Hotuba ya Upinzani iliyozuiwa Bungeni leo Aprili 01, 2020 hii hapa (Full Text)

Hiyo hotuba ambayo spika kasema ni ya upotoshaji ana maana ukweli wote anaujua yeye tu.

Angeacha isomwe, kipindi cha mjadala na kwa kuwa wabunge wa CCM ni wengi wangeipigia kura ya kuikataa kwa huo unaoitwa upotoshaji.

Sioni hata mantiki ya hao wabunge wa upinzani kuendelea kushiriki hivyo vikao. Labda tu ni kwa kuwa kuna vipaumbele zaidi ya kimoja kuwa bungeni.

Fikiria umealikwa kikaoni halafu huruhusiwi kuongea.

Ina maana wabunge wa upinzani hawapaswi kutoa maoni yao kwa mtazamo wa kiupinzani.

Kwamba watoe maoni yao kwa mtazamo wa CCM hilo linawezekana vipi?




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mie ningekuwa spika nisingeruhusu hiyo hotuba kusomwa bungeni, naona imejaa mipasho wampe Aisha mashauzi au waimba singeli na vigodoro wawasute watu huko mwananyamala.
Ndio shida makao makuu ya ofisi kuyaweka uswahilini
Unaita mipasho sababu masahibu yao hayakuhusu. Moyoni unakiri ukweli lakini mdomoni na kimaandishi unaponda.

Ungekuwa spika bila shaka ungewafukuza nje ya bunge hadi uchaguzi.

Siku zote aliyeshika mpini ndiye mjanja, aliye shika makali ajiandae kuumia tu.

Lakini jiulize pamoja na kujeruhiwa kwanini washika makali wanaendelea kuwepo?

Yahitaji kuona mbali sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dungai anaona wapinzani wanakuwa maarufu sana kuliko yeye kwa hotuba zao kwahiyo yeye anaona yeye anatamani angekua maarufu kuliko upinzani ndio maana anaubania.Dungai anafanya mambo kwa utashi wake tu na sio kwa kufwata sheria za bunge.
 

UKIMWI alionao na Kisukari +Magufulism ndo Tatizo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kama nitakosea kwa hiki nitakacho kiandika hapa naomba mnisahihishe,sijawahi kusikia kipindi cha JK hotuba ya kambi rasmi ya upinzani kutopokelewa Bungeni hali kadharika hata katika uongozi wa BWM.Kwanini iwe sasa na hii siyo mara ya kwanza nakumbuka katika Bunge lililopita kuna wabunge wa CCM waliichana hotuba ya KUB pale pale Bungeni na hawajachukuliwa hatua yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duru za kimataifa zinaeleza kwamba mpaka muda huu hii hotuba imefika kila kona ya dunia
 
hujakosea .
 
Mkiambia kuwa Magufuli ni dictator muelewage basi, hizo ndo dalili, kamwe hatojitangaza kuwa yeye ndiye!
 
Unataka tukubali kuwa hiyo ndiyo kweli hotuba iliyoandaliwa na kambi ya upinzani bungeni na kuwasilishwa bungeni? Laiti ungetuwekea nakala badala ya wewe kuchukua jukumu la kuichapisha upya humu JF, angalau tungeamini kwa kiasi fulani na madai ya Spika wa Bunge kuyapa mtizamo mpya.

Sinalo la kuongeza zaidi ya kuhitimisha kuwa nia ya kuileta humu jamvini imekosa nguvu ya uhalisia wake, kujadiliwa.
 
Mhe. Ndugai ni mtumiaji wa kinywaji gani? Inawezekana anatuiaga mjani?
 
Ukisoma makini kwa kipindi cha simba wa Yuda huwezi ungana na KUB,Ila ukisoma baada ya uchaguzi na simba wa Yuda kusafiri kwa gharama kubwa utaelewa kuwa hotuba ilitulia na inapaswa kuheshimika kwamba maendeleo ya watu kwanza then maendeleo ya vitu.
 
Hiyo haikuwa bajeti ni porojo

bajeti upinzani hawajui Bajeti ya upinzani hukosoi iliyopo unatengeneza ya kwako kuwa Sisi tungeshika nchi hii ndio bajeti yetu

Hiyo hotuba inaitwa ya bajeti ya upinzani sio bajeti ni porojo naunga mkono Spika aliyeizuia kusomwa hakuna bajeti kwenye hiyo hotuba
 
Ukisoma makini kwa kipindi cha simba wa Yuda huwezi ungana na KUB,Ila ukisoma baada ya uchaguzi na simba wa Yuda kusafiri kwa gharama kubwa utaelewa kuwa hotuba ilitulia na inapaswa kuheshimika kwamba maendeleo ya watu kwanza then maendeleo ya vitu.
For sure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…