nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=1]Mastaa wa Bongo: [/h]
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo imempa ushindi msanii wa filamu za maigizo nchini, Elizabeth Michael Lulu, katika kesi ya kujadili upya umri wake. Akitangaza ushindi huo jaji aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Twalib Fauz, ameupa ushindi upande wa utetezi uliopeleka ombi la kuujadili upya umri wa msanii huyo na kuutupilia mbali umri wa miaka 18 alioandikisha kituo cha polisi baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba.