DOKEZO Hospitali ya K’s Mbeya mna huduma mbovu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Author

JF-Expert Member
Jan 24, 2014
1,709
8,007
Sina muda wa kueleza sana, nimechoka.

Mmeajiri madaktari vijana wanakaa wanapiga story tu vyumbani badala ya kuhudumia wagonjwa. Watu tumekaa zaidi ya lisaa tunasikia wanachekacheka tu ndani na hakuna mgonjwa.

Unaingia kwa daktari wamekaa kama watatu mmoja anakuhoji wengine wanakuangalia na kujifanya wanachezea simu. Kama mtu ana jambo la siri anaelezaje?

Sijawahi kuona Hospitali ina utaratibu mbovu kama hii, unafika reception mmewaweka vijana wa field wana dharau kama nini: wanaongea kama hawataki. Mtatupeleka kwa amri tu “njooni huku”, “kaa hapa” yaani kama mnatupa huduma bure.

Sintakaa nije kupata huduma kwenu tena.

IMG_1780.jpg


=========
MAJIBU YA HOSPITALI YA K's
Akizungumzia tuhuma hizo, Suma Kabuje ambaye ni Afisa Mahusiano wa Hospitali ya K’s, amesema: "Taarifa hizo siyo za kweli, kwanza hatuna wanafunzi wa field kwa mwaka huu wote (2022), kuhusu madaktari wetu kila mtu ana chumba chake, unapomuona daktari chumba kingine basi ameenda kutoa msaada."

"Kwa leo wameingia madaktari wawili, daktari mmoja anamsaidia mwingine."

Kuhusu madai ya uwepo wa nzi wengi hospitalini hapo amesema: "Sehemu zetu ni safi na mazingira yetu hayana uchafu pia."
 
Sina muda wa kueleza sana, nimechoka.

Mmeajiri madaktari vijana wanakaa wanapiga story tu vyumbani badala ya kuhudumia wagonjwa. Watu tumekaa zaidi ya lisaa tunasikia wanachekacheka tu ndani na hakuna mgonjwa.

Unaingia kwa daktari wamekaa kama watatu mmoja anakuhoji wengine wanakuangalia na kujifanya wanachezea simu. Kama mtu ana jambo la siri anaelezaje?

Sijawahi kuona Hospitali ina utaratibu mbovu kama hii, unafika reception mmewaweka vijana wa field wana dharau kama nini: wanaongea kama hawataki. Mtatupeleka kwa amri tu “njooni huku”, “kaa hapa” yaani kama mnatupa huduma bure.

Sintakaa nije kupata huduma kwenu tena.

View attachment 2447438
Dawa ni kuacha kwenda hapo ili wale ujinga wao
 
Mh! Hosptl karibia zote za serikali kwa sasa ukihudumiwa ukatoka umefurahi shukuru sana Mungu. Zingine unaenda saa 2 asbh unatoka saa 5 au saa 6 mchana kwa case ndogo tu hasa vituo vya afya. Wagonjwa wachache ila wahudumu wanawapita tu kama vijisanam.
Najiuliza, hawa wahudumu kweli wana hofu ya Mungu!? Hivi kweli wakati wanasomea fani walikuwa wakimwomba Mungu awasaidie kufikia malengo yao ili waje wasaidie watu!!? If yes, hivi ndivyo wanavyorudisha fadhila kwa Mungu!!!? Duh! Haya jaman!
dawa ni kuacha kwenda hapo ili wale ujinga wao
Usipoenda wanajisifu hawana wagonjwa, ko kwao inakuwa full bata tu, na ndo nia yao kutoa huduma mbovu usivutiwe ili siku nyingine usiendepo na usishauri mtu mwingine aendepo.
 
Hiyo ni hospitali ya kifamilia ya Dr Kanama, kaweka pale watoto wake ambao hawajielewi, inabidi hao watoto wa dr kanama waende wakasome kwa watoto wa dr kairuki uendeshaji wa hospitali ya Baba, wenzao wa dr kairui wamefanikiwa kusimamia hospitali ya baba yao hadi kuanzisha chuo kikuu na kiwanda cha madawa
 
Ni kukosa maadili, tabia mbaya, ya hovyo na ya kipuuzi sana madaktari au manesi wasiohusika na mgonjwa kuingia consultation room wakati mgonjwa yuko na daktari wake.
 
Back
Top Bottom