HOTUBA ya Seif Sharrif na Majibu yake kuhusu Maridhiano Zanzibar!

Hawa jamaa hawana jipya. Mtu umeshindw chaguzi 3 bado unataka kugombea ili iwe nini? Ili kwamba kuna siku moja kuamini kwako kuwa kura zinaibwa hazitaibwa? May be akiingia mwingine inawezekana zisiibwe.

Waahce uhuni waanze mbele wenye kujua kuongoza waongoze
 
Sitegemei kama itawahi tokea at least on earth kwa rais aliyeko madarakani regardless of how many terms in office atamaliza yote aliyokusudia. Hivyo basi Maalimu Seif ondoka kwenye madaraka ya ukatibu mkuu na Karume, karibu uraiani.

"mchezo wa kupokezana viijiti kwenye uongozi is universal reality"

Mungu Ibariki Tanzania
 
Wananchi hawajajua ni mambo gani yanahitaji yamaliziwe, na kama yana umuhimu sana basi hata akija Rais mwingine atayamalizia, sio lazima awe Karume! Mbona Katibu Mkuu Seif anataka kubinafsisha Ikulu ambayo ni Ofisi ya Umma?
 
Nadhani kama wanaona yapo mabadiliko ya msingi wanahitaji kuyafanya, Amani anao muda wa kufanya mabadiliko hayo kupitia BAraza la Wawakilishi la JAnuary 20 na April na pia muda wa kutekeleza maazimio ya Mkutano wa REDET kuhusu hali ya siasa Zanzibar, wakati wake wa kuondoka madarakani ukifika aondoke mwengine aingie aendelee.

JAna tulikua na dua ya kuiombea nchi na tumekubaliana kwamba yaliopita yamepita kwa kwa kauli tumesema pale MAisara kwamba tumeshasameheana, sasa kama hawa viongozi wao wanahofu na wengine watakao kuja badala yao inaonekana wao bado wanakitu kwenye nyoyo zao na hawajakubali yaishe ninao wasiwasi mkubwa juu ya nia yao wanayodai ni njema kwa ajili ya Zanzibar
 

Kwanza mzanzibari ni nani? Kuna kabila linaloitwa wazanzibari? Kuna "race" inayoitwa wazanzibari? Wau waliokuwa wakiishi Zanzibar walikuwa mchanganyiko. Walikuwepo waarabu, wahindi, wanyasa, wangazija, wafaransa, waingereza n.k. Wote hawa walijitambulisha kwa uasili wao na sio uzanzibari. Mwarabu alikuwa mwarabu, mtumbuka mtumbuka, mhindi mhindi, mnyasa mnyasa n.k. Huo utaifa wa uzanzibari ni kitu kigeni na wala si cha muda mrefu. Watumwa waliokuwa wakiuzwa Zanzibar walitoka kwenye bara la Afrika. Wengine walinunuliwa na watu waliokuwa wakiishi Zanzibar na walitumikishwa majumbani na kwenye mashamba. Wengine walisafirishwa kwenda uarabuni na baada ya biashara ya utumwa Afrika Magharibi kuwa ngumu,wengine walinunuliwa na wazungu na kupelekwa Marekani na kwengineko. Biashara ya utumwa kwa kiasi kikubwa ilifadhiliwa na wafanyabiashara wa kihindi ambao walitoa pesa kwa waarabu ( nadhani unatambua kuwa muarabu alikuwa mtu yeyote aliyekuwa na damu ya muarabu hata kama alichanganya kama Hamad bin Muḥammad bin Jumah bin Rajab bin Muḥammad bin Sa‘īd al-Murgab maarufu Tippu Tib) ambao walisafiri ndani kwenda kununua watu (hawa hawakuwa watumwa wakati huo) kutoka kwa baadhi ya makabila. Watu hawa wengine walitokana na matekwa wa vita baina ya makabila, watu ambao walionekana hawakubaliki katika makabila kwa sababu yeyote (wachawi, wezi n.k.) n.k. Wengine walichukuliwa kwa maelewano kuwa watasaidia kuwabebea mizigo hao wageni. Pamoja na kuyalaumu haya makabila kwa ushiriki wao katika biashara hii haramu ni lazima tukumbuke kuwa dhana ya kumnunua au kumuuza binadamu mwenzako ililetwa hapaa kwetu na waarabu na kwa wenzetu na waarabu pamoja na wazungu.

Watumwa hapa kwetu na sehemu nyingi tu duniani ( ulaya, asia n.k) ulitokana na matekwa wa vita, watu ambao walifanya uovu na sehemu nyingine madeni. Mtumwa hakupoteza utu wake. Kulikuwa na mipaka ya vitu ambavyo anaweza kufanyiwa na alikuwa na haki zake. Waarabu hao unaowatetea ndio walileta tafsiri ya binadamu kama bidhaa. Kwa kuwa alikuwa bidhaa, mwenye mtumwa alikuwa na haki ya kumfanyia chochote atakacho na waliwafanyia. Waliwatumia kama target katika mazoezi ya shabaha, waliwahasi, waliwanyang'anya watoto wao, waliwabaka na matendo mengine maovu. Kwa mtu yeyote kutetea hii biashara na kudai kuwa hao waarabu walichokileta ni uarabu ni beyond contempt. Hasa kama huyo jamaa anajiita mwafrika!

Hao unaowaita wastaarabu hata siku moja hawakujihesabu ni wazanzibari mpaka wimbi la waafrika kuanza kudai haki zao. Ingawa Sultan wa Oman alihamisha makao makuu yake Zanzibar haikuwa na maana kuwa Zanzibar ilitawala Oman. Zanzibar ilitawaliwa na kuingizwa katika himaya ya Oman. Hao unawaita wastaarabu walipobanwa na wazungu kukomesha biashara ya utumwa, na bandari yao kuzingirwa na kuziwa kusafirisha watumwa, walijenga mji wa Dar es Salaam ambao walitegemea utawapa nafasi ya kuendeleza biashara hiyo haramu bila kuingiliwa na wazungu. Hao unaowaita wastaarabu waliona ni haki yao kufanya watu kama mimi kuwa watumwa wao na ndiyo maana huko Saudi Arabia utumwa ulipigwa marufuku mwaka 1959!

Watu wanaojiita wazanzibari sasa hivi wametokana na matunda ya wale waliokuwa wakiishi huko( waarabu, wahindi, wangazija, wanyamwezi, wanyasa n.k.). Wanajumuishwa wale waliokuwa wakijiita waungwana na wale waliokuwa watwana wao. Katika hao waliokuwa watwana wengi wao walitokana na watumwa. Kusema leo kuwa utumwa haukuwahusu ni kuwatukana matusi ya nguoni na ndiyo maana wengi wao hawawaamini mnapotoa machozi ya mamba na kujifanya kuwa ati kuwa nyie wote ni wazanzibari. Mpaka hapo mtakapokiri na kuwaomba msamaha kwa yale mliyowatendea, hatutakuwa na imani na nyie kwa vile tunajua kuwa bado mnatuhesabu kuwa ni watwana wenu. Hilo hatutariruhusu lirudi kamwe. Kwa msemo wa vijana wa siku hizi, mlie tu.

Amandla.......
 
Inaonyesha kuwa Maalim Seif hana imani na CCM, yeye ana imani na Karume tena kwa kipindi hiki tu, not otherwise!
 
they way i ve seen Karume kamuahidi kitu maalim ampigie debe abaki ikulu, Cha msingi maalim na karume watuweke wazi walijadili nini that day!
 
Wasiwasi wa Seif kuhusu haya makubaliano ni kwamba sio rasmi. Walikubaliana tu wawili hawa walipoalikana kwenye ghahawa ya ikulu. Kama ingelikuwa ni zile kamati zilizokuwa zinashughulikia huu mpasuko wa Zn ndio zimefikia muafaka kusingekuwa na wasi wasi hata kidogo. Pili Seif ameonyesha udhaifu mkubwa sana pale anapokubali kuwa atakaechaguliwa baada ya Karume ni kutoka ccm na hivyo kutoendeleza makubaliano. Kwa nini Seif yeye asiamini kwamba cuf itashinda na hivyo kuendeleza haya maridhiano? Hii inaonyesha pia maridhiano haya sii kati ya ccm na cuf bali Maalim na Karume. Labda ithibitishwe kwamba maridhiano haya ni ya ccm na cuf na ni kupitia vikao gani vinavyotambulika kihalali kwa mujibu wa katiba ama ya nchi au vyama husika.
 
Pole sana Mzee naona unajichanganya tu hapa, na yale usiyayajua. Nafikiri inabidi uwatake radhi wewe Wazanzibari. Wazanzibari wanajielewa na wengi wao ni kweli hawahusiani kabisa na mtiririko huo wa watumwa waliotolewa kutoka kwa Mtipu au sehemu nyengine za Bara. Wazanzibari walio wengi ni kutoka sehemu za vijijini (MASHAMBA) mote Unguja na Pemba, ni weusi na wenye asili ya Kiafrika-lakini asilani hawahusiani na kadhia ya utumwa. Ni kweli katika Wazanzibari wa leo wapo wale walioguswa na kadhia ya utumwa lakini ni wachache sana (miongoni wa wale wanaotokana na asili ya kiafrika). Hawa ni wale ambao hawana nasaba na vijijini (Mashamba ya huko)- Ni wale wa kuzikwa Mwanakwerekwe tu. Fundi jitahidi uielewe Zanzibar na Watu wake . Sote tunapinga Utumwa ni jambo baya la Kihistoria.
 

Pumba tupu, hivyo alivyoeleza Maalim imetosha.Ni wazi Zanzibar ilikuwa ni jamii moja sawa na sehemu nyengine yoyote ile.Kuja ukoloni wa kiingereza ndio jamii ilianza kugawika.Hii principle is applicable all over those old colonies.Nenda Rwanda, nenda Burundi...kote humo kulikuwa watu wanaishi fresh walikuja kugawanyika baada ya mkoloni.

Na hiyo principle ya wakoloni kugawa watu, ndio chanzo cha conflicts nyingi za barani afrika.Sasa wewe hapa kwenye hiyo story ndefu sijuwi unatuletea story gani?Zanzibar ni taifa kongwe kushinda Tanganyika, sasa hapo unataka kutuambia kuwa hili taifa miaka yote hiyo ilikuwa halina uongozi na watu wake walikuwa hawajitambulishi kwa uraia wao.???

Acha kasumba za Nyerere ndugu yangu, wazanzibari ni watu wanaoringia sana taifa lao la Zanzibar.Hadi leo wazanzibari hawajakubali kupoteza utaifa wao completely, hii ni kwasababu taifa lao wanaliona lina records nzuri za kumfanya mtu awe really proud of his or her own country.

Hata kama race ni nyingi Zanzibar, kuna sehemu ambayo hakuna?Hapo tanganyika kwani ni vipi?Makabila hayapo?Hakuna huyu mmasai na myakusa??

Mie niliwahi kutoa maoni, kama mtu sio mzanzibari tafadhali kaa kando waachieni hao jamaa wadili na matatizo yao bila ya chochoko.Matatizo yapo kila nchi, Rwanda hapo watu walichinjana na kutoana roho....na sehemu nyengine nyingi tuu hata nyie munazijua za hapo Tanganyika mukitiana mapanga kupigania mifugo.

Sasa hili la Zanzibar nalo halina tofauti yoyote, waacheni wazanzibari wafix problems zao.Kujiingiza kati kati ni kuonesha kuwa muna special interests in those islands...as it has been since Nyerere
 
they way i ve seen Karume kamuahidi kitu maalim ampigie debe abaki ikulu, Cha msingi maalim na karume watuweke wazi walijadili nini that day!
Jitahidi ujifunze uchambuzi wa mambo (analysis).

Kama unayafuatilia mambo yaliyomo katika kadhi hii ya muafaka wa CUF na CCM na pia yale yanayojitokeza baada ya kufanyika kwa mazungumzo hayo ya Karume na Maalim bila ya shaka utakuwa unayaelewa bila ya kutajwa mambo ambayo itakuwa viongozi hao wameyazungumzia na kukubaliana. CCM na CUF walikuwa katika mazungumzo ya muwafaka hapa lakini wakakwama. Tumeelezwa kule kuwa wamekubaliana mambo mengi ya msingi-lakini wakakwamishwa na jambo linalohusiana na kuundwa kwa Serikali ya mseto kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010 (Ingawa kimsingi walikuwa hawana pingamizi na kuundwa kwa Serikali ya mseto baada ya uchaguzi wa 2010). Lakini maandalizi yenyewe ya uchaguzi wa 2010 yemeingia dosari (rudia huko nyuma kadhia za uboreshaji wa daftari la kudumu na uandikishwaji wa Zan ID) Hii ni dalili inayoaashiria kutokuwepo kwa salama katika uchaguzi huo wa 2010.

Sasa kama CCM haitaki kuundwa kwa Serikali ya mseto hivi sasa (kabla ya uchaguzi wa 2010) ili kujenga msingi wa maridhiano. Kwa nini tusiache CCM na Serikali yake halali (ambayo tayari imeshatambuliwa na CUF)ikamaliza kipindi hiki hapo Oktoba 2010. Tukaahirisha uchaguzi na kupisha kipindi cha Serikali ya Mseto (CUF/CCM) kwa miaka miwili kujenga na kukamilisha misingi ya maridhiano ambayo mengi yake ni hayo yanayotokana na muafaka uliokwama wa kina Makamba/Seif. Sioni sababu za kutilia hofu dhamira za Karume/Seif-ikiwa zitakuwa zinaungwa mkono kikamilifu na vikao kama vya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na wananchi wenyewe walio wengi wa Zanzibar.

Tutarudi katika reli ya demokrasia baada ya mpito wa miaka miwili. Tutafanya uchaguzi wa haki na amani unaoridhiwa na wote. Watakaopata ridhaa -si wataongoza tu Wazanzibari walioshikamana na wanaopendana wanaoshi kwa raha na amani. Mtiririko huu si udikteta wala uroho wa madaraka, wala uvunjifu wa demokrasia. Naamini hivyo.
 

Soma vizuri nilichoandika.

Nazungumzia historia. Unataka kuniambia Seyyid Said alikuwa anajihesabu Mzanzibari? Leo tunajihesabu waafrika lakini mababu zetu hawakujihesabu hivyo. Ni wageni ndiyo waliowaita waafrika. Vile vile ni wageni ndiyo waliomuita Tippu Tib mswahili-mzanzibari wakati yeye bila shaka alijiona muarabu safi wa Oman! Kuguswa na utumwa hakuna maana kuwa waliomtangulia walikuwa watumwa peke yake.

Waarabu wengi walizaa na watumwa wao na watoto wao wakahesabiwa waarabu. Wangapi Zanzibar (waarabu, wahindi n.k.) ambao mababu zao walihusika na biashara ya utumwa? Wangapi katika nyie waarabu safi ambao wazazi wenu walikuwa na watumwa au walishiriki katika biashara hiyo? Mnataka kuniambia mashamba ya karafuu yote yalilimwa na watu huru?

Tippu Tib alikuwa na mashamba 7 na watumwa 10,000. Unataka kuniambia aliajiri watu wa kulima mashamba hayo wakati watumwa anao? Na baada ya utumwa kufutwa wote walirudishwa bara? Kupinga utumwa ni kukubali ushiriki wa waliokutangulia katika biashara hiyo ama sivyo itabaki maneno tu. Tunapozungumzia utumwa hatuzungumzii wale waliokuwa watumwa peke yao bali hata wale ambao kwa namna yeyote walishiriki katika hiyo biashara.

Amandla.........
 

Sasa hii sio pumba? Tangu lini Zanzibar ilikuwa koloni la muingereza? Haujui tofauti ya protectorate na colony? Zanzibar kama Tanganyika walikuwa chini ya utawala wa waingereza lakini hawakuwa makoloni ya uingereza.

Haujui hata asili ya vyama vyenu vya siasa? Kama wazanzibari ni wamoja kwa nini Salim Ahmed Salim alipingwa na wazanzibari wenzake? Hao mnaowaita Hizbu ni kutoka wapi? Zanzibar toka mwanzo haijawa jamii moja. Mwanzoni mlikuwa na watwana na waungwana, kabla ya uhuru mkagawanyika kikabila, chama cha weusi, chama cha waarabu n.k. Mapinduzi yalifanyika kwa msingi wa rangi. Masuala ya rangi yalichangia sana katika utawala wa Karume I. Au haujui kuwa wahindi walikimbia Zanzibar kwa kuogopa kuozeshwa kwa nguvu?

Msitufanye wote wajinga. Kwa kukataa matatizo yaliyokuwepo na misingi yake hata siku moja hapatakuwa na suluhisho la kudumu.

Amandla.....
 

Pole sana Fundi wewe ni victim wa historia potofu(iliyogubikwa guo la chuki na hitilafu za kisiasa zilizochangiwa na pande zote zilizoshiriki siasa za Zanzibar kabla ya Mapinduzi ya 1964) Fundi ni wewe usiyejua historia ya vyama vya siasa vya Zanzibar. ZNP si chama cha waarabu peke yake, na ASP si chama cha Waafrika (kwa maana ya waafrika wenye nasaba na utumwa na waliotoka sehemu za Bara nje ya Mwambao wa Mzizima, sehemu za bagamoyo na sehemu za Mwambao wa Tanga). Fundi ZNP ilipata nguvu kutokana na kuuungwa mkono na sehemu kubwa ya Wazanzibari (kindakindaki ambao si waarabu) na ASP ilipata nguvu kubwa sana tu kutokana na kuungwa mkono na Wazanzibar (kindakindaki) ambao sio wale waliotoka Bara kutokana na mtiririko wa watumwa wakina Mtipp.
 

Amandla!!!. Mzee. Hivi sijui unafikiria idadi gani ya waarabu waliingia pale Zanzibar. Sijui walikuwa na uwezo gani hao waarabu kuzaa (watoto) na watumwa wao. Hatimaye wakawa wengi wakaunda ZNP na kuweza kuwapa kashkash ASP hata katika uchaguzi. Tuyasarif ya sasa sijui kwa mantiki hiyo hiyo hao watoto wa waarabu wanaweza kuwa na uwingi wa kiasi gani wakaiwezesha CUF kuisogelea kwa karibu mno CCM katika kura za uchaguzi. Achana na kasumba hizo, tuwape nafasi Wazanzibari wa leo watafute njia za kujenga Zanzibar mpya. Hilo ni jambo lao tuwaachie wenyewe.
 
waacheni wazanzibari wafix problems zao.Kujiingiza kati kati ni kuonesha kuwa muna special interests in those islands...as it has been since Nyerere
Lakini mbona hakuna lolote lile linaloashiria kuwa juhudi za sasa hivi za maridhiano zina dalili ya kuhatarisha special interests (kama unavyofikiria wewe) za Wa-tanganyika ( kumradh- Watanzania). Au unamaana interests za Wa-tanganyika ni kuona Wazanzibari wanagombana na kuhitilafiana kila siku.
 
Msitufanye wote wajinga. Kwa kukataa matatizo yaliyokuwepo na misingi yake hata siku moja hapatakuwa na suluhisho la kudumu.

Amandla.....

Hakuna anae kataa matatizo kuwepo, tunachokataa ni kule kushabikia hilo tatizo liendelee kuwepo.Hivyo ni bora ukajiunga na hao wenye kufanya jitihada za kutatua tatizo hilo.

Nukuu:
**Au hilo tatizo lina tofauti gani na matatizo mengine yote duniani?Kenya, Rwanda, Burundi, US mbinde za mweusi na mweupe && Tanzania pia imo watu hutiana mapanga huko mitaa sijuwi Tarime....au?
**Sasa tusilifanye hili la Zanzibar kuwa ni special
 

Inawezekana kuwa wengi wa Tanganyika au specifically CCM wanaogopa tatizo hilo kutatuliwa.Hata ukitizama KP utaona ujumbe huo.

P:S
**Kumbuka Zanzibar ikiachiwa democracy ikafanya kazi yake huo ndio mwisho wa CCM kukaa madarakani.Na upande mwengine kuondoka kwa CCM madarakani Zanzibar, kunaweza kutoa ushawishi mkubwa Bara kuondolewa chama hicho au kupungua supporters.
 

Attachments

  • kpleo3.jpg
    14.1 KB · Views: 38

Kibunango, kwa vijana wa leo wanaposoma historia ya biashara ya utumwa wengi wao wanawaona weusi wa Marekani na Carribean kama ndio vielelezo vya biashara hiyo na kudhania kuwa Waarabu hawakuhusishwa sana na biashara hiyo kwani huko uarabuni hakuna weusi wengi!! Ukweli ni kwamba waarabu waliwasafirisha watumwa wengi sana kwenda uarabuni lakini wengi wao waliuawa na pia wanaume walikuwa wanahasiwa[ castrated]. Hivyo huwezi kuwaona weusi wengi arabuni waliotokana na uzao wa watumwa!!
 

Usitake kuandika historia upya. ZNP kilikuwa chama cha waarabu ikiwa na maana wafuasi wake wengi walikuwa ni waarabu au wale waliokuwa wakijihesabu waarabu na viongozi wa juu walikuwa waarabu. ZPPP kilikuwa cha washirazi na waafrika. ASP kilitokana na muungano wa chama cha washirazi na chama cha waafrika. Ingawa uchaguzi wa 1961 ulishindwa na ASP, ZPPP na ZNP viliungana na kupewa utawala. Wengi wa hao tunaowaita waarabu wana damu za waafrika weusi mara nyingi kutoka upande wa kike. Waarabu tofauti na wazungu hawakusita kuoa waafrika weusi na watoto wao walikubalika na kujihesabu kuwa ni waarabu. Waarabu hawakuoa waafrika huru peke yake bali wengine walizaa na watumwa wao wa kike. Waarabu, washirazi, wahindi n.k. hawakuanza kutembelea unguja Pwani ya Afrika ya Mashariki hivi karibuni. Miaka nenda rudi walikuwepo lakini walijihesabu tofauti na waafrika weusi na kubakiza identity yao.

Tunaposema kuwa chama fulani ni cha watu fulani haina maana watakaokipigia kura watakuwa ni watu wa kabila hilo peke yake. Zanzibar palikuwa na makabila mengine zaidi ya haya tunayozungumzia ambayo bila shaka yalipigia vyama tofauti. Vile vile kulikuwa na waafrika weusi waliokipigia ZNP na ZPPP na bila shaka kuna waarabu waliokipigia ASP. Chama cha BNP ambacho kinasema kuwa kinalinda maslahi ya watu weupe uingereza bado kina sympathisers weusi!

Baada ya mapinduzi Zanzibar na Muungano na Tanganyika, tofauti zimekuwa katika msingi ya makazi yaani kati ya wanaotoka Pemba ( ambao wengi wanahesabiwa kuwa ni waarabu) na wale wa unguja. Salim Ahmed Salim ambae sisi watu wa bara tunamuona mswahili mwenzetu huko anahesabiwa mpemba na zaidi ya hiyo muarabu.

Katika historia yao kama wanavyotaka isomeke sasa hivi, wanazungumzia waafrika waliotoka bara bila kuainisha ni wakina nani hao. Si wote waliotokea Tanga, Bagamoyo na pwani nyingine. Kama nilivyouliza kabla, watumwa waliokuwa wakitumikishwa kwenye mashamba ya karafuu walipotelea wapi? Katika miaka ya !800s, Tippu Tib peke yake alikuwa na watumwa 10,000. Mwaka 1961, idadi ya watu Zanzibar haikuzidi 400,000. Je miaka mia iliyopita palikuwa na watu wangapi Zanzibar na ni wangapi kati yao walikuwa watumwa?

Siasa na historia ya Zanzibar ilijaa chuki na uhasama wa rangi. Walianza kuchinjana hata kabla ya mapinduzi ya mwaka 1964 (Katika uchaguzi wa 1961 watu 68 waliuawa). Ndivyo ilivyokuwa upende, usipende.

Amandla...........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…