Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Pamoja na kwamba CHADEMA ni wazuri sana katika kujenga hoja na katika hotuba zao lakini natamani wana JF mjaribu kuweka maoni yenu hapa juu ya mambo ambayo ni muhimu wananchi wakayasikia siku ya Alhamisi. Lengo ni kujaribu kutafakari kwa pamoja kama kuna faida kwa maamuzi yaliyochukuliwa au la. Haya hapa chini ni maoni yangu kwani naamini hatua zilizochukuliwa ni sahihi kabisa.
1. Sababu ya kutokumtambua meya haikuwa ni kwa kukosa vyeo. Ilikuwa ni ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi na kutokuwapo kwa haki.
2. Pale ambapo madiwani waliokuwa wanapigania haki wanafuatwa na mtu au kikundi cha watu na baada ya hapo ghafla wanageuka na kubadilisha agenda toka kwenye ukiukwaji wa haki na kutokufuatwa kwa taratibu na sheria, na kuishia kuigeuza agenda hiyo kuwa agenda ya kugawana madaraka, basi mtu unaweza kuamini kuwa kuna nguvu nyuma ya jambo hilo. Na endapo chama bado kilijaribu kuwasaidia kujenga msingi wa kusimamia haki, bado chama kikageukwa basi ni rahisi watu kuamini kuwa kuna nguvu nyingine nyuma yao.
3.Chama makini hakiwezi kuruhusu wanachama wake wachukue hatua ambazo ni kinyume na misingi ya haki, demokrasia na ustawi wa utaratibu na sheria kama ilivyo imani ya chama chao, kisha wao wafuate maslahi binafsi au vyeo.
a)Hatuwezi kuwa kama wengine wanaosema watavua magamba na kila siku wanaendelea kuahirisha kwa hofu ya kuogopa matokeo yanayoweza kuletwa na maamuzi magumu.
b) Pale ambapo kwa sababu zisizoeleweka na kwa ghafla wanachama wanabadilisha msimamo basi kunakuwepo na mmomonyoko wa maadili
na hapo inabidi kuchukua hatua hata kama hatua hizo zitakigharimu chama kukosa nafasi ya udiwani, lakini tutakuwa tumejenga na kutetea haki hata kama ni kwa hasara yetu.
4. Endapo tutashindwa kuchukua hatua basi hatukuwa na haki ya kupiga kelele na kuwashangaa wale wanaoshindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi huku wakiahirisha kila siku. Hatuwezi kuruhusu Gamba kuota kwani tunajua magamba yakiota inakuwa vigumu kuja kuyavua kwani mengine yanaleta hofu ya kutoa damu yakishaachwa kwa muda mrefu.
5. Ujumbe tunaotaka uende kwa kila mtanzania ni kuwa CDM ni chama kinachosimamia na kutekeleza kwa vitendo misingi ya utawala bora na ufuatwaji wa haki , taratibu na sheria na maadili.
6. Mambo yanayofanywa kihuni na kwa ubabe hayapaswi kukubaliwa hata kama matokeo yake yana maslahi binafsi kwangu. Ni lazima tuangalie mbali na kusimamisha, kuenzi na kuheshimu utaratibu wa kisheria na kutimizwa kwa matakwa ya demokrasia.
7. Hatuwezi kuwa kama watu wengine ambao uongozi umewashinda, huku wakitoa matangazo ya kufukuza watu na bado wakipatwa na hofu kila wanapokutana wanaishia kuahirisha maamuzi magumu. Ni lazima chama makini kichukue maamuzi magumu kwa maslahi ya taifa na maslahi ya taifa kwa hili ni kuzuia ukiukwaji wa haki taratibu na misingi ya kidemokrasia katika chaguzi mbalimbali. Ni kuonyesha bayana kuwa heshima sio cheo cha kibinafsi au umaarufu bali ni heshima ni kutimizwa kwa matakwa ya demokrasia.
TUNAAMINI KUWA WANANCHI WALIOWACHAGUA WALIWACHAGUA ILI WAKADUMISHE DEMOKRASIA HAKI NA UTARATIBU WA SHERIA. WANANCHI WA ARUSHA WAKIWEMO VIONGOZI WA DINI WALIONA UHUNI NA UBABE ULIOFANYWA WAKATI WA UCHAGUZI WA MEYA NA UKIUKWAJI WA HAKI. WANANCHI WALIWACHAGUA VIONGOZI KWA KUKIAMINI CHAMA MAKINI KILICHOWATEUA, NI KWA MISINGI HIYO HIYO WANANCHI HUPOTEZA IMANI KWA CHAMA CHAO PALE AMBAPO WANAGUNDUA KUWA WALIOTUMWA WANAFANYA VIBAYA AU TOFAUTI NA MATAKWA YAO, NA KAMA NI KUWAONDOA NI HADI PALE WANAPOSUBIRI UCHAGUZI MWINGINE. HIVYO CHAMA KINAPOCHUKUA HATUA WANANCHI WAKITUMIA BUSARA YAO WATAONA WAMEPUNGUZIWA MZIGO WA KUNGOJA HADI UCHAGUZI MWINGINE WAKATI WALIOWATUMA WAMEGEUKA NA KUUNGA MKONO UKIUKWAJI WA TARATIBU, HAKI, DEMOKRASIA NA MISINGI YA SHERIA
NAOMBA KUWASILISHA ONGEZENI HAPA CHINI
1. Sababu ya kutokumtambua meya haikuwa ni kwa kukosa vyeo. Ilikuwa ni ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi na kutokuwapo kwa haki.
2. Pale ambapo madiwani waliokuwa wanapigania haki wanafuatwa na mtu au kikundi cha watu na baada ya hapo ghafla wanageuka na kubadilisha agenda toka kwenye ukiukwaji wa haki na kutokufuatwa kwa taratibu na sheria, na kuishia kuigeuza agenda hiyo kuwa agenda ya kugawana madaraka, basi mtu unaweza kuamini kuwa kuna nguvu nyuma ya jambo hilo. Na endapo chama bado kilijaribu kuwasaidia kujenga msingi wa kusimamia haki, bado chama kikageukwa basi ni rahisi watu kuamini kuwa kuna nguvu nyingine nyuma yao.
3.Chama makini hakiwezi kuruhusu wanachama wake wachukue hatua ambazo ni kinyume na misingi ya haki, demokrasia na ustawi wa utaratibu na sheria kama ilivyo imani ya chama chao, kisha wao wafuate maslahi binafsi au vyeo.
a)Hatuwezi kuwa kama wengine wanaosema watavua magamba na kila siku wanaendelea kuahirisha kwa hofu ya kuogopa matokeo yanayoweza kuletwa na maamuzi magumu.
b) Pale ambapo kwa sababu zisizoeleweka na kwa ghafla wanachama wanabadilisha msimamo basi kunakuwepo na mmomonyoko wa maadili
na hapo inabidi kuchukua hatua hata kama hatua hizo zitakigharimu chama kukosa nafasi ya udiwani, lakini tutakuwa tumejenga na kutetea haki hata kama ni kwa hasara yetu.
4. Endapo tutashindwa kuchukua hatua basi hatukuwa na haki ya kupiga kelele na kuwashangaa wale wanaoshindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi huku wakiahirisha kila siku. Hatuwezi kuruhusu Gamba kuota kwani tunajua magamba yakiota inakuwa vigumu kuja kuyavua kwani mengine yanaleta hofu ya kutoa damu yakishaachwa kwa muda mrefu.
5. Ujumbe tunaotaka uende kwa kila mtanzania ni kuwa CDM ni chama kinachosimamia na kutekeleza kwa vitendo misingi ya utawala bora na ufuatwaji wa haki , taratibu na sheria na maadili.
6. Mambo yanayofanywa kihuni na kwa ubabe hayapaswi kukubaliwa hata kama matokeo yake yana maslahi binafsi kwangu. Ni lazima tuangalie mbali na kusimamisha, kuenzi na kuheshimu utaratibu wa kisheria na kutimizwa kwa matakwa ya demokrasia.
7. Hatuwezi kuwa kama watu wengine ambao uongozi umewashinda, huku wakitoa matangazo ya kufukuza watu na bado wakipatwa na hofu kila wanapokutana wanaishia kuahirisha maamuzi magumu. Ni lazima chama makini kichukue maamuzi magumu kwa maslahi ya taifa na maslahi ya taifa kwa hili ni kuzuia ukiukwaji wa haki taratibu na misingi ya kidemokrasia katika chaguzi mbalimbali. Ni kuonyesha bayana kuwa heshima sio cheo cha kibinafsi au umaarufu bali ni heshima ni kutimizwa kwa matakwa ya demokrasia.
TUNAAMINI KUWA WANANCHI WALIOWACHAGUA WALIWACHAGUA ILI WAKADUMISHE DEMOKRASIA HAKI NA UTARATIBU WA SHERIA. WANANCHI WA ARUSHA WAKIWEMO VIONGOZI WA DINI WALIONA UHUNI NA UBABE ULIOFANYWA WAKATI WA UCHAGUZI WA MEYA NA UKIUKWAJI WA HAKI. WANANCHI WALIWACHAGUA VIONGOZI KWA KUKIAMINI CHAMA MAKINI KILICHOWATEUA, NI KWA MISINGI HIYO HIYO WANANCHI HUPOTEZA IMANI KWA CHAMA CHAO PALE AMBAPO WANAGUNDUA KUWA WALIOTUMWA WANAFANYA VIBAYA AU TOFAUTI NA MATAKWA YAO, NA KAMA NI KUWAONDOA NI HADI PALE WANAPOSUBIRI UCHAGUZI MWINGINE. HIVYO CHAMA KINAPOCHUKUA HATUA WANANCHI WAKITUMIA BUSARA YAO WATAONA WAMEPUNGUZIWA MZIGO WA KUNGOJA HADI UCHAGUZI MWINGINE WAKATI WALIOWATUMA WAMEGEUKA NA KUUNGA MKONO UKIUKWAJI WA TARATIBU, HAKI, DEMOKRASIA NA MISINGI YA SHERIA
NAOMBA KUWASILISHA ONGEZENI HAPA CHINI