Author
JF-Expert Member
- Jan 24, 2014
- 1,709
- 8,007
Sina muda wa kueleza sana, nimechoka.
Mmeajiri madaktari vijana wanakaa wanapiga story tu vyumbani badala ya kuhudumia wagonjwa. Watu tumekaa zaidi ya lisaa tunasikia wanachekacheka tu ndani na hakuna mgonjwa.
Unaingia kwa daktari wamekaa kama watatu mmoja anakuhoji wengine wanakuangalia na kujifanya wanachezea simu. Kama mtu ana jambo la siri anaelezaje?
Sijawahi kuona Hospitali ina utaratibu mbovu kama hii, unafika reception mmewaweka vijana wa field wana dharau kama nini: wanaongea kama hawataki. Mtatupeleka kwa amri tu “njooni huku”, “kaa hapa” yaani kama mnatupa huduma bure.
Sintakaa nije kupata huduma kwenu tena.
=========
MAJIBU YA HOSPITALI YA K's
Akizungumzia tuhuma hizo, Suma Kabuje ambaye ni Afisa Mahusiano wa Hospitali ya K’s, amesema: "Taarifa hizo siyo za kweli, kwanza hatuna wanafunzi wa field kwa mwaka huu wote (2022), kuhusu madaktari wetu kila mtu ana chumba chake, unapomuona daktari chumba kingine basi ameenda kutoa msaada."
"Kwa leo wameingia madaktari wawili, daktari mmoja anamsaidia mwingine."
Kuhusu madai ya uwepo wa nzi wengi hospitalini hapo amesema: "Sehemu zetu ni safi na mazingira yetu hayana uchafu pia."
Mmeajiri madaktari vijana wanakaa wanapiga story tu vyumbani badala ya kuhudumia wagonjwa. Watu tumekaa zaidi ya lisaa tunasikia wanachekacheka tu ndani na hakuna mgonjwa.
Unaingia kwa daktari wamekaa kama watatu mmoja anakuhoji wengine wanakuangalia na kujifanya wanachezea simu. Kama mtu ana jambo la siri anaelezaje?
Sijawahi kuona Hospitali ina utaratibu mbovu kama hii, unafika reception mmewaweka vijana wa field wana dharau kama nini: wanaongea kama hawataki. Mtatupeleka kwa amri tu “njooni huku”, “kaa hapa” yaani kama mnatupa huduma bure.
Sintakaa nije kupata huduma kwenu tena.
=========
Akizungumzia tuhuma hizo, Suma Kabuje ambaye ni Afisa Mahusiano wa Hospitali ya K’s, amesema: "Taarifa hizo siyo za kweli, kwanza hatuna wanafunzi wa field kwa mwaka huu wote (2022), kuhusu madaktari wetu kila mtu ana chumba chake, unapomuona daktari chumba kingine basi ameenda kutoa msaada."
"Kwa leo wameingia madaktari wawili, daktari mmoja anamsaidia mwingine."
Kuhusu madai ya uwepo wa nzi wengi hospitalini hapo amesema: "Sehemu zetu ni safi na mazingira yetu hayana uchafu pia."