HOTUBA ya Seif Sharrif na Majibu yake kuhusu Maridhiano Zanzibar!

WAKATI vyama vya CCM na CUF vikijiandaa kuteua wajumbe wa kuunda kamati maalumu ya kuangalia mfumo wa kuundwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, vyama ‘vidogo' vya siasa kisiwani hapa vimetishia kwenda mahakamani kupinga hatua hiyo.

Katibu Mkuu wa chama cha Tadea, Juma Ali Khatib alisema "nchi hii si ya CCM na CUF, tunatakiwa kujumuishwa kwenye mchakato huo na pia kupewa vyeo kwenye serikali hiyo.

Mabadiliko yoyote katika Katiba lazima yaangalie uwepo wetu." Khatib alisema vyama hivyo vya siasa vitakutana wiki hii kupanga taratibu za kupata msaada wa kimahakama katika kuhakikisha vyama vingine vya siasa vinapata nafasi kwenye serikali hiyo ya Umoja wa Kitaifa na kuongeza "serikali hiyo pia inatakiwa ijumuishe hata vyama vya kiraia kama walemavu".

Hata hivyo, Rashid Ahmed kutoka NLD ameungana na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka Chama Cha Mapinduzi na Chama cha Wananchi wanaotaka kuundwe Serikali ya Umoja wa Kitaifa na kuunganisha Wazanzibari.

Mwenyekiti wa Chama cha Muungano wa Wakulima Tanzania (AFP), Said Soud alisema "tumeshangazwa na CUF, kunapokuwa na matatizo tunakuwa pamoja, lakini kunapotokea fursa wanatutenga, hii haikubaliki lazima wote tuwepo kwenye serikali hiyo ya mseto." Vyama vingine vilivyo kwenye kundi hilo la vyama vidogo 16 vya siasa kisiwani hapa vinavyotaka kujumuishwa kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa ni pamoja na NCCR Mageuzi, UPDP na Chadema.

Asilimia kubwa ya Wazanzibari wameunga mkono hatua ya wawakilishi kutaka kuanzishwe Serikali ya Umoja wa Kitaifa baada ya Uchaguzi Mkuu ujao. Ijumaa iliyopita, Baraza la Wawakilishi lilikubaliana kuunda kamati ya watu sita itakayofanya kazi na serikali katika kupanga namna ya kufanyika kura ya maoni ikiwa ni hatua ya kuwa na Serikali hiyo ya Umoja wa Kitaifa.

Wawakilishi hao wamependekeza Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kuendesha kura ya maoni na ikiwa matokeo yataonesha wananchi wanataka serikali hiyo ya umoja wa kitaifa, hatua itakayofuata ni kufanya mabadiliko ya Katiba kuruhusu kuwepo kwa serikali hiyo.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa ZEC, Salum Ali Said alisema Tume yake itaendesha kura hiyo ya maoni, lakini akasema kuwa kupatikane fedha za kutosha kwa ajili ya kufanyika kampeni ili watu waelewe kabla ya maoni hayo kukusanywa.

Ikiwa tutataarifiwa kuandaa kuchukua maoni ya wananchi, tutahitaji si chini ya bilioni mbili kwa ajili ya shughuli hiyo," alisema Said.

Source Habari Leo

Ijapokuwa mie naisupport hii hoja ya serikali ya mseto ila hawa akina soud na Juma khatibu haiwaitakii mema zanzibar.

Kabla hata serikali ya mseto haijaanza wanaanza lawama watu wengine sijui vipi kwani wao wakifanya jitihada wakapata kwanza hao wawakilishi ndipo wakaja katika uwakilishi katika serikali hawaoni wangelifanya la maana. Mtu unalilia representatio serikalini huna hata mwakilishi mmoja bungeni.

Either jamaa ni mamluki au basi tu wanataka madaraka wasiyoyatolea jasho
 
Good sasa kaa chini tukupe historia ya Jaws Corner na Barza, Jaws Corner imetokana na movie inaitwa American Jaws iliyotoka mwaka 1974. Hizi baraza mbili zilikuwa maarufu kwa vijana ambao baba zao au mama zao walikuwa wametokea katika chama kinachoitwa ZNP. Kutokana na ubaguzi wa wazee wao kuwa wanachama wa ZNP vijana walikuwa wakinyimwa kazi, kusoma, kubaguliwa, kubakwa na hivyo basi kukawa na population kubwa ya vijana wana dukuduku miyoni mwao ikawa cinema na vijiwe ndio sehemu ya kupast time kupoteza yale machungu yao dhidi ya serikali.
Sidhani kama kuna sinema iliyoitwa American Jaws. Hata kimsamiati wa kiingereza title hiyo haina maana. Labda kama unazungumzia Jaws ambayo ilikuwa sinema inayohusu papa mla watu! ZNP kilikuwa chama kilichoongozwa na kukubalika zaidi na waarabu. Kwa hiyo unataka kutuambia kuwa Jaws Corner ni sehemu ya waislamu,waarabu na washiriki wao? Mahali ambapo wakristu hawajisikii huru kufika kutokana na hao wanaokuweko Jaws bado wanakumbuka waliyofanyiwa babu zao na wanawalaumu wakristu kwa hilo? H

Barza watu wengine waliokuwa hapo walikuwa ni watu wakifuatilia sasa mambo ya political movement marekani. Wakawa kila mmoja anajiita brother etc. Jaws corner vilevile sasa kwakuwa serikali adhimu ya CCM ilikuwa haiyapendi haya ikawa inawapiga vita sana waliokuwa wakikaa baraza hizi kubwa mbili. Wengine walifungwa, wengine waliuwawa, wengine walikimbia znz kuja kuishi dar kwasababu walikuwa wanaonekana wataipindua serikali.
Kwa hiyo pamoja na kuwa wao asili yao ilikuwa ni kwenye chama kilichohesabiwa cha kiarabu, influence kubwa kwao ilikuwa kutoka Civil Right Movement ya marekani? Kuitana brother na pengine kuweka Afro ndiko kuliwafanya revolutionaries? Na hao waliokimbia Dar kukwepa serikali dhalimu ya Zanzibar kwa nini hawakushikwa na kurudishwa Zanzibar maana waasisi wa maovu yote Zanzibar walikuwa wanaishi Dar na kuongoza serikali ya JMT? Hawa ambao walionekana wanataka kuipindua SMZ walipata hifadhi kwa yule ambaye ndiye alikuwa anaisukumiza SMZ iwatendee maovu! Hauoni unavyojichanganya?

Tuje sasa kwa wakiristo kwanza wakiristo wengi if not all (kwasababu sina statistics) walikuwa chini ya ASP. na walishiriki kikamilifu katika mapinduzi. Sasa katika mapinduzi watu wengi waliumia ndani ya mapinduzi hayo walikuwa ni wanachama wa ZNP ambapo wengi wao waliuliwa, kubakwa, kutekwa. Sasa wewe kwa akili yako unadhani kama baba yako alifanya mambo haya kwa jirani yako utakaa naye kweli meza moja mkanywa kahawa???? Bongo tu hapa wale watoto wa vigogo wana club zao za kujichanganya na akina walalahoi nao pia wana club zao.


Hawa wakristu ndiyo peke yao walioshiriki kwenye mapinduzi Zanzibar? Kama ni hivyo mbona hawakuonekana katika serikali iliyofuata. Na kweli unataka kutuambia leo miaka zaidi ya 40 baada ya wao kufanya maasi hayo bado wanaogopa kufika Jaws Corner maana wanajua watakiona cha mtema kuni? Halafu hao hao ndiyo unaosema watajiunga katika mapinduzi yatakayoongozwa na hao hao vijana wa Jaws Corner kwa vile wao ni wazanzibari? Watashirikiana kuikabidhi nchi kwa wale ambao kuna uwezekano mkubwa wa kulipiza yale waliofanyiwa waliowatangulia wakati wa mapinduzi! Iko kazi.

Ninavyojua mimi Jaws Corner ni public space na siyo club. Sasa itakuwaje kuwa raia wa Zanzibar aogope kufika hapo kutokana na dini yake kuhusishwa na maovu yaliyofanyika hata kabla yeye kuzaliwa? Na leo ndio unatuambia kuwa yale mapinduzi yalikuwa ya kidini ambapo wakristu weusi waliwaua, kuwabaka na kuwatendea maovu waislamu safi wa kiarabu na washiriki wao! Kama hii ni kweli basi kwa nini hizo nafasi za juu wasishike wao maana kama alivyosema Mao,"nguvu inatokana na mtutu wa bunduki"? Au muda wote huu wameishika nchi, wakivuta nyuzi kwa nyuma? Hii ndio historia mnayofundishana Jaws! Bila aibu mnaandika upya historia kama vile watu hawakushuhudia.

Niliwahi kuuliza hapo, "hivi kwa nini hamtaki kujiuliza hiyo chuki kiasi hicho dhidi ya waarabu na washiriki wao ilitokana na nini?
" Kama walikuwa wanafaidi maziwa ya bure kwa nini waliamka siku moja na kuwatendea maovu kiasi hicho hao wanaowapa hayo maziwa? Maziwa ya bure hayawezi kubadili utu wa binadamu. Bila shaka wafungwa waliopo Guatanamo wanakula vizuri na bure kuliko ndugu zao walioko Afghanistan, Yemen na kwengineko. Kwa mantik yenu, basi Guatanamo ni peponi!

Ukweli ni kuwa uovu mkubwa ulifanywa dhidi ya weusi waliokuwa wakiishi Zanzibar. Utu wao ulidhalilishwa na walionekana si watu mbele ya wale wenye rangi nyeupe. Haya haya tuliyaona Rwanda ambako pamoja na kuwa wa.hutu walifanya unyama mkubwa dhidi ya watutsi lakini ukiangalia historia yao, vitendo hivyo vilichangiwa na chuki iliyotokana na vitendo vya watutsi dhidi ya wahutu.

Unadai mama na baba yako wote ni watu wa bara, lakini wazee wako wengine (ambao natumai ni ndugu wa baba yako au mama yako) ni watu wa Zanzibar! Mbona haijakaa vizuri?
Hata hivyo, inatosha.

F.y.i. historia haipatikani kijiweni peke yake. Inabidi uingie kwenye mtandao, maktaba au kwenye archive ili uthibitishe yale uliyoyasikia mahali kama Jaws Corner.

Nilikuwepo.

Amandla..........
 
Sidhani kama kuna sinema iliyoitwa American Jaws. Hata kimsamiati wa kiingereza title hiyo haina maana. Labda kama unazungumzia Jaws ambayo ilikuwa sinema inayohusu papa mla watu! ZNP kilikuwa chama kilichoongozwa na kukubalika zaidi na waarabu. Kwa hiyo unataka kutuambia kuwa Jaws Corner ni sehemu ya waislamu,waarabu na washiriki wao? Mahali ambapo wakristu hawajisikii huru kufika kutokana na hao wanaokuweko Jaws bado wanakumbuka waliyofanyiwa babu zao na wanawalaumu wakristu kwa hilo? H

Kwa hiyo pamoja na kuwa wao asili yao ilikuwa ni kwenye chama kilichohesabiwa cha kiarabu, influence kubwa kwao ilikuwa kutoka Civil Right Movement ya marekani? Kuitana brother na pengine kuweka Afro ndiko kuliwafanya revolutionaries? Na hao waliokimbia Dar kukwepa serikali dhalimu ya Zanzibar kwa nini hawakushikwa na kurudishwa Zanzibar maana waasisi wa maovu yote Zanzibar walikuwa wanaishi Dar na kuongoza serikali ya JMT? Hawa ambao walionekana wanataka kuipindua SMZ walipata hifadhi kwa yule ambaye ndiye alikuwa anaisukumiza SMZ iwatendee maovu! Hauoni unavyojichanganya?



Hawa wakristu ndiyo peke yao walioshiriki kwenye mapinduzi Zanzibar? Kama ni hivyo mbona hawakuonekana katika serikali iliyofuata. Na kweli unataka kutuambia leo miaka zaidi ya 40 baada ya wao kufanya maasi hayo bado wanaogopa kufika Jaws Corner maana wanajua watakiona cha mtema kuni? Halafu hao hao ndiyo unaosema watajiunga katika mapinduzi yatakayoongozwa na hao hao vijana wa Jaws Corner kwa vile wao ni wazanzibari? Watashirikiana kuikabidhi nchi kwa wale ambao kuna uwezekano mkubwa wa kulipiza yale waliofanyiwa waliowatangulia wakati wa mapinduzi! Iko kazi.

Ninavyojua mimi Jaws Corner ni public space na siyo club. Sasa itakuwaje kuwa raia wa Zanzibar aogope kufika hapo kutokana na dini yake kuhusishwa na maovu yaliyofanyika hata kabla yeye kuzaliwa? Na leo ndio unatuambia kuwa yale mapinduzi yalikuwa ya kidini ambapo wakristu weusi waliwaua, kuwabaka na kuwatendea maovu waislamu safi wa kiarabu na washiriki wao! Kama hii ni kweli basi kwa nini hizo nafasi za juu wasishike wao maana kama alivyosema Mao,"nguvu inatokana na mtutu wa bunduki"? Au muda wote huu wameishika nchi, wakivuta nyuzi kwa nyuma? Hii ndio historia mnayofundishana Jaws! Bila aibu mnaandika upya historia kama vile watu hawakushuhudia.

Niliwahi kuuliza hapo, "hivi kwa nini hamtaki kujiuliza hiyo chuki kiasi hicho dhidi ya waarabu na washiriki wao ilitokana na nini?
" Kama walikuwa wanafaidi maziwa ya bure kwa nini waliamka siku moja na kuwatendea maovu kiasi hicho hao wanaowapa hayo maziwa? Maziwa ya bure hayawezi kubadili utu wa binadamu. Bila shaka wafungwa waliopo Guatanamo wanakula vizuri na bure kuliko ndugu zao walioko Afghanistan, Yemen na kwengineko. Kwa mantik yenu, basi Guatanamo ni peponi!

Ukweli ni kuwa uovu mkubwa ulifanywa dhidi ya weusi waliokuwa wakiishi Zanzibar. Utu wao ulidhalilishwa na walionekana si watu mbele ya wale wenye rangi nyeupe. Haya haya tuliyaona Rwanda ambako pamoja na kuwa wa.hutu walifanya unyama mkubwa dhidi ya watutsi lakini ukiangalia historia yao, vitendo hivyo vilichangiwa na chuki iliyotokana na vitendo vya watutsi dhidi ya wahutu.

Unadai mama na baba yako wote ni watu wa bara, lakini wazee wako wengine (ambao natumai ni ndugu wa baba yako au mama yako) ni watu wa Zanzibar! Mbona haijakaa vizuri?
Hata hivyo, inatosha.

F.y.i. historia haipatikani kijiweni peke yake. Inabidi uingie kwenye mtandao, maktaba au kwenye archive ili uthibitishe yale uliyoyasikia mahali kama Jaws Corner.

Nilikuwepo.

Amandla..........

Cinema ya Jaws iliyotoka mwaka 1974 ilitengenezwa wapi mbona unazungumza pumba?

Pili kusoma historia kwenye internet ni uchache wa elimu kwani internet ni pana na can be misleading as well. Hii inajidhihirisha uchache wa elimu ulionao.

Tatu Jaws corner ni kijiwe kama umenisoma vizuri lakini kaa ukifahamu ni akina nani walikuwa wanakaa pale ni watu ambao hadi leo hupita kukaa pale magharibi.

Nne Chuki ya waarabu ilijengwa na unafiki wa Waingereza wapate kututawala vizuri maana ndio hulka yao (na hili mie ndio naona balaa kubwa lililowahi kutokea katika historia ya zanzibar). Katugawa kimatabaka tukagawika hadi leo na hadi kesho kama hatujakuwa makini.

Tano kama hukubaliani na historia ya Jaws corner tupe wewe historia yake kama una nyengine!!!!

Ciao
 
Sidhani kama kuna sinema iliyoitwa American Jaws. Hata kimsamiati wa kiingereza title hiyo haina maana. Labda kama unazungumzia Jaws ambayo ilikuwa sinema inayohusu papa mla watu! ZNP kilikuwa chama kilichoongozwa na kukubalika zaidi na waarabu. Kwa hiyo unataka kutuambia kuwa Jaws Corner ni sehemu ya waislamu,waarabu na washiriki wao? Mahali ambapo wakristu hawajisikii huru kufika kutokana na hao wanaokuweko Jaws bado wanakumbuka waliyofanyiwa babu zao na wanawalaumu wakristu kwa hilo? H

Kwa hiyo pamoja na kuwa wao asili yao ilikuwa ni kwenye chama kilichohesabiwa cha kiarabu, influence kubwa kwao ilikuwa kutoka Civil Right Movement ya marekani? Kuitana brother na pengine kuweka Afro ndiko kuliwafanya revolutionaries? Na hao waliokimbia Dar kukwepa serikali dhalimu ya Zanzibar kwa nini hawakushikwa na kurudishwa Zanzibar maana waasisi wa maovu yote Zanzibar walikuwa wanaishi Dar na kuongoza serikali ya JMT? Hawa ambao walionekana wanataka kuipindua SMZ walipata hifadhi kwa yule ambaye ndiye alikuwa anaisukumiza SMZ iwatendee maovu! Hauoni unavyojichanganya?



Hawa wakristu ndiyo peke yao walioshiriki kwenye mapinduzi Zanzibar? Kama ni hivyo mbona hawakuonekana katika serikali iliyofuata. Na kweli unataka kutuambia leo miaka zaidi ya 40 baada ya wao kufanya maasi hayo bado wanaogopa kufika Jaws Corner maana wanajua watakiona cha mtema kuni? Halafu hao hao ndiyo unaosema watajiunga katika mapinduzi yatakayoongozwa na hao hao vijana wa Jaws Corner kwa vile wao ni wazanzibari? Watashirikiana kuikabidhi nchi kwa wale ambao kuna uwezekano mkubwa wa kulipiza yale waliofanyiwa waliowatangulia wakati wa mapinduzi! Iko kazi.

Ninavyojua mimi Jaws Corner ni public space na siyo club. Sasa itakuwaje kuwa raia wa Zanzibar aogope kufika hapo kutokana na dini yake kuhusishwa na maovu yaliyofanyika hata kabla yeye kuzaliwa? Na leo ndio unatuambia kuwa yale mapinduzi yalikuwa ya kidini ambapo wakristu weusi waliwaua, kuwabaka na kuwatendea maovu waislamu safi wa kiarabu na washiriki wao! Kama hii ni kweli basi kwa nini hizo nafasi za juu wasishike wao maana kama alivyosema Mao,"nguvu inatokana na mtutu wa bunduki"? Au muda wote huu wameishika nchi, wakivuta nyuzi kwa nyuma? Hii ndio historia mnayofundishana Jaws! Bila aibu mnaandika upya historia kama vile watu hawakushuhudia.

Niliwahi kuuliza hapo, "hivi kwa nini hamtaki kujiuliza hiyo chuki kiasi hicho dhidi ya waarabu na washiriki wao ilitokana na nini?
" Kama walikuwa wanafaidi maziwa ya bure kwa nini waliamka siku moja na kuwatendea maovu kiasi hicho hao wanaowapa hayo maziwa? Maziwa ya bure hayawezi kubadili utu wa binadamu. Bila shaka wafungwa waliopo Guatanamo wanakula vizuri na bure kuliko ndugu zao walioko Afghanistan, Yemen na kwengineko. Kwa mantik yenu, basi Guatanamo ni peponi!

Ukweli ni kuwa uovu mkubwa ulifanywa dhidi ya weusi waliokuwa wakiishi Zanzibar. Utu wao ulidhalilishwa na walionekana si watu mbele ya wale wenye rangi nyeupe. Haya haya tuliyaona Rwanda ambako pamoja na kuwa wa.hutu walifanya unyama mkubwa dhidi ya watutsi lakini ukiangalia historia yao, vitendo hivyo vilichangiwa na chuki iliyotokana na vitendo vya watutsi dhidi ya wahutu.

Unadai mama na baba yako wote ni watu wa bara, lakini wazee wako wengine (ambao natumai ni ndugu wa baba yako au mama yako) ni watu wa Zanzibar! Mbona haijakaa vizuri?
Hata hivyo, inatosha.

F.y.i. historia haipatikani kijiweni peke yake. Inabidi uingie kwenye mtandao, maktaba au kwenye archive ili uthibitishe yale uliyoyasikia mahali kama Jaws Corner.

Nilikuwepo.

Amandla..........

Tupe statistics ni waislamu wangapi walishiriki kuikomboa zanzibar kwa hao unaowaita waarabu???? Pili waliokimbilia dar walikimbia zanzibar kwasababu ya maovu yaliyokuwa yakifanywa na serikali ya SMZ (aka visasi), akina marehemu mshangama, abood maalim na wengineo waliona ni vema waje kuishi dar wakaendeleza maisha yao kwani zanzibar wangeliuwawa. Na dar walienda kwanza kwasababu dar nguvu ya ubaguzi ilikuwa ndogo, pili walipokuwa dar ufanisi wao kwa kuendeleza changamoto ungelikuwa mdogo. Kumbuka enzi hizo telephone ni telegram, simu za kutafuta, usafiri wa majahazi hivyo basi wakaja kuishi dar wengine wakawa hadi mawaziri muungano.

Dar kumbuka kipindi hicho ilikuwa almost 99.9% walikuwa ni waislamu kwa taarifa yako.
 
Tupe statistics ni waislamu wangapi walishiriki kuikomboa zanzibar kwa hao unaowaita waarabu???? Pili waliokimbilia dar walikimbia zanzibar kwasababu ya maovu yaliyokuwa yakifanywa na serikali ya SMZ (aka visasi), akina marehemu mshangama, abood maalim na wengineo waliona ni vema waje kuishi dar wakaendeleza maisha yao kwani zanzibar wangeliuwawa. Na dar walienda kwanza kwasababu dar nguvu ya ubaguzi ilikuwa ndogo, pili walipokuwa dar ufanisi wao kwa kuendeleza changamoto ungelikuwa mdogo. Kumbuka enzi hizo telephone ni telegram, simu za kutafuta, usafiri wa majahazi hivyo basi wakaja kuishi dar wengine wakawa hadi mawaziri muungano.

Dar kumbuka kipindi hicho ilikuwa almost 99.9% walikuwa ni waislamu kwa taarifa yako.

Unataka kutuambia kuwa hakuna muislamu aliyeshiriki katika hayo mapinduzi? Waliopindua serikali ni John Okello na wakristu wenzake peke yao! Unaamini kweli hivyo?

Niambie hiyo filamu ya American Jaws nani alikuwa starring na ilihusu nini? Kwa vile haujui kiingereza hauoni hata namna hilo jina American Jaws halina mantik.

Filamu inayoitwa Jaws, director wake alikuwa Steven Spielberg na stars walikuwa Roy Scheider, Richard Dreyfuss n.k. Plot ilihusu papa mla watu aliyetishia usalama wa kakisiwa cha Amity. Google Jaws utapata taarifa zaidi.

Sasa wewe, tufahamishe hiyo filamu ya American Jaws, nani alikuw adirector, nani waliicheza na ilihusu nini! Wakati pekee ambapo asilimia kubwa kiasi hicho cha waislamu walikuwepo Dar es Salaam labda ni wakati wa Seyyid Majid. Hiyo unayoijua kama Dar es Salaam imejengwa palipokuwa kakijiji kilichoitwa Mzizima. Ingawa bila shaka waislamu walikuwepo kijijini hapo lakini hawakuwa peke yao maana watu wengi waliamani zaidi imani zao kuliko hizi za kuletewa. Dar es Salaam iliendelezwa na wajerumani baada ya kifo cha Seyyid Majid. Kanisa la kwanza lilijengwa Kigamboni na baadae hayo ya Saint Joseph na Azania Front. Wakati wa wajerumani na waingereza watu wengi waliingia kutoka bara (ambao walikuwa wakristu, wasio na dini na waislamu)na vile vile palikuwa na idadi kubwa ya wahindi. Haiwezekani kabisa baada ya yote haya waislamu wawe zaidi ya asilimia 99! Ndiyo maana nakwambia hiyo elimu uliyoipata jaws corner ina walakin.

Naona ni kujipotezea muda kuendeleza majadiliano na mtu kama wewe. Hautakuja kuelewa maana basic education yako ina walakin. Sitakujibu tena.

Nilikuwepo.

Amandla.....
 
Back
Top Bottom