Wandugu, nimepata kipande kikubwa cha hotuba ya Lowassa ya kufungia Kampeni, kuna mambo mapya meengi saana atayaongea, ambayo nina uhakika yatamuongezeau kura nyiiingi saaana zilizokua zimebaki CCM.
Kwa ufupi kati ya hayo mambo ni yafuatayo;
1. Kulipa madeni yote ya ndani, kuanzia kwa watu binafsi, makampuni ya ndani na watumishi wa umma, wanoidai serikali, wakiwemo na wafanyakazi wa iliyokua jumuiya ya Africa Mashariki, (wale wazee), pia kuna watu wanaidai serikali kutokana na kuishinda serikali kwenye kesi mahakamani lakini hawajalipwa na serikali haina mpango wa kuwalipa.
Hatua hiyo, licha ya kwamba itamuongezea kura, itasaidia saana kunyanyua uchumi wa watanzania wengi.
2. Lowassa, anaahidi kuwalipa fidia (kuwarudishia fedha zao) wale wote walioathirika na upatu wa DECI, walipanda lakini hawakuvuna. Ikumbukwe kwamba fedha zao zilikamatwa na serikali ikazichukua, viongozi wao wakafungwa lakini serikali haijawarudishia fedha waathirika na wala haijasema imeweka wapi zile fedha ambazo zinakadiriwa kuwa zaidi ya Billioni 29.
3. Pia anawapa moyo na kuwaahidi watumishi wa umma, kwamba ajira zao katika utumishi wa Umma zitaendelea kuwa vile vile, mathalani kwa mfano wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu wakuu na manaibu makatibu wakuu, wakurugenzi wa halimashauri, wakurugenzi wa idara mbali mbali. Vyeo vyao vitaendelea kuwa kama kawaida, kama kubadirishwa itakua ni sababu yabutendaji na sio uhusiano wao na vyama.
Na mengine mengi subirini wenyewe kuisikiliza hotuba.
Nahisi hotuba ya hitimisho itamuongezea kura nyiingi saana Lowassa.