Constitution if it was to be in force?

How many Tanzanians would die for lack of services resulted to unquestionable poor governance? What kind of generation in terms of intellectual competencies would be manufactured out of weak education system orchestrated by irresponsible and unaccountable system?


I see, a loss of 21 Billion is unacceptable but is less harmful than deterrent of Tanzanians' lives to infinity which would occur by passing what ccm is doing in Dodoma!. By stopping this fake constitution, we shall be able to come up with a right one that will take us through to our brighter future while working on recovering our stolen 21 Billions.

Good day friends!.
 
Una akili sana Mkuu MANI. Hili la katiba mpya ndio limetoka maana 2015 baada ya MACCM kuchakachua uchaguzi kwa kushirikiana na vyombo vya dola na Tume ya uchaguzi ya MACCM na hivyo kufanikiwa tena kumuweka Rais wa MACCM huyo Rais ajaye anaweza kabisa kusema katika awamu zake mbili mjadala wa kutunga katiba mpya hauna kipaumbele chochote, Serikali "haina pesa" na uongo mwingine wa kila aina. Tutamfanya nini? maana wanajua vyombo vya dola vyote ni vitengo vya MACCM. Hivyo hili la kupatikana katiba mpya ambayo itakubaliwa na Watanzania walio wengi ndio tusahau kabisa tutaendelea kuwa na katiba ya MACCM kwa miaka chungu nzima ijayo.

Hivi Sitta hana mtu wa kumuwajibisha? Jk naye anashindwa nini kuonyesha nguvu ya uraisi kwa kulivunja hili bunge. Mnapo sema mtaendelea na mchakato 2015 mna hakika gani raisi ajae atakubali huu uhuni uliofanywa na bunge la Sitta let alone ccm kushinda.
 
Last edited by a moderator:
[h=2]People worried JK's successor might not prioritise new constitution writing[/h]

By The guardian team



11th September 2014

jk-sept11-2014.jpg

President Jakaya Kikwete

Wananchi have expressed worries that a new constitution may after all not be realised this despite reassurance by President Jakaya Kikwete and other party leaders who met twice last week.

The public’s general view gathered from separate interviews with The Guardian yesterday was that the process be suspended with immediate effect saying its continuation was ‘a waste of tax payers’ money.’

Several interviewees were of the view that even though the President and Tanzania Centre for Democracy (TCD) pledged that the process will be completed next year after the General Election they are concerned that the incoming president may not necessarily prioritise the issue.

Home
Hivi Sitta hana mtu wa kumuwajibisha? Jk naye anashindwa nini kuonyesha nguvu ya uraisi kwa kulivunja hili bunge. Mnapo sema mtaendelea na mchakato 2015 mna hakika gani raisi ajae atakubali huu uhuni uliofanywa na bunge la Sitta let alone ccm kushinda.
 
Una akili sana Mkuu MANI. Hili la katiba mpya ndio limetoka maana 2015 baada ya MACCM kuchakachua uchaguzi kwa kushirikiana na vyombo vya dola na Tume ya uchaguzi ya MACCM na hivyo kufanikiwa tena kumuweka Rais wa MACCM huyo Rais ajaye anaweza kabisa kusema katika awamu zake mbili mjadala wa kutunga katiba mpya hauna kipaumbele chochote, Serikali "haina pesa" na uongo mwingine wa kila aina. Tutamfanya nini? maana wanajua vyombo vya dola vyote ni vitengo vya MACCM. Hivyo hili la kupatikana katiba mpya ambayo itakubaliwa na Watanzania walio wengi ndio tusahau kabisa tutaendelea kuwa na katiba ya MACCM kwa miaka chungu nzima ijayo.

Dawa tuombe mungu watanzania walichukulie hili kama ajenda ya kuwaadhibu 2015.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Hivi Sitta hana mtu wa kumuwajibisha? Jk naye anashindwa nini kuonyesha nguvu ya uraisi kwa kulivunja hili bunge. Mnapo sema mtaendelea na mchakato 2015 mna hakika gani raisi ajae atakubali huu uhuni uliofanywa na bunge la Sitta let alone ccm kushinda.

we hujui kitu.. kiongozi yoyote wa nchi yoyote duniani lazima awe na maamuzi binafsi kwa ajili ya taifa lake. haijalishi udogo wake. lkn kama katika nchi yanatokea mambo magumu na mazito yahusuyo nchi yake ni lazima afanye maamuzi either ni magumu kwa kiasi gani hapa lazima achukue hatua kwa ajili ya kuokoa taifa lake. sasa! ukiona hakuna maamuzi yoyote yanachukuliwa na kiongozi mkuu kwa ajili ya nchi yake basi utambue kuwa nchi haina kiongozi bali ina sanamu tu ambalo nadhani wewe unafahamu sanamu huwa linafanyaje ukilisemesha. hii ndio picha tunayoiona mbele ya mtawala huyu.
 
Hili pamoja na wengi wetu kuomba litokee sijui kama litatokea Mkuu. Kuna baadhi ya Watanzania wakishapewa ubwabwa, kofia, kanga na fulana za rangi ya Yanga basi kwa wao MACCM ni nambari one. Na MACCM kwa kushirikiana na vyombo vya dola na kitengo chao kingine cha Tume ya uchaguzi hawaogopi kuchakachua chaguzi kuanzia ngazi za chini hadi za juu.

Dawa tuombe mungu watanzania walichukulie hili kama ajenda ya kuwaadhibu 2015.
 
UKAWA wamtwisha zigo JK

  • Wamtaka asitishe mara moja Bunge Maalumu
  • Samuel Sitta ‘alazimisha' Katiba
  • Rais Shein atwishwa lawama
11/09/2014 | Posted by Waandishi Wetu | |


SIKU mbili baada ya mazunguzo baina Rais Jakaya Kikwete na viongozi wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), kukubaliana Bunge maalumu lisitishwe Oktoba 4 mwaka huu, Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umemtaka atoe tamko haraka kwenye gazeti la serikali kusitisha bunge hilo mara moja kunusuru zaidi ya sh 3,090,000.
Kwa mujibu wa UKAWA, fedha hizo zinatosha kujenga madarasa 195 kwa sh milioni 20 kwa kila moja au kuwaongeza posho askari 35,000 kila mmoja sh 111,000.
Zaidi ya hayo, UKAWA umedai kitendo cha Bunge Maalumu la Katiba kuendelea bila uwepo wa Waziri wa Sheria na Katiba na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar bila Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kutoa kauli yoyote, ina maana vitendo hivyo vilikuwa na baraka za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar jambo linalozidisha mgogoro wa Muungano.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari kwenye ofisi ya NCCR Mageuzi jijini Dar es Salaam jana, viongozi wa UKAWA wamesema Bunge lisipositishwa watatangaza ni mikakati gani watakuja nayo kwa wananchi mapema wiki ijayo, huku wakishukuru kusimama kwa mchakato huo, kwani uchakachuaji uliyokuwa umefanywa kwa kukiuka kanuni mbalimbali sasa umekuwa kazi bure.

Aidha, UKAWA wamemtaka mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG), achunguze ufisadi wa fedha katika Bunge Maalumu la Katiba, wakidai wajumbe wa Bunge la Katiba waliyobaki walikuwa ‘kombakomba' huku wakikosa hata tone la aibu kuondoka huko, ingawa walijua kuwa Bunge hilo lisingepata Katiba mpya ambayo ingepigiwa kura.

Katika mkutano huo, viongozi wa UKAWA wamewaondolewa wananchi wasiwasi kuhusu iwapo baada ya uchaguzi mkuu suala la katiba litaendelea au la. Wamesema kuwa walikubaliana na Rais kuwa vyama vya siasa viandae mapendekezo ya mambo machache na ya msingi, yatakayokubaliwa na wadau wote yapelekwe serikalini, hivyo suala la katiba mpya litawekwa sasa kwenye sheria ili rais ajaye alazimike kulifanyia kazi mara baada ya kuingia madarakani.

Mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia akisaidiana na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa, walisema wajumbe wa Bunge Maalumu walikosa hata tone la aibu hata baada ya kugundua siku zilizobaki hazitoshi na akidi kutotimia, walishindwa kutumia mwanya huo kusema Bunge lisitishwe badala yake wakaendelea ili waendelee kuchukua posho.

"Walijua mchakato hauwezi kukamilika, akidi ilikuwa haitoshi, Mwanasheria wa Zanzibar hakuwepo, Waziri wa Sheria wa Zanzibar hakushiriki, lakini wajumbe hawa kwa sababu ya tabia ya kombakomba hawakutaka kuacha senti chache zilizobaki ili waendelee kuchukua posho bila aibu, hawa ni mafisadi hasa," alisema Prof Lipumba.

Kwa upande wake, Dk. Slaa alisema amebaini kuwa siku zilizoongezwa kwa ajili ya Bunge Maalumu la Katiba hazikuongezwa kisheria, bali zilitangazwa kwa tangazo la serikali tu, ndio maana wanamshauri Rais Kikwete atoe tangazo tu asisubiri wajumbe hao waendelee kutafuna posho kwa kazi ambayo sio ya kisheria na ambayo haitapigiwa kura.

Dk. Slaa, alimshangaa Mwenyekiti wa Bunge hilo kuwahadaa watanzania kuwa kazi zote zitamalizika na zitaenda vema, hivyo kumtaka Rais Kikwete baada ya kushauriana na washauri wake na kubaini kasoro zote hizo, atoe tangazo la kusitisha Bunge hilo kunusuru fedha hizo.

Hata hivyo, akihitimisha kikao hicho, Mbatia alionya kuwa endapo damu ya Mtanzania yeyote itamwagika kutokana na ukaidi na ubabe wa Sitta, basi atapaswa kushitakiwa kwenye mahakama ya kihalifu ya Uholanzi.

Aliongeza kuwa kutokana na ubabe wa Sitta, sasa Mwenyekiti huyo hata Urais hatauona na ubunge wake upo hatarini, kwani UKAWA watakwenda kupiga kambi jimboni kwake kuwaeleza wananchi madhambi yake aliyofanya kwenye Bunge Maalumu la Katiba.

Mrema, Cheyo na Dovutwa wasaliti
Katika hatua nyingine akionyesha nyaraka za makubaliano waliyofanya, Mbatia aliwatupia lawama viongozi wa vyama vingine vya upinzani kwa kushindwa kusaini makubaliano ya kusitisha Bunge yaliyosainiwa na UKAWA kwa upande mmoja na CCM kwa upande mwingine, akisema viongozi wa vyama hivyo hawataki Bunge lisitishwe ili waendelee kuchukua posho.

"Augustino Mrema, John Cheyo na Fahmi Dovutwa, wameshindwa kusaini makubaliano haya wakitaka waendelee uchukua posho, kwa hapa naona wamepitiliza kuliko hata upande wa CCM amesaini Mzee Philipo Mangula kwa niaba ya Rais," alisema Mbatia.

Sitta ‘alazimisha Katiba
Licha ya Rais Kikwete kuridhiana na vyama vya siasa, kwamba Bunge Maalum la Katiba liishie Oktoba 4 mwaka huu, ili mchakato huo uendelee baada ya uchaguzi mkuu wa 2015, Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta amesema rasimu ya mwisho itatolewa Septemba 21 na kuanza kupigiwa kura Septemba 26 mwaka huu.

Hatua hiyo ni baada ya Kamati ya Uongozi ya Bunge, kuifanyia
marekebisho ratiba ya awali ili iendane na muda uliyosalia kufikia
Oktoba 4, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo aliahidi rasimu hiyo
ingekabidhiwa kwa Rais Kikwete Oktoba 31, mwaka huu.

Kwa mabadiliko hayo ya ratiba, sasa Bunge hilo litamalizika huku
wajumbe wakiwa wamefanya uamuzi wa sura na ibara za rasimu kwa kuzipigia kura, na kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba, ili uamuzi huo uweze kukubalika, lazima ipatikane theluthi mbili ya kura za wajumbe kwa pande zote mbili za Bara na Visiwani.
Pamoja na Bunge hilo kufikia hatua ya kuandika katiba mpya
inayopendekezwa, kuendelea kwa mchakato huo, kutategemea ridhaa na busara ya Rais wa awamu ya tano atakayemrithi Kikwete kama ataamua uanzie hapo ulipoishia au uanze upya.
Ili kuhakikisha wajumbe wake wote wanakuwa wamoja na kuiunga mkono rasimu itakayopendekezwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimewafunga midomo baadhi ya wabunge wake ambao wanaonekana kutounga mkono muundo wa serikali mbili kinaoupigia chapuo.
Akitangaza ratiba mpya jana bungeni mjini hapa, Sitta alisema kuwa siku 60 za Bunge Maalum ambazo ni nyongeza waliyopewa na Rais Kikwete kwa mujibu wa sheria, bila kuhesabu siku za Jumamosi, Jumapili na sikukuu, zinaisha Oktaba 4 mwaka huu.
"Nafurahi kuwafahamisha kwamba katika kikao cha kamati ya uongozi jana, tumejiridhisha tunakwenda vizuri na kamati ya uandishi ambayo imekuwa ikitazama mambo yanavyokwenda na mjadala ulivyokuwa, imejipanga kutupa rasimu ya mwisho Septemba 21 mwaka huu.

"Kwa hiyo ni dhahiri kabisa kwamba lengo tulilopewa na taifa la kutoa katiba inayopendekezwa tunalimudu ndani ya wakati. Tunaangalia utaratibu wa upigaji kura kwa wenzetu ambao wana sababu mbalimbali nje ya ukumbi huu, ukiacha wale waliosusia," alisema.

Kwa mujibu wa Sitta, kura za kuamua ibara na sura za rasimu zitaanza kupigwa Septemba 26, mwaka huu, na kwamba wako wajumbe wana sababu za kutokuwepo, hivyo wataangalia utaratibu wa kuwafuata popote wapige kura.

"Tutatoa maelezo ya utaratibu upi utatumika kwa sababu akidi inatuhusu sisi wote tulioteuliwa na mheshimiwa Rais kuwa wajumbe wa Bunge Maalum.
"Tunawasiliana na balozi zetu nje ili wajumbe waliyoko huko wakiwemo wanaopata matibabu nchini India ili watumiwe rasimu waweze kupiga kura,"alisema.

Pia aliwataka wajumbe Waislam ambao wanakusudia kwenda hija nje ya nchi, kujiandikisha na kuacha taarifa zao za mawasiliano yao kwa ajili ya ofisi ya Bunge kufanya utaratibu wa kuwawezesha kupiga kura popote watakapokuwa.

Wajumbe CCM
Katika kuhakikisha wajumbe wake wanaunga mkono muundo wa serikali mbili na kuipitisha rasimu ya mwisho itakayotolewa na Bunge Maalum, juzi usiku CCM iliitisha kikao na kuwaweka sawa wajumbe wake.

Hatua hiyo ilitokana na mgawanyiko uliyojitokeza ndani ya Bunge baina ya wajumbe Waislamu na Wakristo kuhusu hoja ya kuingiza suala la Mahakama ya Kadhi katika katiba.

 
Namuona Sitta akichanganyikiwa mwaka 2015 baada ya kukosa hata Ubunge baada ya kuwa amepigwa chini katika uteuzi wa CCM na EL wa Urais na anaomba kujiunga na ACT apate walau ukatibu wa Wilaya nao wanamkatalia.
 
Mkuu Tized hii nchi kwa kweli inaudhi sana. Rais ana mamlaka ya kupindisha sheria ili mafisadi, wauza unga, majangili na magaidi wasiguswe na mkono wa sheria. Kwa mfano kama utakumbuka katika sakata la EPA Rais alitamka hadharani kwamba wahusika ufisadi ule wa $133 million wamerudisha pesa na hakutaka majina yao yatajwe hadharani. Kwenye sakata la wauza unga alidai list ya majina ya wauza unga anayo lakini mpaka hii leo haijaweka hadharani. Kwenye mabilioni ya Uswiss uchunguzi ni zaidi ya miaka miwili sasa na hajatia neon hata siku moja kuhusu mabilioni ya Uswiss na hizi bilioni 200 za Escrow nazo ameamua kuwa kimya kabisa (hayamuhusu).

Ikija kwenye kuokoa mabilioni chungu nzima ya walipa kodi kwenye Bunge la Mafisadi wapenda posho eti Rais wa nchi hana mamlaka!!! Alikuwa na mamlaka ya kuwateua na wabunge wa BMK na hivyo kuunda BMK lakini kwenye kulivunja hana mamlaka!!! Mwenye mamlaka ya kulivunja bunge hilo ni fisadi Sitta! Sijui walifikiria nini hadi kumnyima Rais mamlaka ya kuvunja BMK.

Inatia hasira sana mkuu BAK

Tumeshafikia hatua sasa tumezoea hii hali na sisi tumekua sehemu yake kuona hela zetu zinafujwa kirahisi kiasi hiki.
Watu wengi sasa maweshakata tamaa kutokana na philosofia ya uongozi kwa Kaka mkubwa ambao umepelekea wa chini wafanye watakavyo tu...

Naogopa sana mwisho wa huku kutaka kwetu tamaa kutakapofikia yatatokea nini................ Kwa bwana six hii bila shaka ndio fursa yake ya mwisho ya kuchaguliwa atabaki kuteuliwa tu wa walaji wenzie.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu BAK Huyu bwana kutokana na uoga wake wa kufanya maamuzi na kutaka kwake kupendwa na kila mtu hata na shetani.... amejua aina ya watawaliwa alionao na kwa kweli anawapatia sana yanapokuja maswala mazito kama haya... anajua hili nalo watapiga kelele mwishoni watalala. Simple as that. ... Na kweli wadanganyika watapika kelele wataonekana ITV kwenye kipima joto, TBC na Star Tv na matamko mbalimbali ya akina Deus Kibamba na akina Usu Malya basi... business as usual.

Tatizo kubwa lipo kwetu sisi waajiri wake na sio yeye. Na inavyoonekana waajiri tunalalama tu tukipiga kelele n.k n.k Ingekua kwa nchi za wenzetu au hata hapo Kenya tu... Wangeshalitibua zamani sana.

Sijui nani ametuloga au woga umetuzidi au ndio ile ''Amani ya Kupumbaza'' anayoisemaga Mh MB Godbless Lema.

Mkuu Tized hii nchi kwa kweli inaudhi sana. Rais ana mamlaka ya kupindisha sheria ili mafisadi, wauza unga, majangili na magaidi wasiguswe na mkono wa sheria. Kwa mfano kama utakumbuka katika sakata la EPA Rais alitamka hadharani kwamba wahusika ufisadi ule wa $133 million wamerudisha pesa na hakutaka majina yao yatajwe hadharani. Kwenye sakata la wauza unga alidai list ya majina ya wauza unga anayo lakini mpaka hii leo haijaweka hadharani. Kwenye mabilioni ya Uswiss uchunguzi ni zaidi ya miaka miwili sasa na hajatia neon hata siku moja kuhusu mabilioni ya Uswiss na hizi bilioni 200 za Escrow nazo ameamua kuwa kimya kabisa (hayamuhusu).

Ikija kwenye kuokoa mabilioni chungu nzima ya walipa kodi kwenye Bunge la Mafisadi wapenda posho eti Rais wa nchi hana mamlaka!!! Alikuwa na mamlaka ya kuwateua na wabunge wa BMK na hivyo kuunda BMK lakini kwenye kulivunja hana mamlaka!!! Mwenye mamlaka ya kulivunja bunge hilo ni fisadi Sitta! Sijui walifikiria nini hadi kumnyima Rais mamlaka ya kuvunja BMK.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Lawama zianzie kwa kikwete kushuka chini, yeye ndo anawapa nguvu ya kufanya hivyo.
 
Folks, this is what happens when the basic qualification for leadership in the country is being good at corruption and deceit. Kwani tulidhani ni nini kitafuata? Walitoa hela kwa kuwa kwao ile ni biashara tu! Unatoa mtaji, halafu unatafuta faida! Simple as that.

Mathalan, hata uteuzi wa wajumbe karibu wote ulibebwa na rushwa, hata kama siyo za moja kwa moja. Najua wengi hawatanielewa. Lakini ilie tu kuwa waliteuliwa na Rais, amabye he turns out to mwenyekiti wa CCM, amabye kipindi anakampeni tulishuhudia jinsi alivyoshiriki kampeni kwa kejeli na matusi, rushwa na wizi, bila kusahau kubebana katika uteuzi ndani ya chama! Unategemea kizaliwe nini hapo? Uzalendo? Kweli? Katika utaratibu huo kilichotengenezwa ni kusanyiko la wanasiasa-mafisi, wenye uchu na uroho wa kila senti inayopatikana karibu.

Lakini bado nawshangaa na wle wenzetu walio bungeni! Ilikuwaje wakakubaliana na upuuzi huu tangu mwanzo? Kwa wanaojua, kulikuwa na kasoro tangu kuundwa kwa sheria ya katiba. Sheria ilionyesha wazi kukwama kwa mchakato wa katiba mapema. Kivipi? Pale iliposema wazi kuwa:

1. Wajumbe wa bunge Maalum la Katiba watakuwa:

i. Wabunge wote wa bunge la Jamhuri ya muungano-wa kuchaguliwa na kuteuliwa!.....ambapo hata mjinga anajua kuwa katika hali ya kawaida hakuna uwiano wa idadai katika bunge hilo. Kwamba wale mafisi ni wengi kuliko wengine! Lakini hata hao wengine wakakubali!!!!!

ii. Ili kuleta uwiano wa uwakilishi katika Bunge Maalum la Katiba kutakuwa na nyongeza ya wajumbe 201 kutoka makundi maalum........wajumbe hao watateuliwa na rais baada ya kuchaguliwa na vikundi vyao na majina 3 kuwasilishwa kwa Rais..... Kwamba wote hawakuona kuwa Rais anayetajwa ndiye mwenyekiti wa Chama cha Mafisadi-CCM, chama ambacho kimekumbatia mafisadi kwa muda mrefu na kwa nguvu zote. Kwamba hata yeye Rais ana kashfa yake ambayo haisemwi tu kwa kumwogopa! Kwamba hata hao wenzetu waliona Rais huyo anafaa na anatosha kufanya kazi hiyo ya uteuzi? Kwamba ana sifa za kutosha kututeulia wawakilishi waadilifu wakati yeye mwenyewe hajwahi kuwa muadilifu! Au tulitegemeaje? Kwamba ukimtuma fisi akalete marafiki zake ataweza kabisa kuwa na uwezo wa kuleta kuku eti tu kwa kuwa ni waadilifu! Kwa hali ya kawaida hata mtoto angeweza kujua kuwa ukimpa kazi hiyo fisi ataleta fisi wenzake! Ajabu ni kuwa hawa wenzetu hawakuona hilo, hata baada ya mimi kuwaandikia baadhi yo mapema tu-wakati wa kuandika sheria hiyo!.....kuna wakati nakosa imani na wanasiasa kabisa!

Lakini nimalizie kwa haya ya mwisho. Kwamba Serikali ilishatoa tamko kuwa Katiba hapana! Waziri Kombani na Mr Mwanasheria mkuu wakasema haihitajiki, mara ghafla rais anasema itaandikwa. Mara kama ndoto CCM imeshika kibendera cha katiba kama siyo wao waliosema haihitajiki- hakuna aliyeamka wala kustuka! Mpaka ikapitishwa sheria mbovu haaaa-salama kabisaaaaa! mara uteuzi ukawa una maluweluwe haaaa! baridiiii kabisa. Leo matusi na kejeli yameanza ndiyo tunakurupuka kuwa hatuko sawa! Leo mafisi yanapitisha vifungu kwa ubinafsi na ubabe ndiyo tunajuwa wametuzidi idadi! huu ni upunguwani!

Kana kwamba haitoshi, imekuja hii ya mwisho, kwamba hata rais anaona katiba imeshindikana lakini hataki kuchukua maamuzi magumu. Wao waendelee kule Ddodma kufuja hela na mchakato utaendelea baada ya uchaguzi!!!! Nadahni tukubalianae tu kuwa:

Kwa kuwa CCM iliona hakuna haja ya katiba, na kwa kuwa iliamau kwa makusudi kuamua kuuharibu mchakato huo ni wazi kuwa lengo halikuwa katiba bali ulaji kama kawaida! na ndiyo maana hata baada ya kuona katiba haitaweza kupatikana, bado tumeendelea kujiweka bungeni na kulipana posho huku tukijua kuwa katiba haitapatikana!

Kinachonishangaza tu ni kuwa hawa wanafanya haya kwa kuwa sisi wananchi tuekubali wayafanye. Ni kwa nini tumewapa mamlaka hayo? What are we gonna do about it?


 
Huu mchakato una negative impact kwa ccm. Na ni makosa ya wababe wachache
 
Ni with each ache sana wanafuatilia yanayojadiliwa kama is hara ya kuudhika
 
Back
Top Bottom