Hotuba ya rais Kikwete ya kufunga mwaka 2010

Hotuba ya rais Kikwete ya kufunga mwaka 2010

:whoo:kilio changu ni kwenye hili swala la dowans mbona hajagusia kuna nini kama sio na yeye kuwa mhusika,au ndon yale aliyoyasema Hosea kwa wakubwa kwamba anawalinda mafisadi
 
mkwere ujumbe wangu kwa mwaka huu 2011 nakuchukia na haufai na sijivunii kua na rais kama wewe. Mungu akulaani kwa adha na tabu unazo wasababishia wa tz kwa uozo wa uongozi wako.
 
The so called pumba ambazo zimepamba sana vyombo vya habari hivi karibuni ilikuwa ni kwa sababu ya lager, umbumbumbu au kujipendekeza kupita kiasi?
 
Again from CHOMA CHA NKOLA to all wana JF, Happy New Year 2011 to all of U!
 
Mimi nijuavyo Jakaya Kikwete hana cha kupoteza. Kwa hiyo hicho nilikitarajia.
 
ht mimi cjasikia na ndilo lilikuwa kubwa la kuzungumzia pia
 
Ngnjera, ngonjera hatutaki tena tunataka vitendo. Nani ana muda wa kusoma kurasa zote hizo na kibatari. Washauri wake hawajui tuko gizani? au tusome saa za kazi. JK NAKUCHUKIA.
 
Jamani..jamani... jamani...Huyu mtu mimi simtambui kama rais wa Tz....lakini hata kwa hao mapimbi wanaomtambua mbona hajawaelezea kusu Dowans na hizo gharama mpya za umeme?
 
Sasa Jaji Werema wakati anatoa maoni yake kuhusu katiba alikuwa ame base wapi? au alikuwa hajui ofisi yake imemshauri nini Rais? au Ikulu imeamua nini kuhusu ushauri alioutoa? Sielewi vizuri haya mambo yanavyokwenda
  1. Celina Kombani -- Serikali haina pesa wala bajeti ya kuandaa katiba mpya
  2. PM Pinda: Serikali inalipokea swala la katiba mpya, italifanyia kazi kwa kumshauri Rais
  3. AG Werema: Katiba mpya hapana, tuweke viraka kwenye hii iliyopo kama ni lazima
  4. President: Anakubali katiba mpya ni muhimu, na ataunda tume kushughulikia hilo
Haya yote ni ndani ya siku 60 baada ya uchaguzi.
Simple hayo ni matokeo ya kuwa na serikali ya kishkaji.
Enzi za mwalimu kujiunga na chama ni lazima usome itikadi ya chama kwa miezi mitatu ukitoka hapo umeiva na unakuwa unaifahamu vyema itikadi ya chama chako.
Siku hizi tunapata wanachama sokoni na hata baa matokeo ya mziki huo ndio haya.
Kuna wakati viongozi wanasahau kwamba hakuna aliyejuu ya sheria kwa mujibu wa katiba iliyopo na ambayo wameahidi kuilinda.
Na pia hawajui hata namna ya kutekeleza kiapo na maana yake.
 
Pamoja na vyombo vya habari, CDM, JAMII FORUMS imetoa mchango mkubwa sana katika kupeleka kilio cha katiba mpya kwa KIKWETE. Hongera sana wana JF kwa michango yenu na hoja zenye nguvu. Tusichoke, tuendelee kufuatilia ahadi hii ya Kikwete, ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa maoni ni nini kiwekwe kwenye katiba yetu mpya ijayo. Nina uhakika hiyo tume itakayoundwa itakuwa inatembelea jamvi letu kupata maoni yetu.
 
[FONT=Palatino Linotype, serif]Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru

[/FONT]​
[FONT=Palatino Linotype, serif]Mwaka mpya tunaouanza usiku wa leo una umuhimu wa kipekee katika uhai na historia ya nchi yetu. Tarehe 9 Desemba 2011 nchi yetu itatimiza miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara. Haya si mafanikio madogo hata kidogo. Ni mafanikio makubwa sana ambayo hatuna budi kuyafurahia na kuyasherekea kwa uzito unaostahili. [/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Katika miaka 50 ya Uhuru wetu tumefanya mambo mengi mazuri ya kujivunia katika nyanja mbalimbali. Tumedumisha uhuru na umoja wa nchi yetu. Kwa hakika hali yetu ilivyo leo kisiasa, kiutamaduni, kiuchumi, kijamii, kiusalama na kimaendeleo kwa jumla, ni tofauti sana na hali ilivyokuwa wakati Tanzania Bara inapata uhuru wake tarehe 9 Desemba, 1961. Natambua pia kwamba katika miaka 50 hii, nchi yetu na watu wake wamekumbana na kukabili changamoto nyingi. Zipo nyingi tulizoziweza na zipo ambazo tunaendelea kuzikabili na tunayo mipango thabiti ya kuhakikisha tunafanikiwa.[/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Kwa kutambua umuhimu wa aina yake wa maadhimisho ya mwaka huu ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2011, tumekubaliana na viongozi wenzangu Serikalini kuwa tusherehekee siku hiyo kwa uzito unaostahili. [/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Ndugu Wananchi;[/FONT]
[FONT=Palatino Linotype, serif]Tumekubaliana pia, tufanye mambo manne muhimu katika maadhimisho hayo. [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]Kwanza,[/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif] nautangaza mwaka 2011 kuwa ni Mwaka wa Maadhimisho ya Miaka Hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara. Kilele chake kitakuwa tarehe 9 Desemba, 2011 ambapo kutafanyika sherehe kubwa na za aina yake nchi nzima ambapo wananchi watashirikishwa kwa ukamilifu. [/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Pili,[/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif] tufanye tathmini ya kina ya mafanikio tuliyoyapata, katika juhudi zetu za kujiletea maendeleo katika miaka hamsini hii. Kila Wizara, idara na taasisi za Serikali na hata sekta binafsi zifanye tathmini ya eneo lake. Tathmini hizo ziandikwe katika vitabu ili kuhifadhi kumbukumbu hizo muhimu kwetu na kwa vizazi vijavyo. Vitabu na nyaraka hizo vitakuwa kumbukumbu zenye manufaa makubwa kwa wenzetu watakaokuwepo mwaka 2061 wakati wa kusherehekea miaka [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]100[/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif] ya Uhuru wa Tanzania Bara. Itarahisisha kazi yao ya kufanya tathmini wakati huo. [/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Tatu,[/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif] kwamba yafanyike maonyesho maalum katika Uwanja wa Maonyesho wa Julius Nyerere hapa Dar es Salaam na kote mikoani kwenye viwanja vya maonyesho, kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali katika miaka 50 tangu Uhuru wa Tanzania Bara.[/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Ndugu Wananchi;[/FONT]
[FONT=Palatino Linotype, serif]Jambo la [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]nne [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]ambalo tulilokubaliana kufanya ni kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya Nchi yetu kwa lengo la kuihuisha ili hatimaye tuwe na Katiba inayoendana na taifa lenye umri wa nusu karne. Katiba yetu ya sasa tuliyoachiwa na waasisi wa taifa letu, imeifanyia nchi yetu mambo mengi mazuri na kuifikisha Tanzania na Watanzania hapa tulipo. Tunayo nchi moja huru, ya kidemokrasia na inayoendesha mambo yake kwa kuzingatia utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu na mgawanyo wa madaraka miongoni mwa mihimili mikuu ya dola. Nchi yenye amani, utulivu na watu wake ni wamoja, wanaopendana na kushirikiana na maendeleo yanazidi kupatikana. [/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Pamoja na hayo, mwaka 2011, nchi yetu inatimiza miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara, miaka 47 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar na miaka 47 ya Muungano wa nchi zetu mbili. Yapo mabadiliko mengi yaliyotokea katika nyanja mbalimbali za maisha ya nchi yetu na watu wake katika kipindi hiki. Kwa ajili hiyo ni vyema kuwa na Katiba inayoendana na mabadiliko na matakwa na hali ya sasa. Katiba ambayo italipeleka taifa letu miaka 50 ijayo kwa salama, amani, umoja na kuwepo maendeleo makubwa zaidi.[/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Ndugu Wananchi;[/FONT]
[FONT=Palatino Linotype, serif]Ndiyo maana tukaamua kuanzisha mchakato huu na kwa ajili hiyo, nimeamua kuunda Tume maalum ya Katiba, yaani [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]Constitutional Review Commission. [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]Tume hiyo [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]itakayoongozwa na Mwanasheria aliyebobea, itakuwa na wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali katika jamii yetu kutoka pande zetu mbili za Muungano. Jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato utakaowashirikisha wananchi wote bila kubagua, vyama vya siasa, wanasiasa, wafanyabiashara, asasi za kiraia, mashirika ya dini, wanataaluma na makundi mbalimbali ya watu wa nchi yetu kote nchini, katika kutoa maoni yao juu ya wayatakayo kuhusu Katiba ya nchi yao.[/FONT]

WanaJF,
Hii kidogo ni nje ya mada ila nimeshindwa kuvumilia.
Tizama hizo red highlights.

Mimi nilifikiri uchakachuaji uko kwenye kura tu.
Mkuu wa nchi, amelisahau jina la nchi iliyopata uhuru. Angesema mara moja tungechukulia mwandishi wa hotuba alisahau.
Basi mkuu anachakachua hata jina la nchi? Jina la sehemu ya upande huu wa muungano.

Mbona sehemu ya upande wa pili ameiita kwa jina lake..tizama zambarau highlight

Je hivi ndivyo tunavyowafundisha watoto wetu historia ya nchi yetu huko mashuleni? Jee tunawatendea haki?
 
Pamoja na vyombo vya habari, CDM, JAMII FORUMS imetoa mchango mkubwa sana katika kupeleka kilio cha katiba mpya kwa KIKWETE. Hongera sana wana JF kwa michango yenu na hoja zenye nguvu. Tusichoke, tuendelee kufuatilia ahadi hii ya Kikwete, ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa maoni ni nini kiwekwe kwenye katiba yetu mpya ijayo. Nina uhakika hiyo tume itakayoundwa itakuwa inatembelea jamvi letu kupata maoni yetu.


shame to yoy jaji werema.....umeaibisha wanasheria wenzako kwa kuikataa hoja ambayo iko wazi.........sasa kwa kuwa ulimshauri rais akatae katiba mpya na rais kwa kupima upepo mzito akaamua kufuata maoni ya wapinzani ...ni wazi badala ya kufuata mizizi ya sheria unajipendekeza sana.....ni aajabu ulipandaje hadi kuwa jaji.....jaji warema resign now!!!!!!

jk ni wazi ameona wimbi linalotaka mabadiliko ni kubwa!!!
 
shame to yoy jaji werema.....umeaibisha wanasheria wenzako kwa kuikataa hoja ambayo iko wazi.........sasa kwa kuwa ulimshauri rais akatae katiba mpya na rais kwa kupima upepo mzito akaamua kufuata maoni ya wapinzani ...ni wazi badala ya kufuata mizizi ya sheria unajipendekeza sana.....ni aajabu ulipandaje hadi kuwa jaji.....jaji warema resign now!!!!!!

jk ni wazi ameona wimbi linalotaka mabadiliko ni kubwa!!!
hapa jk kwa mjanja ktuzuga tena ili watu wasizungumzie dowans....katiba kulikuwa hakuna njia ya kuepuka........mbona hakuzungumzia dowans?
 
Wewe una matatizo maana sidhani kama hii speech ni mbovu.

Mdondoaji, ushabiki uskutie upofu! Nipe majibu yafuatayo ili ujue ubovu wa speech yako, Ivi wawezaje zungumzia wizi wa pembejeo usingumzie wizi wa Dowans, Epa nk! Kwa akili yako n kweli inflation imeshuka kama alivyosema?
 
Rais Kikwete :Hotuba ya Mwaka Mpya 2011 kwa wananchi wa Tanzania
 
Last edited by a moderator:
Kauri ya Rais ni ya mwisho, Werema na Celina hawakuwa makini kwa kutokuangalia hali halisi na hivyo hawana sifa ya kiongozi bora. They lack "vision"
 
Kikwete ameongea pumba tupu. Hata katiba sijaona bado. Kwa nini yeye aseme ndo atateua constitutional review commission? Na si kufanywa na bunge? atateua washikaji zake na at the end of the day, CCM ndo watakuwa favoured. Nadhani mnyika alikuwa sawa aliposema anataka ili jambo lifanywe na chombo cha kutunga sheria yaani bunge ndo libebe dhamana yote ya mchakato wa katiba mpya na si rais(kama nilimuelewa vizuri mnyika)
 
Back
Top Bottom