Hotuba ya Mo Simba day nini maoni yako

Hotuba ya Mo Simba day nini maoni yako

Rico redi

Senior Member
Joined
Jul 15, 2023
Posts
166
Reaction score
348
Hotuba ya jana ilikua ni kama inataka kufikisha ujumbe kuhusiana na hali halisi ya kinachoendelea pale unyamani

Kwa anayefahamu Kwa mujibu wa katiba ya simba muundo wa kimamlaka uko vipi upande wa mwekezaji na wanachama je budget ikitangazwa ni kila upande unachangia au upande wa mwekezaji tu

Nani anapaswa kua decision maker wa mwisho SSC ni mwenyekiti wa bodi au mwenyekiti wa klabu au mwekezaji mwenyewe

Transformation imeanza toka mwaka 2017 mpaka leo ni kipi haswa kinachokwamisha mchakato huu kukamilika

Kwanini usajili wa wanachama hauendelei upande wa wanachama

Status ya mo pale klabuni wakati huu ambapo Bado transformation haijakamilika ni ipi mfadhili au mwekezaji

Maswali ni mengi

SIMBA NGUVU MOJA
 
Mchakato unachelewa kwa sababu ya maslahi na urasimu wa kisheria kutoka serikalini na klabuni kwenyewe.
 
Seriksli mtailaumu bure maana imeshapitisha Katiba ya Simba. Changamoto iliyopo ni Mo kutaka awe mwekezaji peke yake wakati Katiba inataka wawekezaji 3.
Uko sawa kisheria, lakini tuongee ukweli wa soko la Bongo. Ni mfanyabiashara gani mwingine mwenye akili timamu atakayeingiza mabilioni yake Simba akubali kuwa mwekezaji wa pili au wa tatu chini ya Mo?
 
Uko sawa kisheria, lakini tuongee ukweli wa soko la Bongo. Ni mfanyabiashara gani mwingine mwenye akili timamu atakayeingiza mabilioni yake Simba akubali kuwa mwekezaji wa pili au wa tatu chini ya Mo?
Wakishaanza mchakato ndio tutajua kama wapo au hawapo.
Azam alipotangaza kuingia mkatabawa tv kwa Simba na yanga wa miaka 10 na kulipa bilioni 10 mo alipinga na kusema brand ya Simba ni kubwa kuliko yanga. Baadae Simbawalichukua pesa kimyakimya.
Kama bilioni 40 kwa miaka 10 ni ndogo hixo bilioni zake 30 zinalingana na thamani ya Simba?
 
Wakishaanza mchakato ndio tutajua kama wapo au hawapo.
Azam alipotangaza kuingia mkatabawa tv kwa Simba na yanga wa miaka 10 na kulipa bilioni 10 mo alipinga na kusema brand ya Simba ni kubwa kuliko yanga. Baadae Simbawalichukua pesa kimyakimya.
Kama bilioni 40 kwa miaka 10 ni ndogo hixo bilioni zake 30 zinalingana na thamani ya Simba?
Unachofeli ni kulinganisha mkataba wa biashara na kununua hisa. Bilioni 40 za Azam ni za kuonyesha mechi kwa miaka 10, hiyo ni biashara ya haki za TV, sio kwamba Azam wameingia kumiliki klabu. Mo anatoa Bilioni 20 plus ruzuku za kila mwaka kwa ajili ya kununua 49% tu ya hisa. Hata mkileta hao wawekezaji wengine watatu, hisa zao hazitazidi hiyo 49%. So, unataka Mo atoe bilioni 100 kwa hisa zisizompa maamuzi kamili? Thamani ya Simba ipo juu, lakini hisa zina kikomo chake.
 
Unachofeli ni kulinganisha mkataba wa biashara na kununua hisa. Bilioni 40 za Azam ni za kuonyesha mechi kwa miaka 10, hiyo ni biashara ya haki za TV, sio kwamba Azam wameingia kumiliki klabu. Mo anatoa Bilioni 20 plus ruzuku za kila mwaka kwa ajili ya kununua 49% tu ya hisa. Hata mkileta hao wawekezaji wengine watatu, hisa zao hazitazidi hiyo 49%. So, unataka Mo atoe bilioni 100 kwa hisa zisizompa maamuzi kamili? Thamani ya Simba ipo juu, lakini hisa zina kikomo chake.
Hebu rudia kusoma ulichoandika
 
Unachofeli ni kulinganisha mkataba wa biashara na kununua hisa. Bilioni 40 za Azam ni za kuonyesha mechi kwa miaka 10, hiyo ni biashara ya haki za TV, sio kwamba Azam wameingia kumiliki klabu. Mo anatoa Bilioni 20 plus ruzuku za kila mwaka kwa ajili ya kununua 49% tu ya hisa. Hata mkileta hao wawekezaji wengine watatu, hisa zao hazitazidi hiyo 49%. So, unataka Mo atoe bilioni 100 kwa hisa zisizompa maamuzi kamili? Thamani ya Simba ipo juu, lakini hisa zina kikomo chake.
Mo angekuwa anapata hasara angeiacha Simba ili waingie wawekezaji wapya. Tatizo la Mo anataka mchakato wa uwekezaji ukamilike huku yeye akiwa ni mwekezaji pekee kitu ambacho kwa Katiba ya sasa ya Simba hakiwezekani.
 
Mo angekuwa anapata hasara angeiacha Simba ili waingie wawekezaji wapya. Tatizo la Mo anataka mchakato wa uwekezaji ukamilike huku yeye akiwa ni mwekezaji pekee kitu ambacho kwa Katiba ya sasa ya Simba hakiwezekani.
Kwenye mpira wa Afrika hakuna faida ya moja kwa moja ya kifedha, Mo hawezi kuiacha Simba kwa sababu Simba inampa brand leverage na nguvu ya kisiasa kwenye biashara zake zingine za METL, hiyo ndio faida yake.

Halafu kwanini nyie Simba msibadili hiyo katiba ili iendane na uhalisia wa soko?
 
Huyu Mo keshaona Shabiki wa Simba ni misukule yake.

Kajinga sana haka ka kanjibai
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom